STD IV SAYANSI ONLINE NECTA EXAM REVIEW FOR YEAR 2011

SAYANSI 2011

SEHEMU A  

Chagua jibu sahihi na andika herufi yake kwenye karatasiya kujibia

1.Tunapaswa kuoga kila siku ili  . . . . . . . . .

  1. kuchangamsha mwili na kuondoa magonjwa
  2. kuondoa harufu mbaya na kuzuia imagemagonjwa ya ngozi
  3. kupendeza na kuonekana nadhifu
  4. kunukia vizuri na kupendeza sana
Chagua Jibu


2 Inatupasa kuepuka kula vyakula vinavyosababisha meno kuoza: Mfano wa vyakula hivyo ni  . . . . . . . . .

  1. peremende, machungwa na ndizi
  2. peremende, biskuti na mananasi
  3. peremende, keki na biskuti
  4. peremende, keki, biskuti na maziwa
Chagua Jibu


3. Vifuatavyo ni baadhi ya vyakula vyenye protini  . . . . . . . . .

  1. Nyama, maharage, samaki na mayai
  2. Maharage, ndizi samaki na wali
  3. Samaki, nyama, kunde na mhogo
  4. Ndizi, maharage, mayai na nyama
Chagua Jibu


4. Vifuatavyo ni vyanzo vya umeme isipokuwa  . . . . . . . . .

  1. jenereta 
  2.  jua
  3. sufuria 
  4. betri
Chagua Jibu


5. Kifaa kinachotumika kupimia vimiminika kama vile maji na mafuta ya taa huitwa  . . . . . . . . .

  1. Themometa 
  2. Silinda kipimo
  3. Barometa 
  4. Pima maji
Chagua Jibu


6. Vishikio vya pasi, vikaangio na masufuria hutengenezwa kwa mbao ili kuvifanya  . . . . . . . . .

  1. vipendeze
  2. viwe vyepesi
  3. visiunguze mikono
  4. visiharibike upesi
Chagua Jibu


7 Mtu anayeota moto hupata joto kwa njia  . . . . . . . . .

  1. mnunurisho na msafara
  2. mpitisho na mnunurisho
  3. myuko na mpitisho
  4. mgandamizo wa hewa
Chagua Jibu


8. Ni kundi lipi la vitu vifuatavyo vinaelea kwenye maji? . . . . . . . . .

  1. Meli, mpira na kijiko
  2. Meli, boti na msumari
  3. Mpira, boti na sindano ya kushonea 
  4. Boti, mpira na kipande cha ubao
Chagua Jibu


9. Zifuatazo ni sifa zinazomwezesha mnyama kuruka  . . . . . . . . .

  1. Mifupa yenye hewa, mabawa na mwili uliochongoka
  2. Mabawa, mwili uliochongoka na mwili nwororo
  3. Mwili mwororo, mifupa yenye hewa na mwili uliochongoka
  4. Mabawa, mwili mwororo na mwili uliochongoka
Chagua Jibu


10. Mojawapo kati ya makundi yafuatayo ya wanyama hutaga mayai  . . . . . . . . .

  1. Kuku, popo na mamba
  2. Bata, chura na mbwa
  3. Kuku, bata na mbu
  4. Popo, kinyonga na kuku
Chagua Jibu


SEHEMU B

Jaza nafasi zilizoachwa wazi

11. Joto husafiri kwa njia zipi? . . . . . . . . . . . . . . . na . . . . . . . . . . . . . . .image

Fungua Jibu


12. Taja milango ya fahamu . . . . . . . . . . . . . . .image

Fungua Jibu


13. . . . . . . . . . . . . . . . katika ramani huelezea kwa kifupi kile kilichokusudiwa kuoneshwa katika ramani.

Fungua Jibu


14. Ni njia gani ambayo joto husafiri na kufikia maji yaliyoko kwenye birika katika mchoro hapo chini?

Fungua Jibu


15. Virusi vya UKIMWI (VVU) daima hushambulia chembe chembe  . . . . . . . . . . . . . .  za damu.

Fungua Jibu


16. Jua ni chanzo kikuu cha  . . . . . . . . . . . . . .  duniani.

Fungua Jibu


17. Mwanga husafirishwa katika mstari  . . . . . . . . . . . . . .  

Fungua Jibu


SEHEMU C

Andika Kweli au Si Kweli

18. Maji siyo sehemu ya mlo kamili . . . . . . . . . .

Fungua Jibu


19. Sumaku huvuta vitu vilivyotengenezwa kwa chuma au shaba . . . . . . . . .

Fungua Jibu


20. Katika nyenzo daraja la pili, mzigo upo kati ya jitihada na egemeo . . . . . . .

SEHEMU D

Fungua Jibu


Oanisha maneno ya Fungu A na Fungu B ili kupata jibu sahihi

 FUNGU A

 FUNGU B

.

21. Taswira

22. Nguo za hariri

23. Husababisha upofu kwa watoto wachanga

24. Ogani inayotusaidia kutambua harufu

25. Hutumika katika kitendo cha usanisi wa chakula

  1. Kaswende
  2. Hutokana na manyoya ya kondoo
  3. Husharabu sauti
  4. Oksijeni
  5. Matokeo ya kupinda kwa mwanga
  6. Kabonidayoksaidi
  7. Hutokana na buu wa nondo
  8. Kisonono
  9. Huakisi sauti
  10. Matokeo ya kuakisi mwanga
  11. Pua
  12. Ngozi
Fungua Jibu


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256