SAYANSI 2011
SEHEMU A
Chagua jibu sahihi na andika herufi yake kwenye karatasiya kujibia
1.Tunapaswa kuoga kila siku ili . . . . . . . . .
- kuchangamsha mwili na kuondoa magonjwa
- kuondoa harufu mbaya na kuzuia
magonjwa ya ngozi - kupendeza na kuonekana nadhifu
- kunukia vizuri na kupendeza sana
Chagua Jibu
2 Inatupasa kuepuka kula vyakula vinavyosababisha meno kuoza: Mfano wa vyakula hivyo ni . . . . . . . . .
- peremende, machungwa na ndizi
- peremende, biskuti na mananasi
- peremende, keki na biskuti
- peremende, keki, biskuti na maziwa
Chagua Jibu
3. Vifuatavyo ni baadhi ya vyakula vyenye protini . . . . . . . . .
- Nyama, maharage, samaki na mayai
- Maharage, ndizi samaki na wali
- Samaki, nyama, kunde na mhogo
- Ndizi, maharage, mayai na nyama
Chagua Jibu
4. Vifuatavyo ni vyanzo vya umeme isipokuwa . . . . . . . . .
- jenereta
- jua
- sufuria
- betri
Chagua Jibu
5. Kifaa kinachotumika kupimia vimiminika kama vile maji na mafuta ya taa huitwa . . . . . . . . .
- Themometa
- Silinda kipimo
- Barometa
- Pima maji
Chagua Jibu
6. Vishikio vya pasi, vikaangio na masufuria hutengenezwa kwa mbao ili kuvifanya . . . . . . . . .
- vipendeze
- viwe vyepesi
- visiunguze mikono
- visiharibike upesi
Chagua Jibu
7 Mtu anayeota moto hupata joto kwa njia . . . . . . . . .
- mnunurisho na msafara
- mpitisho na mnunurisho
- myuko na mpitisho
- mgandamizo wa hewa
Chagua Jibu
8. Ni kundi lipi la vitu vifuatavyo vinaelea kwenye maji? . . . . . . . . .
- Meli, mpira na kijiko
- Meli, boti na msumari
- Mpira, boti na sindano ya kushonea
- Boti, mpira na kipande cha ubao
Chagua Jibu
9. Zifuatazo ni sifa zinazomwezesha mnyama kuruka . . . . . . . . .
- Mifupa yenye hewa, mabawa na mwili uliochongoka
- Mabawa, mwili uliochongoka na mwili nwororo
- Mwili mwororo, mifupa yenye hewa na mwili uliochongoka
- Mabawa, mwili mwororo na mwili uliochongoka
Chagua Jibu
10. Mojawapo kati ya makundi yafuatayo ya wanyama hutaga mayai . . . . . . . . .
- Kuku, popo na mamba
- Bata, chura na mbwa
- Kuku, bata na mbu
- Popo, kinyonga na kuku
Chagua Jibu
SEHEMU B
Jaza nafasi zilizoachwa wazi
11. Joto husafiri kwa njia zipi? . . . . . . . . . . . . . . . na . . . . . . . . . . . . . . .![image](https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1598594467_sayansi-2011_files/image079.jpg)
Fungua Jibu
12. Taja milango ya fahamu . . . . . . . . . . . . . . .![image](https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/1598594467_sayansi-2011_files/image079.jpg)
Fungua Jibu
13. . . . . . . . . . . . . . . . katika ramani huelezea kwa kifupi kile kilichokusudiwa kuoneshwa katika ramani.
Fungua Jibu
14. Ni njia gani ambayo joto husafiri na kufikia maji yaliyoko kwenye birika katika mchoro hapo chini?
![](https://myfiles.space/user_files/30996_4958b541bbe404eb/30996_custom_files/img1598595390.png)
Fungua Jibu
15. Virusi vya UKIMWI (VVU) daima hushambulia chembe chembe . . . . . . . . . . . . . . za damu.
Fungua Jibu
16. Jua ni chanzo kikuu cha . . . . . . . . . . . . . . duniani.
Fungua Jibu
17. Mwanga husafirishwa katika mstari . . . . . . . . . . . . . .
Fungua Jibu
SEHEMU C
Andika Kweli au Si Kweli
18. Maji siyo sehemu ya mlo kamili . . . . . . . . . .
Fungua Jibu
19. Sumaku huvuta vitu vilivyotengenezwa kwa chuma au shaba . . . . . . . . .
Fungua Jibu
20. Katika nyenzo daraja la pili, mzigo upo kati ya jitihada na egemeo . . . . . . .
SEHEMU D
Fungua Jibu
Oanisha maneno ya Fungu A na Fungu B ili kupata jibu sahihi
FUNGU A | FUNGU B |
. 21. Taswira 22. Nguo za hariri 23. Husababisha upofu kwa watoto wachanga 24. Ogani inayotusaidia kutambua harufu 25. Hutumika katika kitendo cha usanisi wa chakula | - Kaswende
- Hutokana na manyoya ya kondoo
- Husharabu sauti
- Oksijeni
- Matokeo ya kupinda kwa mwanga
- Kabonidayoksaidi
- Hutokana na buu wa nondo
- Kisonono
- Huakisi sauti
- Matokeo ya kuakisi mwanga
- Pua
- Ngozi
|
Fungua Jibu