KISWAHILI STANDARD SEVEN REGIONAL EXAMS (MOCK, PRE-NATIONAL, etc.)
OFISI YA RAIS - TAWALA ZA MIKOA NA SERIKAKI ZA MITAA, HALMASHAURI YA WILAYA YA UVINZA

 

MTIHANI WA KUJIANDAA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI - 2023

SOMO: KISWAHILI DARASA: VII MUDA: SAA 1:40 

MAELEKEZO:

  • Mtihani huu una maswali 45
  • Jibu maswali yote kama ulivyoelekezwa  

SEHEMU A

Sikiliza habari itakayosomwa na msimamizi kisha jibu maswali yanayofuata kwa kuchagua herufi ya jibu sahihi

1. Habari hii inahusu nini? _______

A. umoja B. Tanzania C. utamaduni D. wageni E. ulaya [       ]

2. Nchi gani inasifika kuwa na ukarimu?

A. Asia B. Ulaya C. Amerika D. Tanzania E. India [       ]

3. Ni vipengele vipi vya utamaduni vimetajwa katika habari hii? _______

A. amani na desturi B. upendo na mila C. amani na upendo D. upendo E. mila na desturi [       ]

4. Wageni wanaotoka Tanzania hutoka katika jamii za nchi gani? ______ 

A. Ulaya tu B. wenyeji wa Tanzania C. Umerika asia na Ulaya D. Uganda na Ulaya E. Asia tu [       ]

5. Kichwa cha habari hii cha faa kiwe ______

A. Mila B. Desturi C. Utamaduni D. Umoja E. Amani [       ]

 Katika swali la 6 – 35 chagua herufi ya jibu sahihi kisha iandike kwenye mabano uliyopewa.

6. Katika maneno yafuatayo ipi ni nomino ya dhahani? ________

A. unakuja B. umeenia C. utalima D. uelewe E. ulisoma

7. Neno lipi ni tofauti na mengine?_____ 

A. embe B. chungwa C. ndizi D. ng’ombe E. papai [       ]

8. “Nitatetema kama Mayele” Kiambishi cha njeo katika neno nitatetema ni kipi? _____

A. nita B. -ta C. te D. –a- E. tema [       ]

9. Walimu walifundisha masomo vizuri. Sentensi hii ipo katika wakati gani? ____ 

A. uliopita B. ujao C. uliopo D. mazoea E. usiodhihirika [       ]

10. Neno “paka” lina silabi ngapi? _____ 

A. mbili B. nne C. tano D. moja E. sita [       ]

11. Umoja wa neno nyaraka ni _________

A. waraka B. nyaraka C. miwaraka D. wawaraka E. kanyaraka [       ]

12. Hadi sasa hakuna mtu_________ aliyekamatwa kuhusika na wizi. 

A. yoyote B. wowote C. yeyote D. yote E. vyovyote [       ]

13. Mahali ambapo anaishi Rais wa nchi huitwa? _______

A. nyunbani B. makao ya Rais C. ikulu D. ngome E. banda [       ]

14. Neno “kitongoji” lina konsonati ngapi? _______ 

A. moja B. mbili C. tano D. tatu E. kumi [       ]

15. Wahenga walisema “hakuna marefu yasiyokuwa na ncha” nini maana ya methali hii? ______

A. hakuna kitu kisicho kirefu B. hakuna kitu kisicho na ncha C. hakuna jambo lenye mwanzo mrefu

D. hakuna jambo lisilokuwa na mwisho E. hakuna marefu yasiyokuwa na mafupi [       ]

16. “Angeliamka” mapema asingeliachwa na ndege. Kipi ni kiambishi cha masharti katika sentensi hii? _______

A. –a- B. –nge- C. –ngeli- D. angel E. –ili- [       ]

17. Mzee Juma ameishi Morogoro ____miaka kumi. 

A. toka B. kwa C. tangu D. kipindi E. tangia [       ]

18. Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo lipo katika kundi la majina?_______ 

A. mlimani B. peponi C. mweusi D. utoto E. kwaya [       ]

19. Kama ungeliimba vizuri _____ zawadi.

A. ungelipewa B. ungepewa C. ungalipewa D. ungapewa E. ukipewa [       ]

20. Kitabu chako ni kizuri ukienda dukani nami ninunulie ________. Ni kifungu kipi cha maneno kinakamilisha sentensi hiyo? ___ 

A. kama hivyo B. kama hiko C. kama hicho D. kama iko E. kama icho [       ]

21. John husafisha eneo lake mpaka muda wa kuingia darasani unapowadia. Neno wadia lina maana gani? ___

A. kuwasili B. kuisha C. kufika D. kusogea E. rejea [       ]

22. Kila mtu atalipitia darasa hili apende asipende. Darasa hili ni lipi ? ________ 

A. kifo B. elimu ya msingi C. elimu ya awali D. dini E. semina [       ]

23. Mzee Mpili alizunguka mbuyu, nini maana ya nahau zunguka mbuyu? _______ 

A. kutoa rushwa B. kupiga rushwa C. kupokea rushwa D. kuleta rushwa E. kula rushwa [       ]

24. Mihogo iliyotoka Kidahwe haipikiki, imekaa sana. Neno lililopigiwa mstari liko katika kauli gani ya utendaji?__

A. Kutendeana B. Kutendewa C. Kutenda D. Kutendana E. Kutendeka [       ]

25. Asha anapia uvivu maana yake maneno yaliyopigiwa mstari ni ______ 

A. kutabili kazi B. kula uvivu C. kukaa raha  D. kuamka na uvivu E. kukaa huku ukifanya kazi [       ] 

26. __________________ mbele kiza. Methali hii inakamilishwa na maneno yapi kati ya haya yafuatayo?

A. Usiku B. Ujinga mwingi C. Werevu mwingi D. Ubishi mwingi E. Upendo [       ]

27. Malizia methali hii. “Mwenda tezi na omo ________” 

A. ni mnafiki B. marejeo ngamani C. hafai kwenye raha D. uakufa naye E. hufaidi siku ya iddi [       ]

28. “Gari lile liliendeshwa na mdogo wangu.” Hii ni kauli ya ______ 

A. kutendeka B. kutendewa C. kutenda D. kutendwa E. kutendana [       ]

29. Tegua kitendawili kisemacho Kondoo wetu ana nyama nje ngozi ndani. ________ 

A. Nywele na kichwa B. Katani C. Uyoga D. Chungwa E. Filigisi [       ]

30. Siwema ni msichana mzuri lakini ana mkono wa birika. Maana ya nahau iliyokolezwa ni ipi? _____

A. Mchoyo B. Mwizi C. Muongo D. Kusengenya E. Msahaulifu [       ]

31. Tegua kitendawili hiki “bomu la machozi baridi” _______

A. nywele B. moshi C. miguu D. ngozi E. gesi [       ]

32. Maana ya nahau “kufa moyo” ni ipi ? _______

A. kufariki B. kuugua sana C. kuchoka sana D. fia ndani ya moyo E. kukata tama [       ]

33. Samaki mkunje angali mbichi. Methali ipi kati ya hizi ina maana sawa na hii ? ______ 

A. samaki huanza kuoza kichwani B. ukitaka riba ziba C. jino la pembe si dawa ya pengo D. sikio la kufa halisikii dawa E. ngozi ivute ingali maji [       ]

34. Methali ipi haifanani na zingine kati ya hizi? ________

A. sikio la kufa halisikii dawa B. chombo cha kuzama hakina usukani C. siku ya kufa nyani miti yote huteleza D. maji yakimwagika hayazoleki [       ]

35. Maana ya “fuja mali” ni ________

A. kuiba mali B. kutumia mali ovyo C. kuhifadhi mali D. kutumia mali kibali E. kuitumia mali [       ]

 SEHEMU B: UTUNGAJI

 Panga sentensi zifuatazo katika mfuatano sahihi kwa kizipa herufi A, B, C, D na E.

36. Zima taa ulale, kuna radi sana. [       ]

37. Nilikuwa chumbani kwangu nikisoma kitabu cha hadithi. [       ]

38. Ilikuwa ni wakati wa usiku. [       ]

39. Mara nilimsikia baba akiniita, Bura! Bura! [       ]

40. Siku hiyo kulikuwa na mvuya kubwa iliyoambatana na radi. [       ]

SEHEMU C: USHAIRI - Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yafuatayo Ukiwepo darasani, mwalimu msikilize,

Kisichotiwa mizani, angalia usimeze, 

Kilopita kipimoni, ndicho ukitekeleze, 

Elimu ni ufunguo, kila mtoto sikia.

Mazoezi darasani, yatakufanya uweze,

La kufanya akilini, kuchagua ipendeze, 

Uzio ubaini, jamii usipumbaze,

Elimu ni ufunguo, kila mtoto sikia.

MASAWALI

41. Shairi hili lina jumla ya beti ngapi? ......................................................................

42. Taja vina vya mwisho katika ubeti wa kwanza . . . . . . . . . . . . . . . . . . ...

43. Kila ubeti wa shairi hili una mishororo mingapi? ....................................................

44. Ubeti wa pili una mizani mingapi? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

45. Mstari unaojirudiarudia katika kila ubeti unaitwaje? . . . . . . .. ... . . . . . . . .




HABARI YA KUSOMA

Utamaduni ni mfumo wa maisha ya watu na jinsi wanavyoishi na taratibu zao za kijamii, kiuchumi na kisiasa. Tanzania ni moja ta kati ya nchi zinazosifika duniani kwa ukarimu, amani na upendo kwa wageni, licha ya kuwa na makabila zaidi ya mia moja na ishirini ambayo yote hutunza mila na desturi zao, watanzania wanaishi kwa umoja, upendo na mshikamano. Hali hiihuwavutia watu wa mataifa mengine na wengine na wengine hupenda kuishi Tanzania.

Wageni hawa hutoka katika jamii za nchi tofauti zikiwemo zile za Asia, Ulaya na Amerika.

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 21  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 21  

 JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA  OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

 HALMASHAURI YA MANISPAA YA UBUNGO

 MTIHANI WA UTAMILIFU KATA 
 KISWAHILI DARASA LA SABA – MACHI, 2023

 MUDA: SAA 1:30

 MAELEKEZO 

  1. Mtihani huu una maswali arobaini na tano (45) tu.
  2. Jibu maswali yote
  3. Soma maelekezo kwa kila kurasa uliyopewa
  4. Kumbuka kuandika Jina lako, Namba yako ya mtihani na Jina la shule yako katika karatasi ya kujibia.
  5. Tumia penseli ya HB tu.
  6. Simu hazihitajiki katika chumba cha mtihani.

SEHEMU A: UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Sikiliza kwa makini habari utakayosomewa na msimamizi kisha jibu swali 1- 5 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu sahihi katika fomu yako ya kujibia. 

1. Kutokana na habari uliyoisikiliza, ni nani aliyezungumziwa?

(A) Amani (B) Bibi (C) Wananchi (D) Bibi na Amani (E) Kilole [     ]

2. Amani alimuuliza swali gani bibi yake? 

(A) kama unajua kusoma na kuandika (B) kama unajua kuandika (C) kama unajua kusoma (D) kama unajua kuimba na kuandika (E) kama unajua kuimba [     ]

3. Amani anaishi katika kijiji cha Kilole. Je, Amani anaishi na nani?

(A) Bibi (B) Babu (C) Shangazi (D) Mjomba (E) Babu na bibi [     ]

4. Kwa mujibu wa habari uliyoisikiliza. Amani ana tabia gani?

(A) mvivu (B) mdadisi (C) mkarimu (D) mchapakazi na mdadisi (E) mpole [     ]

5. Kichwa cha habari hii kinafaa kiwe kipi miongoni mwa hivi?

(A) kijiji cha Kilole (B) Amani (C) Amani na bibi yake (D) Kilole (E) Bibi [     ]

Katika Swali la 6 – 35 weka kivuli katika herufi ya jibu sahihi 

6. Neno machweo lina maana ipi kati ya hizi zifuatazo?

(A) wakati jua linapozama (B) wakati jua linapochomoza (C) wakati jua linapokuwa la utosi

(D) wakati jua linapokuwa kati (E) wakati jua linapokuwa pembeni [     ]

7. “Kazi mbaya si mchezo mwema” methali inayofanana na methali hii ni ipi kati ya hizi zifuatazo?

(A) hewala haigombi (B) mchezea tope humrukia (C) mcheka kivu asiyefikwa na jeraha (D) lila na fila havitengamani (E) mcheza kwao hutunzwa [     ]

8. Wanafunzi wale wanapenda kucheza mpira. Katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kivumishi? 

(A) wanafunzi (B) wale (C) wanapenda (D) mpira (E) kucheza [     ]

9. Katika lugha ya Kiswahili neno “staftahi” lina silabi ngapi?

(A) sita (B) tano (C) nne (D) tatu (E) saba [     ]

10. “Ukitaka kuruka agana na nyonga”. Sentensi hii iko katika aina gani ya sentensi kati ya hizi?

(A) sahihi (B) ambatano (C) changamano (D) tegemezi (E) shurutia [     ]

11. Ipi ni maana ya kitedawili “nyumba yangu imeungua mwamba wake umebaki”

(A) mfupa (B) njia (C) kaburi (D) kisima (E) mlima [     ]

12. Kuwa na nyota ya jaha maana yake ni___________ 

(A) jua la mchana (B) nyota ya asubuhi (C) bahati nzuri (D) bahati mbaya (E) bahati nasibu [     ]

13. Wewe ni mtoto mdogo sana. Sentensi hii iko katika nafsi gani?

(A) ya kwanza umoja (B) ya pili umoja (C) ya tatu wingi (D) ya pili wingi (E) ya kwanza umoja na wingi [     ]

14. Watu hufanya kazi mbalimbali ili kuweza kujipatia kipato. Mtu anayefanya kazi ya kutunza na kuazima vitabu maktaba anaitwa Mkutubi. Je! mtu anayefanya kazi ya kuzibua vyoo anaitwa nani? 

(A) kuli (B) topasi (C) toinyo (D) chepe (E) zubaifu [     ]

15. Bwana Afya aliuliza, kuna umuhimu gani wa kuchemsha maji ya kunywa? Je! sentensi hii iko katika kauli ipi kati ya zifuatazo? 

(A) taarifa (B) halisi (C) tata (D) tungo huru (E) kutenda [     ]

16. Asha ana gari. Neno “ana” ni aina gani ya neno?

(A) kitenzi (B) nomino (C) kiunganishi (D) kielezi (E) kihusishi [     ]

17. Baba amelima shamba kubwa sana. Silabi inayoonesha nafsi ni ipi?[     ]

(A) –li– (B) –a– (C) –me– (D) –i– (E) –lim–[     ]

18. Ngumi  zilipigika vilivyo, Neno lililopigiwa mstari lipo katika kauli gani?

(A) kutenda (B) kutendewa (C) kutendwa (D) kutendeka (E) kutendesha [     ]

19. __________ Kamilisha methali ifuatayo. Akikalia Kigoda

(A) huanguka (B) usimtukane (C) mtii (D) mfukuze (E) harudi [     ]

20. _______________ Ali anakula wali maharage.

(A) na (B) kwa (C) ni (D) ya (E) pamoja [     ]

21. Simba mkali amepita shuleni kwetu. Mchanganuo wa sentensi hii ni upi kati ya michanganuo ifuatayo? 

(A) T+N+V+W+E (B) N+E+V+T+W (C) V+E+T+W+N (D) N+V+T+E+V (E) N+V+E+T+V [     ]

22. ________ Kinyume cha methali isemayo; “Ngoja ngoja yaumiza matumbo” ni

(A) bendera hufuata upepo (B) mtu hujikuna hajipatiapo (C) mwisha hadhuru maiti (D) haraka haraka haina Baraka (E) asiyesikia la mkuu huvunjika guu [     ]

23. ______ Wakoloni walitunyanyasa lakini hatimaye unyanyasaji huo ulifika ukingoni kwani Ni methali ipi kati ya zifuatazo inamalizia sentensi hii?

(A) hakuna marefu yasiyokuwa na ncha (B) mchumia juani hulia kivulini (C) ukiona vyaelea ujue vimeundwa (D) umoja ni nguvu utengano ni udhaifu (E) bandubandu humalia gogo [     ]

24. Kazi ya Daudi ni kazi ya kijungujiko. Je! kazi ya kijungujiko ni kazi ya aina gani?

(A) kazi ya kuchimba vyoo (B) kazi ya kujitolea (C) kazi ya kufundisha wanafunzi (D) kazi isiyo rasmi au inayotosha mahitaji ya mlo tu (E) kazi ya kikoa [     ]

25. Ikiwa mzizi wa neno “PIK” tukiunda neno litakalokuwa katika wakati uliopita nafsi ya kwanza
umoja hali ya kutenda tunapata neno.

(A) alipika (B) nilipika (C) walipika (D) tulipika (E) nimepika [     ]

26. Akikosekana maana inakosekana. Jibu la kitendawili hiki ni lipi?

(A) kitabu (B) kamusi (C) magazeti (D) shairi (E) vipeperushi [     ]

27. Mashairi ya kimapokeo yamegawanyika katika aina mbalimbali. Je ubeti wa shairi wenye mistari minne huitwaje?

(A) mshororo (B) tarbia (C) kituo (D) kibwagizo (E) mizani [     ]

28. _______ Mnyama ambaye amekuwa laini bado hajazaa anaitwa

(A) mtamba (B) mbuguma (C) maksai (D) fahali (E) beberu [     ]

29. Nenda ukawasikilize watakachokueleza uniletee mrejesho. Katika sentensi hii mtenda ni nafsi ya ngapi? 

(A) ya kwanza umoja (B) ya pili umoja (C) ya tatu wingi (D) ya kwanza wingi (E) ya pili wingi [     ]

30. _______________________ Ali ni askari kanzu. Ali ni 

(A) trafiki (B) kanga (C) bunduki (D) mpelelezi (E) askari mwenye cheo cha juu [     ]

31. Jambazi alihukumiwa kwa kuua mfanyabiashara. Sentensi hii iko katika hali gani?

(A) hali timilifu (B) hali ya kuendelea (C) hali isiyodhihirika (D) hali ya mazoea (E) hali tata [     ]

32. Tungo changamano ni tungo yenye vishazi vingapi?

(A) vitatu (B) viwili (C) vinne (D) vitano (E) kimoja [     ]

33. _______ Kisawe cha jogoo ni jimbi, kisawe cha beseni ni karai. Je kisawe cha kinyonga ni

(A) bombo (B) hua (C) lumbwi (D) kelbu (E) baghala [     ]

34. Katika neno anacheza. Kipi ni kiambishi njeo?

(A) –a– (B) –na– (C) –chez– (D) –a– (E) –cheza– [     ]

35. Lipi kati ya maneno yafuatayo si kivumishi likiambatanishwa na nomino?

(A) Yule (B) nzuri (C) polepole (D) huyo (E) hawa [     ]

 SEHEMU B:

 Panga sentensi zifuatazo kwa kuzipa herufi A – E ili zilete maana kamili kwa kujibu swali la 36 – 40 kwa kuweka kivuli katika herufi ya jibu lililo sahihi

36. Niliogopa lakini nilipiga moyo konde  [    ]

37. Nilirudi nyuma kidogo nikaokota fimbo na kumpiga   [    ]

38. Jumamosi iliyopita mama alinituma sokoni   [    ]

39. Nilipokuwa njiani nilimwona nyoka   [    ] 

40. Aliniambia ninunue nyanya, vitunguu, sukari na mafuta   [    ]


 SEHEMU C: 

 Soma habari ifuatayo kisha jibu maswali yafuatayo 

Masebo ni mwalimu anayefundisha katika shule ya Msingi Maendeleo iliyoko wilaya ya Masasi. Anakaa katika kitongoji cha usafi kilichopo umbali wa kilometa tano kutoka shuleni. Siku moja mwalimu Masebo alikuwa anakwenda shuleni. Pembezoni mwa msitu wa kijiji aliwaona vijana watatu, vijana hao walikuwa wakikata miti kwa kutumia mapanga na mashoka na kuivundika pembeni. Aliwatambua vijana hao kuwa ni Juma, Sadiki na Joseph. Mwalimu Masebo alisikitika sana. Alisimamisha pikipiki yake haraka na kwenda katika eneo lile. Alianza kuwafokea vijana wale kwa kukata miti mingi kiasi kile. Vijana wale walishangaa sana.

 Maswali 

41. Juma, Sadiki na Joseph walikuwa wanafanya nini msituni?

42. Mwalimu Masebo aliona nini pembezoni mwa msitu wa kijiji?

43. Je! ukikuta watu wanaoharibu mazingira utafanya nini?

44. Kwa nini mwalimu Masebo alisikitika sana?

45. Kwa nini tunashauriwa kutokata miti ovyo?



UFAHAMU WA KUSIKILIZA

Amani anaishi na bibi yake katika kijiji cha Kilole. Anamsaidia bibi yake shughuli za nyumbani. Anamsaidia kusafisha nyumba, kupika, kuosha vyombo na kufua. Juzi Amani alimuuliza bibi yake; bibi unajua kusoma? Bibi akajibu ninajua kusoma na kuandika. Amani akasema sawa bibi, kesho nitaleta kitabu changu ili tusome pamoja.



STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 3  

STANDARD SEVEN KISWAHILI EXAM SERIES 3  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256