HISTORIA STANDARD FOUR REGIONAL EXAMS (MOCK, PRE-NATIONAL, etc.)

JAMHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA, OFISI YA RAIS TAWAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA UPIMAJI DARASA LA NNE

 A07 HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

Muda: Saa 1:30 Mwaka: 2025

Maelekezo 

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali sita (6)
  2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.
  3. Andika majibu katika nafasi zilizotolewa katika kila swali.
  4. Majibu yote yaandikwe kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au mweusi.
  5. Vifaa vya mawasiliano na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha upimaji
  6. Andika Jina lako, Namba ya Upimaji, Mkoa na Halmashauri katika sehemu ya juu ya kila ukurasa.
KWA MATUMIZI YA MPIMAJI TU
NAMBA YA SWALI ALAMA SAINI YA MPIMAJI
1.

2.

3.

4.

5.

6.

JUMLA

SAINI YA MHAKIKI

SEHEMU A (Alama 20)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

1. Jibu vipengele (i) - (x) kwa kuchagua jibu sahihi na kuandika herufi yake katika kisanduku ulichopewa.

(i) Misingi ya ukuzaji na utunzaji wa maadili katika jamii za Kitanzania kabla ya ukoloni ilisisitiza mambo gani? [     ]

  1. Uwazi, upendo, umoja na teknolojia
  2. Uadilifu, haki, usawa na uwazi
  3. Haki, hekima umoja na utajiri
  4. Uadilifu, nidhamu, teknolojia na haki

(ii) Njia gani ilitumika kufundisha maadili katika jamii za kale? [     ]

  1. Maonesho
  2. Mahojiano
  3. Masimulizi
  4. Majadiliano

(iii) Siku rasmi ya soko kwa ajili ya kununua na kuuza bidhaa baina ya jamii za Kitanzania kabla ya ukoloni iliitwaje?

  1. Soko
  2. Maonesho
  3. Gulio
  4. Mnada

(iv) Ugunduzi wa madini gani ulichochea kukua na kuimarika zaidi kwa shughuli za uzalishaji mali kabla ya ukoloni? [     ]

  1. Chuma
  2. Shaba
  3. Chumvi
  4. Dhahabu

(v) Shughuli gani za kiuchumi husaidia kujenga uhusiano mwema katika jamii?[     ]

  1. Biashara, ufugaji na uwindaji
  2. Kilimo, muziki na ufugaji
  3. Ufugaji, kilimo na uvuvi
  4. Uwindaji, kilimo na michezo

(vi) Ili watoto wakue katika maadili mema, wazazi wanapaswa kufanya nini? [     ]

  1. A Kuwapatia kila wanachotaka
  2. B Kuwafanyia kazi za nyumbani
  3. C Kuwapeleka shule za gharama
  4. D Kutenda matendo mema

(vii) Elimu ya maadili na afya ya uzazi kwa vijana iliyotolewa kabla ya ukoloni ilijulikana kama [     ]

  1. A unyago na ususi.
  2. B ufinyanzi na jando.
  3. C ususi na uhunzi.
  4. D jando na unyago.

(viii) Mtoto wa kaka wa mama yako anaitwaje? [     ]

  1. Binamu
  2. Kaka
  3. Dada
  4. Shangazi

(ix) Uhusiano mzuri baina ya ndugu au jamaa wa karibu unajengwaje? [     ]

  1. Kutembeleana wakati wa raha tu
  2. Kutembeleana mara kwa mara
  3. Kuandikiana barua kila wakati
  4. Kutembeleana wakati wa shida tu

(x) Bainisha njia mojawapo ya kujenga uhusiano wa kirafiki uwapo nyumbani au shuleni [     ]

  1. Kuandikiana barua
  2. Kupigiana simu
  3. Kucheza pamoja
  4. Kupeana pesa

2. Jibu vipengele (i) – (v) kwa kuoanisha maelezo kuhusu majukumu ya viongozi mbalimbali wa shule katika Orodha A na mfumo wa uongozi katika ngazi ya shule katika Orodha B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi kwenye mabano uliyopewa.

Orodha A

Herufi

Orodha B

(i) Husimamia mambo ya taaluma na nidhamu za wanafunzi shuleni. [     ]
  1. Kiranja wa shule
  2. Kamati ya Shule
  3. Mwalimu Mkuu
  4. Msaidizi
  5. Mwalimu wa Taaluma
  6. Mwalimu Mkuu
  7. Walimu
  8. Mwalimu wa Michezo
(ii) Hufuatilia maadili na taaluma shuleni katika ngazi mbalimbali. [     ]
(iii) Huongoza wanafunzi wengine katika kukuza na kutunza maadili mema. [     ]
(iv) Hukuza, hutunza na husimamia maadili ya wanafunzi na walimu shuleni. [     ]
(v) Huratibu mitihani ya ndani na kupanga ratiba ya masomo shuleni. [     ]

3. Jibu vipengele (i) - (v) kwa kuchagua jibu sahihi katika mabano na kuliandika katika sehemu iliyoachwa wazi.

(i) Wazazi wanawahimiza watoto wao kuzingatia usafi wa mwili, nguo na vyombo ili kuepuka nini? _____________________________________ (Ukorofi, Magonjwa, Uvivu)

(ii) Kuwahi shuleni na kuwepo darasani kwa wakati humuwezesha mtoto kuepuka nini? ______________________________________________ (Ukaidi, Adhabu, Utukutu)

(iii) Unashauriwa kufanya nini ukiona mtoto mwenzio anafanyiwa vitendo vibaya? __________________________________________________________ (Kuondoka haraka, Kutoa taarifa, Kujificha)

(iv) Tabia ipi humaanisha utayari wa kutekeleza amri za viongozi shuleni? _________________________________________________________ (Upole, Ucheshi, Utii)

(v) Tabia ipi humaanisha kukiuka maagizo na ushauri wa wazazi au walezi? _________________________________________________________ (Ukatili, Utukutu, Ubinafsi)

SEHEMU B (Alama 18)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

4. Chunguza kielelezo kifuatacho cha mti wa familia kisha jibu maswali katika vipengele (i) - (v)

image

(i) Familia inayoonekana katika mchoro huo inaundwa na jumla ya watu wangapi? _______________________________________________________.

(ii) Uhusiano wa Baba na Mama katika familia hiyo unaitwaje? _______________________________________________________.

(iii) Juma anamuita jina gani Asha linalowakilisha uhusiano wao kama wanafamilia? _______________________________________________________.

(iv) Asha na Juma wanawaita jina gani Baba na Mama linalowakilisha uhusiano wao kama wanafamilia? ____________________________.

5. Chunguza kwa makini picha ifuatayo, kisha jibu maswali yanayofuata.

image

Maswali

(a) Ni shughuli gani inayofanywa na watu wanoonekana katika picha? ________________________________________________________

(b) Ni kifaa gani kinatumika katika shughuli inayoonekana katika picha? ________________________________________________________

(c) Ni mbinu gani itakayowezesha mazao yanayoonekana katika picha kustawi wakati wa ukame utokanao na uhaba wa mvua? ________________________________________________________

(d) Vitu gani viwili vitawezesha mazao yanayoonekana katika picha kukua na kustawi?

(i) _____________________________________________________

(ii) _____________________________________________________

(e) Faida zipi zinatokana na mavuno ya mazao yanayoonekana katika picha? Taja faida mbili

(i) _____________________________________________________

(ii) _____________________________________________________

SEHEMU C (Alama 12)

Jibu swali la sita (6)

6. Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho, kisha jibu maswali katika vipengele (a) – (f) kwa kuandika jibu lililo sahihi katika sehemu zilizoachwa wazi.

Jamii za kale zilitumia dawa za asili kutibu magonjwa mbalimbali. Dawa za asili zilitokana na vitu vya asili kama mimea. Dawa hizo zilitayarishwa kwa kutumia maarifa na ujuzi wa asili. Maarifa na ujuzi wa asili ulizingatia maadili katika utayarishaji na matumizi ya dawa. Maadili yaliyozingatiwa katika utayarishaji ni usafi. Dawa zilitayarishwa kwa njia za asili kama kuchemshwa, kupondwa, kutwangwa na kusagwa. Usafi ulizingatiwa katika njia zote hizo.

Maadili yaliyosisitizwa katika matumizi ya dawa ni kuzingatiwa maelekezo ya matumizi ya dawa. Maadili ya kuzingatia maelekezo ya matumizi ya dawa yalisisitizwa ili kuepuka madhara yanayoweza kusababishwa na matumizi yasiyo sahihi ya dawa. Maelekezo ya matumizi ya dawa yalitolewa na watu wenye maarifa na ujuzi wa kutayarisha dawa hizo.

Maswali

(a) Jamii za kale zilitumia dawa za asili kufanya nini? _________________________________________________________

(b) Dawa za asili zilitokana na nini? _________________________________________________________

(c) Maadili gani yalizingatiwa katika utayarishaji wa dawa? _________________________________________________________

(d) Njia zipi zilitumika katika kutayarisha dawa za asili. Taja njia mbili

(i) ____________________________________________________

(ii) ____________________________________________________

(e) Maelekezo ya matumizi ya dawa yalitolewa na watu wenye sifa ipi? _________________________________________________________

(f) Kwa nini maadili ya kuzingatia maelekezo ya dawa yalisisitizwa? _________________________________________________________

STANDARD FOUR HISTORIA EXAM SERIES 64  

STANDARD FOUR HISTORIA EXAM SERIES 64  

Jina la mwanafunzi ________________________
Namba ya upimaji____________________
Mkoa____________________________
Halmashauri___________________

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

 HALMASHAURI YA MANISPAA YA KINONDONI 

MTIHANI WA UPIMAJI  DARASA LA NNE 

 A07   HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI  

 Muda: Saa 1 Mwaka: 2025 

 Maelekezo kwa mtahiniwa 

  1. Mtihani huu una sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali sita(6)
  2. Jibu maswali yote kama ulivyoelekezwa katika kila sehemu.
  3. Majibu yote yaandikwe kwenye nafasi ulizopewa katika mtihani.
  4. Epuka kufuta kufuta.
  5. Simu za mkononi, karatasi zisizohusika na vitabu haviruhusiwi kaika chumba cha mtihani.
  6. Kumbuka kuandika jina lako, namba ya upimaji, mkoa na halmashauri kila ukurasa kwenye sehemu uliyopewa upende wa juu kulia.
 KWA MATUMIZI YA MTAHINI TU 
 NAMBA YA SWALI   ALAMA   SAHIHI YA MTAHINI 
 1.  
 
 2.  

 3.  

 4.  

 5.  

 6.  

 JUMLA 

  SEHEMU A: (ALAMA 20)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake kwenye kisanduku kwa kila kipengele (i)-(x)

(i) Hali ya kupiga hatua mbele au kuongeza kitu kutoka kiwango cha chini kwenda cha juu huitwaje? 

  1. Ujima
  2. Ukabaila
  3. Umwinyi
  4. Maendeleo

(ii) Mifano ipi inaeleza stadi za elimu kabla ya ukoloni?

  1. Uhunzi, ususi na uporaji
  2. Ufugaji, uvuvi na ujenzi
  3. Ususi, ufugaji na uvuvi
  4. Kilimo, uvuvi na ujangili

(iii) Kwanini elimu wakati kabla ya ukoloni ilitolewa kwa lugha ya jamii husika?

  1. Kupinga ukoloni
  2. Kujua vitu vya muhimu pekee
  3. Kuelewa maarifa kwa urahisi
  4. Kuwaficha watoto wasijue yanayoendelea

(iv) Shughuli ya ususi ilichangiaje maendeleo ya jamii kabla ya ukoloni?

  1. Kuhifadhi mazao na vyombo
  2. Kupata utajiri
  3. Kuonesha ufahari
  4. Kupata sifa kwa watu

(v) Teknolojia ya chuma ilisaidia vipi maendeleo ya kilimo?

  1. Zana za chuma zilirahisisha kilimo
  2. Chuma ilitumika kama zawadi kwa wakulima
  3. Chuma ilikuwa inalimwa
  4. Chuma ilipelekea wakulima na wafugaji wagombane

(vi) Katika utunzaji wa mazingira, jamii iliweka sheria gani ili kutunza mazingira kabla ya ukoloni?

  1. Kutowinda wanyama na kukata miti ovyo
  2. Kulima karibu na vyanzo vya maji
  3. Kulisha wanyama ovyo kwenye vyanzo vya maji
  4. Kukata miti sana

(vii) Miongoni mwa maadili yaliyokuwa yanazingatiwa kwa wataalamu wa sayansi asilia kabla ya ukoloni ilikuwa ni___

  1. Kuwapa zawadi kila muda
  2. Kuwaheshimu na kuwajali
  3. Kuwa karibu nao mara kwa mara
  4. Kuwa nao mbali

(viii) Jamii ipi kati ya hizi ilitengeneza mavazi kwa kutumia magome ya miti na ngozi za wanyama?

  1. Wahaya
  2. Wazaramo
  3. Wapare
  4. Wazigua

(ix) Eneo maarufu kwa kilimo cha umwagiliaji kabla ya ukoloni ni lipi kati ya haya?

  1. Umatumbi
  2. Engaruka
  3. Kilwa kivinje
  4. Olduvai

(x) Ni teknolojia ipi ya asili ya kuhifadhi samaki ilikuwa ikitumika hapo kale?

  1. Friji
  2. Kemikali maalum
  3. Kukausha kwa moto na kuweka chumvi
  4. Kuchemsha sana na kutia Magadi mengi

2. Oanisha maneno kutoka Orodha A na yale ya Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi kwenye sehemu uliyopewa.

Orodha A

Majibu

Orodha B

(i) Dini [    ]
  1. Maziwa, mabwawa na mito.
  2. Kuabudu katika miti mikubwa na mapango.
  3. Ukatili kwa watoto.
  4. Wajibu wa mtoto
  5. Upendo na chuki
  6. Vitendo vya heshima
  7. Kutoamini uwepo wa mizimu.
(ii) Kupewa kazi kinyume na umri wako [    ]
(iii) Shughuli za uvuvi [    ]
(iv) Kusaidia kazi ndogo ndogo za nyumbani [    ]
(v) Kusalimia na kuongea lugha nzuri [    ]

3. Chagua jibu kutoka kwenye kisanduku kisha liandike kwenye nafasi zilizoachwa wazi.

  China, Litti, Mkwawa, Mirambo, Mangi sana, Machemba, Ushujaa wa vita, Ujerumani

(i) Chifu wa jamii za wahehe kabla ya ukoloni ___________________________________

(ii) Mtemi wa jamii za wanyaturu kabla ya ukoloni _______________________________

(iii) Mtemi wa wanyamwezi kabla ya ukoloni ___________________________________

(iv) Njia mojawapo ya kupata uongozi hapo kale_______________________________

(v) Jamii nyingi zilipambana na wavamizi kutoka wapi?__________________________

SEHEMU B: (ALAMA 18)

Jibu maswali yote kutoka sehemu hii.

4. Soma mchoro ufuatao kisha jibu maswali yanayofuata.

image

Maswali

(a) Mchoro huo hapo juu unawakilisha nini?

_________________________________________________________________

(b) Kiongozi gani wa shule anahakikisha wanafunzi wanafuata sheria za shule?

_________________________________________________________________

 (c) Ni ngazi ipi inahusika kuhakikisha wanafunzi wenzao wanafuata sheria za shule?

_________________________________________________________________

(d) Ni nani anahakikisha darasa lake linakuwa na maadili?

_________________________________________________________________

5. Soma picha ifuatayo kisha jibu maswali.

image

Maswali

(i) Vitu unavyoviona pichani kwa jina moja huitwaje?

______________________________________________________

(ii) Ni wageni kutoka maeneo gani walileta vitu hivyo pichani?

______________________________________________________

(iii) Nini matumizi ya vitu hivyo?

______________________________________________________ 

(iv) Ni aina gani ya urithi unaoonekana pichani?______________________________________________________

(v) Ni urithi gani mwingine ulioletwa na watu walioleta vitu vinavyoonekana hapo pichani?

______________________________________________________

SEHEMU: (ALAMA 12)

Jibu swali la sita (6) 

6. Sentensi zifuatazo zimechanganywa haziko katika mtiririko wenye kuleta mantiki. Zipange sentensi hizo kwa kuzipa herufi A-F ili kupata habari yenye kuleta mantiki kuhusu familia.

(i) Uhusiano huo ni wa asili kwani mtu hujikuta tu yupo katika familia fulani na watu fulani.

(ii) Baada ya mtu kuwa na ndugu hao, anapaswa atambue kuwa baba na mama ni viongozi wa familia.

(iii) Vile vile, anapaswa kujua na kutambua mchango wa kila mwanafamilia ili kuwa na familia yenye upendo.

(iv) Familia ni uhusiano wa damu uliopo baina ya watu fulani.

(v) Hivyo anapaswa awaheshimu na kuwajali kwa kila hali kwani ni sababu ya yeye kupatikana. 

(vi) Katika kujikuta huko, mtu huwa ana baba, mama, kaka na dada zake katika familia husika.

STANDARD FOUR HISTORIA EXAM SERIES 50  

STANDARD FOUR HISTORIA EXAM SERIES 50  

Jina la Mwanafunzi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

Shule . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAIS UTAWALA WA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA 

MKOA WA DODOMA 

MTIHANI WA MUHULA DARASA LA NNE

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI [06E]

MUDA : Saa 1:30 2025

MAELEKEZO:

  1. Mtihani huu una maswali sita (6) yenye sehemu A na B
  2. Jibu maswali yote kwenye sehemu zote
  3. Andika majibu yote katika nafasi ulizopewa
  4. Majibu yote lazima yaandikwe kwa kutumia kalamu ya wino mweusi au bluu.
  5. Simu za mkononi au nyenzo yoyote hairuhusiwi katika chumba cha mtihani.
  6. Andika jina na namba ya mtihani katika kila ukurasa wa mtihani huu.
KWA MATUMIZI YA WATAHINI TU
Namba ya Swali Alama Sahihi ya Mtahini Sahihi ya Mhakiki
1.


2.


3.


4.


5.


6.


JUMLA


SEHEMU A: (ALAMA 26)

1. Chagua herufi ya jibu sahihi kisha ujaze kwenye kisanduku ulichopewa

i. Kitendo cha kutoa au kupokea kitu chochote kwa lengo la kupewa upendeleo katika jambo fulani au kupata huduma fulani huitwaje? [      ]

A. Zawadi C. Nidhamu B. Rushwa D. Msaada

ii. Tanzania ni nchi iliyoundwa na mataifa mawili; Tanganyika na Zanzibar. Ni lini muungano wan chi hizo ulifanyika?

A. 9/12/1961 C. 14/10/1999 B. 26/12/1964 D. 26/4/1964

iii. Ipi miongoni mwa tabia zifuatazo huonyesha kitendo cha heshima?

  1. Kumpisha mkubwa kukalia kiti kwenye gari 
  2. Kukataa kuagizwa na mkubwa wako 
  3. Kucheza na wanyama
  4. Kutumia lugha mbaya

iv. Katika historia ya Tanzania, Ni mreno gani wa kwanza kuingia pwani ya Afrika Mashariki?

  1. Mwl. J.K. Nyerere 
  2. Dr. Louis Leakey 
  3. Vasco da Gama
  4. Sultan Seyyid Said

v. Kitu chochote ambacho mtu anastahili kupewa huitwaje?

A. Haki C. Mali B. Wajibu D. Majukumu

2. Oanisha maelezo yaliyopo kwenye orodha A na majibu yaliyopo kwenye orodha B, na kisha uandike herufi ya jibu sahihi kwenye chumba ulichopewa.

ORODHA A MAJIBU ORODHA B
(i) Majengo ya zamani yaliyobaki kama sehemu ya historia na utamaduni.
  1. Makavanzi
  2. Makumbusho
  3. Masimulizi
  4. Maeneo ya kiakiolojia
  5. Magofu

(ii) Sehemu ambapo nyaraka na taarifa mbalimbali za kihistoria huhifadhiwa.
(iii) Maeneo yanapopatikana masalia ya mambo ya kale na utamaduni wa mwanadamu.
(iv) Maeneo yanayotumiwa kuhifadhi vitu vyenye historia na urithi wa kiasili na kiutamaduni.

3. Chagua jibu sahihi kutoka kwenye kisanduku kasha jibu maswali yanayofuata;

Kaole, Zanzibar, Olduvai Gerge, Zinjanthropus, Link

(i) Mji palipogundulika mabaki ya Dinosaria wa Tendaguru.

image

(ii) Sehemu ambapo lipo jengo la maajabu ambalo lina historia ya kuwa jengo la kwanza kuwekwa lifti za umeme.

image

(iii) Eneo lilipogunduliwa fuvu la Binadamu wa kale na Dr. Louis Leakey.

image

(iv) Jina lilopewa fuvu la binadamu wa kale lililogunduliwa mwaka 1959.

image

(v) Mji yanapopatikana magofu ya msikiti na kituo cha kuhifadhia watumwa.

image

SEHEMU B: (ALAMA 24)

4.  Ainisha matendo yafuatayo kwa kusoma maelezo yake na kuweka alama ya vema (√) katika chumba sahihi. Kipengele cha tano (v) kimefanywa kama mfano kwa ajili yako.

Kitendo

Kitendo cha kimaadili

Kitendo kisicho cha kimaadili

(i) Kupigana na wenzako



(ii) Kusalimia watu wakubwa



(iii) Kushirikiana na watu wengine



(iv) Kuwatukana watu wazima



(v) Kumsaidia mzee kubeba mizigo


5.  Tazama picha hizi kwa makini kasha jibu maswali yanayofuata

Maswali

i. Mwanamke aliyeoneshwa katika picha A anafanya nini?

image

ii. Mwanaume anayeonekana kwenye picha B anafanya nini?

image

iii. Jamii ya mtu aliyeoneshwa kwenye picha B hupendelea kula chakula gani.

image

iv. Aina ya nguo aliyoivaa mtu aliyeoneshwa kwenye picha B inaitwaje?

image

6. Soma habari ifuatayo kasha ujibu maswali yanayofuata;

Jamii za Tanzania hapo Kale zilifanya biashara na wafanyabiashara kutoka Mashariki ya Mbali na ya Kati. Nchi hizo ni India, Irani, Iraki, Kuwait, China na Saud Arabia. Biashara hii ilifanyika katika miji iliyopo katika mwambao wa Pwani ya Bahari ya Hindi kama vile Dar es Salaam, Bagamoyo, Tanga, Kilwa na Zanzibar. Biashara hizi zilifanyika kwa kubadilishana bidhaa. Bidhaa kubwa katika biashara hii kutoka nchini ilikuwa dhahabu na pembe za ndovu. Dhahabu ilitoka Zimbabwe kupitia bandari ya Sofala, Msumbiji. Kutoka kwa wageni kuja nchini, bidhaa kubwa zilikuwa shanga na vyombo vya ndani kama vile mabakuli na sahani za udongo. Baadhi ya mabaki ya bidhaa hizi yapo katika Makumbusho hapa nchini, kama vile makumbusho ndogo iliyopo Kaole, Bagamoyo.

Maswali

(i) Mabaki ya bidhaa zilizotumika katika biashara na watu wa Mashariki ya mbali zimehifadhiwa wapi?

image

(ii) Taja bidhaa mbili zilizokuwa zinaletwa kutoka kwa wageni?

image

(iii) Tja nchi mbili za Mashariki ya mbali zilizotajwa kwenye habari hii?

image

(iv) Taja miji miwili iliyopo katika Mwambao wa Pwani

image


STANDARD FOUR HISTORIA EXAM SERIES 48  

STANDARD FOUR HISTORIA EXAM SERIES 48  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256