OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
MTIHANI WA NUSU MUHULA - KIDATO CHA NNE
015 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU
(Kwa watahiniwa walioko na wasiokuwa shuleni)
Maelekezo
SEHEMU A (Alama 16)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
1. Katika kipengele (i) – (x), chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake katika kijitabu chako cha kujibia.
i) Kwanini Waislamu wa leo wanapaswa kuipa elimu kipaumbele?
ii) Umeombwa kuwaelezea wanafunzi wenzio kuhusu historia ya madhehebu ya Ki-Fiqh. Utachagua yapi kati ya haya kutekeleza jambo hilo?
iii) Kosa gani walilofanya watu wa Madyan tu ambalo hadi sasa linafanywa?
iv) Mwalimu amekusimamisha useme ulichojifunza kutokana na maandalizi ya kimafunzo ya Mtume wa mwisho. Utasema lipi kati ya haya yafuatayo?
v) Bwana Mbundu ni mwanasayansi anayetaka kuanzisha mfumo wa maisha utakaowasaidia watu wote kuishi kwa raha kwa kutumia ujuzi wake, lakini akaambiwa hawezi kufanya hivyo. Kwanini bwana huyu asiweze?
vi) Kwa ujumla kanuni zinazotumika kuweka sheria za Kiislamu hujulikana kwa jina gani?
vii) Bwana Ngugu ametokewa na jambo fulani mchana wa Ramadhani lakini
akaambiwa funga yake haijaharibika. Bwana huyu ametokewa na nini?
viii) Muandaaji wa sanda ya mtoto wa kike anapaswa kuzingatia jambo gani kati ya haya?
(ix)
Nuun Sakna ) ((ن au (Tan wiin) inapokutana na Qaaf yenye fat-ha inapatikana hukumu gani?
x) Bwana Ng’ombo anamiliki mbuzi na mbuzi 40. Baada ya kupinduka mwaka nini anapaswa kutoa kama Zakat katika hiki alichonacho?
2. Oanisha maelezo ya shahada yaliyo katika Oradha A na aina za shahada zilizo katika Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihih katika kijitabu chako cha kujibia.
| ORODHA A | ORODHA B |
|
|
SEHEMU B (ALAMA 54)
Jibu maswali yote katika sehemu hii
Jibu maswali yote katika sehemu hii. Andika majibu yako kwa ufupi na ufasaha.
3. Wewe kama Muislamu unapaswa kuvifanyia nini viungo vyako vifuatavyo?
4. Tumia hoja tatu kuwafafanulia wanajamii wa mtaani kwako ni kwa namna gani mahari inaweza kushusha hadhi ya mwanamke?
5. Umekutana na vijana watatu wanaotetea sheria zilizotungwa kwenye mabunge mbalimbali kuwa hazina kasoro.
6. Wayahudi walifanya jitihada kubwa ya kuuzima Uislamu Madinah kwa kufanya vitimbi mbalimbali dhidi ya Dola na Waislamu. Wewe kama khatibu wa Ijumaa wafahamishe Waumini wa msikitini hapo mambo sita hayo ili waweze kuchukua tahadhari na wanaofanana na hao.
7. Umekaribishwa katika mjadala wa wasioamini siku ya mwisho kwa kutoa hoja zao mbalimbali. Wathibitishie ulazima wa kuwepo siku hiyo kwa kuwabainishia hoja tatu ili waondokane na fikra yao hiyo potofu.
8. Katika jamii ya Waislamu wapo watu wasiokubali ukhalifa wa Khalifa wa kwanza kwa kutokana na mitazamo tofauti juu ya uchaguzi wake. Tumia hoja mbili madhubuti kuwafafanulia waislamu hao mitazamo hiyo ili wasije kuingia kwenye makosa.
SEHEMU C (Alama 30)
Jibu maswali mawili (2) kutoka sehemu hii
9. Miongoni mwa hoja wanazozitumia wasio waislamu katika kuichafua Qur’an ni kudai kuwa ni kitabu cha mashairi ya Mtume Muhammad (Sallallahu Alayhi Wasallam). Toa hoja nne kuwadhihirishia watu hawa kuwa wanachokidai si sahihi.
10. Umealikwa kutoa semina kwa mahujaji watarajiwa juu ya utekelezaji wa ibada ya Hijjah. Waambie namna watakavyoweza kufikia kumpenda Allah kikwelikweli kwa kupitia utekelezaji wa ibada hiyo? (Hoja tano)
11. Mwalimu ameingia darasani kufundisha usahihi wa hadith za Mtume Muhammad (Sallallahu Alayhi Wasallam) kwa kuangalia matini yake. Atatumia hoja gani kuelezea mada hii? (Hoja tano)
FORM FOUR EDK EXAM SERIES 244
FORM FOUR EDK EXAM SERIES 244