FORM TWO HISTORIA TERMINAL EXAMS

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA 

MTIHANI MUHULA WA KWANZA KIDATO CHA PILI 

060 HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI 

Muda: Masaa 2:30 Mei 2026 

MAELEKEZO

  1. Mtihani huu una sehemu tatu (3) A, B na C).
  2. Jibu maswali yote katika Sehemu A na B, na swali moja kutoka Sehemu C.
  3. Sehemu “A” ina alama 15, sehemu “B” ina alama 70, na sehemu “C” ina alama 15
  4. Andika namba yako ya mtihani katika kila ukurasa wa karatasi yako ya kujibia.
  5. Tumia kalamu ya wino wa bluu au mweusi kujibu maswali yote.
  6. Fuata maelekezo yote ya mtihani kwa makini.

SEHEMU A (ALAMA 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

1. Chagua jibu sahihi katika vipengele (i) – (x) kisha andika herufi ya jibu sahihi kwenye jedwali ulilopewa hapo chini.

i. Mzee Mpenda Ukweli alitaka kujua ni kwanini wanafunzi katika shule za Tanzania wanasoma somo la Historia ya Tanzania. Alipowauliza kidato cha pili walimpa jibu lifuatalo:

  1. Linafundisha zaidi mambo ya kisiasa pekee.
  2. Linafundisha maadili ya mataifa jirani.
  3. Ili kuelewa dini zetu za jadi zenye miungu wengi.
  4. Ili kuelewa mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi, na kiutamaduni, tulikotoka, tuliko na tuendako.

ii. Mwanafunzi Juhudi alisoma kuhusu vyama vya ushirika vya wakulima vilivyo anzishwa kabla ya uhuru. Je vyama hivyo vilikua na lengo gani?

  1. A.Kufundisha watu kujiamini. 
  2. B. Kujifunza uvumilivu.
  3. Kuwasaidia wakulima kupata bei nzuri na haki zao.
  4. Kujifunza ujasiliamali.

iii. Katika makundi ya jamii za asili zaTanzania, ni kundi moja tu ambao ndio wazawa wa Tanzania waliokutwa na jamii nyingine. Kundi hilo ni:

  1. Wakichembe 
  2. Wabantu 
  3. Wanilo 
  4. Wakushito

iv. Msichana aitwaye Elizabeth aliambiwa na mwalimu ataje vitendo vyenye maadili ambavyo hutendwa na wanafunzi wenzake awapo shuleni. Majibu aliyotoa ni haya yafuatayo isipokuwa:

  1. Husaidiana katika masomo ili nifaulu vizuri.
  2. Hushauriana pale inapohitaji.
  3. Huhimizana kuwahi shuleni.
  4. Kugawana vitafunwa wakati wa mapumziko

v. Kwa mujibu wa wanafalsafa mbalimbali, neno 'Jamii' lina maana gani?

  1. Ni mkusanyiko wa watu wanaoishi pamoja na kushirikiana.
  2. Ni mkusanyiko wa baba, mama na Watoto.
  3. Ni mkusanyiko wa wanaume na wanawake.
  4. Ni muunganiko ya familia mbalimbali.

vi. Mkutano wa kimataifa uliofanyika nchini Ujeruman katika mji wa Berlin mwaka 1884-1885 ukiongozwa na Otto Von Bismark ulifanyika kwa lengo gani?

  1. Kuanzisha mashindano ya Ulaya
  2. Kukuza uchumi kwa bara la Afrika
  3. Kugawanya bara la Afrika na Mataifa ya Ulaya
  4. Kugawanya bara la Afrika kwa mataifa ya Ulaya

vii. Ni aina gani ya elimu ilikuwa ikitolewa katika jamii za Kitanzania kabla ya ujio wa kikoloni?

  1. Elimu rasmi katika shule. 
  2. Elimu ya kilimo cha jadi pekee.
  3. Elimu isiyo rasmi kupitia mafunzo ya familia.
  4. Elimu isiyo rasmi madarasani katika shule.

viii. Wakati Wajerumani na Waingereza wanaitawala Afrika mashariki walitoa huduma ya elimu kwa waafrika. Hii ilikua na maana gani?

  1. Waafrika waliwaomba kufanya hivyo
  2. Waafrika waliwaajiri wazungu kufundisha watoto wao
  3. Wajerumani na waingereza walihitaji kuwaandaa waafrika ili wawatumie katika ngazi za chini za uongozi.
  4. Wajerumani na waingereza waliwapenda waafrika na kuwazawadia elimu

ix. Ashura anawadharau wenzake kwasababu wanatoka familia masikini. Kitendo cha Ashura kuwa na tabia hii kinakiuka maadili yapi kati ya haya yafuatayo?

  1. Ujasiri na ukarimu. 
  2. Utu na heshima.
  3. Utii wa sheria za jadi. 
  4. Utii wa mila na desturi.

x.…..ni hali ya mtu au nchi kuamua na kufanya mambo yake bila kuingiliwa na mtu au taifa lolote.

  1. Uhuru 
  2. Uzalendo 
  3. Maadili 
  4. Harakati

Majibu

i ii iii iv v vi vii viii ix x









.

2. Oanisha maelezo yaliyopo katika Orodha Ana dhana zilizopo katika Orodha Bkwa kuandika herufi ya jibu sahihi.

Orodha A

Orodha B

  1. Uadilifu
  2. Utu
  3. Umoja
  4. Lugha ya taifa
  5. Uzalendo
  1. Kurahisisha mawasiliano ya watu wa taifa kwa sababu inaunganisha watu wa Tanzania.
  2. Kuheshimiana na kujali hali za wengine kwa kuwasaidia na kutunza haki za binadamu.
  3. Unaunganisha watu wa Tanzania kutoka makabila, dini na utamaduni tofauti
  4. Inahusu watu kuwa waaminifu na nidhamu
  5. Watu wa Tanzania wanavyotambua haki za kila mtu mbele ya sheria
  6. Inahusu upendo wa watu kwa nchi yao

Majibu

Orodha A i ii iii iv v
Orodha B




SEHEMU B (ALAMA 70)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

3. a) Eleza maana ya dhana “Mfumo wa ukoo”

b) Taja na eleza kwa kifupi sifa kuu nne (04) zilizozingatiwa ili mtu ateuliwe kuwa kiongozi wa ukoo.

4. Ujenzi wa maadili katika jamii sio tukio la siku moja bali kuna mifumo mbalimbali ya kijamii inayosaidia. Fafanua mifumo ya kijamii inayohusika kujenga maadili kabla ya ujio wa wakoloni katika jamii za kitanzania

5. Tunapaswa kufahamu kuwa ujio wa wakoloni uliathiri nyanja nyingi katika jamii za kitanzania hivyo jamii nyingi za kiafrika zilipinga ili kuhifadhi na kulinda maadili, uchumi, utawala na tamaduni zao. Eleza sababu zilizosababisha mapinduzi matukufu ya Zanzibar.

6. Jamii za asili ya kitanzania zilihama kutoka sehemu na kwenda maeneo mengine kutokana na sababu mbalimbali. Mueleweshe mwanafunzi wa kidato cha kwanza sababu hizo. Hoja tano

7. Ukiwa kama mwanafunzi wa kidato cha pili na mbobezi wa somo la Historia ya Tanzania na Maadili. Elezea utofauti wa mfumo wa elimu ya jadi na mfumo wa elimu ya sasa. Hoja tano

8. Katika mapambano dhidi ya uvamizi wa wakoloni, jamii za Kitanzania zililenga kulinda maadili yao. Bainisha maadili ya jamii za kitanzania yaliyodumu licha ya ushawishi wa utawala wa kikoloni kuyafuta. Hoja tano.

9. Taja na eleza kifupi mbinu zilizotumika kudai uhuru wa Tanganyika na Zanzibar katika kipindi cha kwanza kwanzia mwaka1900 mpaka 1944. Hoja tano (05)

SEHEMU C (ALAMA 15)

Jibu swali namba 10

10. Tanzania ina utajiri mkubwa wa urithi wa asili, ambao huwapa manufaa makubwa wanajamii na Taifa kwa ujumla. Waeleweshe watanzania umuhimu huo kwa kutumia aina mbalimbali za urithi wa asili

FORM TWO HISTORIA EXAM SERIES 253  

FORM TWO HISTORIA EXAM SERIES 253  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256