FORM THREE KISWAHILI MIDTERM-2 EXAMS

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MITIHANI YA KUJIPIMA KWA SEKONDARI 

                           MTIHANI WA NUSU MUHULA WA PILI

KISWAHILI KIDATO CHA TATU

 

MUDA: MASAA 3                                                                         AUG 2023

 

MAELEKEZO

1.      Karatasi hii ina sehemu A, B na C

2.      Jibu maswali yote sehemu A na B na maswali 2 sehemu C

3.      Zingatia maelekezo ya kila swali

 

SEHEMU A (ALAMA 16) JIBU MASWALI YOTE.

1. Chagua jibu sahihi katika vipengele (i-x) kisha andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi ya kujibia.

i.      Huyu ni mwanafunzi hodari sana. Je “ni” ni aina gani ya neon.

a)      Kitenzi shirikishi

b)      Kiunganisha

c)      Kitenzi kisaidizi

d)      Kielezi cha wakati

 

ii.      Njia ipi ni ya uhifadhi wa fasihi simulizi inayoweza kupokea mabadiliko kwa haraka kati ya hizi

a)      Maandishi

b)      Vinasa sauti

c)      Kichwa                                     (d)Kanda za video

 

iii.      Tofauti ndogondogo zinazojitokeza katika lugha moja huitwa

a)   Kimtang’ata

b)  Lugha za kikanda

c)   Lahaja

d)  Kiimbo

 iv.      Wazo kuu la mtunzi katika kazi ya fasihi huitwa

a)      Ujumbe

b)      Dhamira

c)      Falsafa

d)      Mtazamo

v.      -------------- ni maneno yasiyo sanifu yayozuka na kutoweka

a)      Misimu

b)      Rejesta

c)      Msamiati

d)      Kishazi tegemezi

vi.      Kisawe cha neno umaskini

a)      Ukwasi

b)     Ubahili

c)      Ujima

d)     Ukata vii. Ni neno pamoja na taarifa zake kwenye kamusi huitwa

a)      Kidahizo

b)      Kitomeo

c)      Msamiati

d)      Muundo

viii.      Utofauti wa kazi za kifasihi toka muandishi mmoja dhidi ya mwingine husababishwa na 

a)      Mtindo wa kazi

b)      Dhamira za kazi za fasihi

c)      Migogoro ya kazi husika

d)      Muundo wa kazi ya fasihi

 ix.      Moja ya sifa kuu ya kirai ni 

a)      Kukaa sehemu yeyote katika sentensi 

b)      Hakina muundo wa kiima na kiarifu

c)      Hutoa maana kamili

d)      Huwa na muundo wa kiima na kiarifu

x.      Neon lipi kati ya maneno haya linaweza kudokeza mtenda au mtendwa wa jambo

a)      Kiunganishi

b)      Kihisishi

c)      Kielezi

d)      Kivumishi

2.      (a) Oanisha dhana katika orodha A kwa kuchagua herufi ya dhana husika kutoka orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi ya kujibia. 

 

ORODHA A

ORODHA B

I.   Tungo shurutia

II.   Kosa la mpangilio mbaya wa viambishi

III.   Maneno yasiyo sanifu yanayozungumzwa na kikundi kidogo cha watu

IV.  Viambajengo vya sentensi

V.    Sehemu ya nchi kavu iliyochongoka na kuingia baharini

VI.  siataimba

A.    Ghubu

B.     Mpegani

C.     Ukanushi

D.    Anampigia pasi

E.     Rasi

F.      Ukimwonw ndani ya gari utamlipia nauli

G.    Kiima na kiarifu

H.    Simo

I.        Misemo

J.       jakabu

 

 

 

SEHEMU B (ALAMA 54)

 

3.      Wewe ni mwanafunzi wa shule ya sekondari Mazinyungu iliyopo Morogoro.

Umepokea barua kutoka kaka yako aitwaye Amani Furaha anayeishi Tabora S.L.P 300  pamoja na kukujulia hali amekueleza vipi wanavyoendelea huko kwenu Tabora. Pia ametaka uwajulishe ni lini utakwenda huko Tabora. Kutokanaa na ratiba ya shule kukubana unatarajia kwenda utakapofunga shule mwezi Septemba mjulishe kwa kutumia simu ya maandishi jina lako liwe Tusekele Amani.

4.      Kw kutoa hoja nne na mifano eleze jinsi matumizi ya picha na michoro yanavyosaidia matumizi ya kamusi.

5.      (a) toa dhana ya sentensi

(b)  sentensi za Kiswahili hujipambaua kwa sifa zake (taja 3).

(c)   changanua sentensi zifuatazo kwa mkabala wa kimuundo na kimapokeo

(i)     watu wote walimsikilza Rais (kwa njia ya matawi)

(ii)  wao wanaimba lakini sis tuanacheza ngoma (kwa njia ya jedwali)

6.      (a) nini maana ya mzizi wa neon

(b)  Onesha mizizi ya maneno yafatayo 

(i)       Salisha

(ii)    Onesha

(iii)  Onyana 

(iv)   Mpiganaji

(c)   Eleza maana ya istilahi zifuatazo

(i)       Sarufi

(ii)    Kitomeo

(iii)  Lugha

(iv)   Kielezi

7.      Kwa kutumia mifano toshelezi toa uthibitisho wa kiisimu wa Kiswahili ni kibantu.

8.      Kwa kuzingatia maumbo ya umoja na wingi tunga sentensi mbili kwa kila ngeli zifuatazo 

(a)                YU-A-WA

(b)               KI-VI

(c)                U-ZI

(d)               I-ZI                                 

(e)LI-YA. 

 

SEHEMU C (ALAMA 30)

JIBU MASWALI MAWILI KUTOKA SEHEMU HII

9.      Ujio wa waarabu ulisaidia sana kukuza lugha ya Kiswahili. Thibitisha kauli hii kwa hoja zisizopungua nne (4).

10.  Wanaisimu huona kuwa fasihi simulizi ni bora kuliko fasihi andishi. Kwa kutumia hoja tano (5) thibitisha ukweli huu.

11.  Methali zinafunza na zinaweza kupotosha jamii zisipotumika kwa ukamilifu kwwa kutumia methali tano (5) thibitisha kila moja inayoweza kufunza na kupotosha.

 

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 148  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 148  

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

KIDATO CHA TATU 2021

MSIMBO: 021 KISWAHILI

MUDA: SAA 3:00                                                             AUG 2021

 

MAELEKEZO

  1.                Karatasi hii ina sehemu A, B and C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12)
  2.                Jibu maswali yote katika sehmu A na B na maswali matatu (03) kutoka sehemu C
  3.                Zingatia maagizo ya kila sehemu na kila swali
  4.                Andika namba yako ya mtihani katika kila ukurasa wa karatasi

SEHEMU A {Alama 15 }

Jibu maswali yote

  1.                Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x) kisha andika herufi ya jibu hilo katika karatasi yako ya kujibia.
  1. Tuimbe sote ni


  1.                 Wingi nafsi ya kwanza
  2.                Wingi nafsi ya pili
  3.                 Umoja nafsi ya kwanza
  4.                Umoja nafsi ya pili
  5.                 Wing nafsi ya tatu


 

  1. Kusoma kwake kwa bidii kumempatia mafanikio, Neno lililopigiwa mstari ni:


  1.                 Kitenzi
  2.                Kitenzzi kisaidizi
  3.                 Kitenzi jina
  4.                Kitenzi kikurupushi
  5.                 Nomino


 

  1. Jozi ipi ina vipengele sahihi vinavyounda umbo la ndani la kazi ya fasihi simulizi
  1.                 Falsafa, muundo, ujumbe, wahusika
  2.                Mandhari, msimamo, ujumbe, dhamira
  3.                 Ujumbe, mtizamo, migogoro, dhamira
  4.                Ujumbe, msimamo, dhamira, wahusika
  5.                 Lugha, migogoro, falsafa, mtindo

 

  1. Mpangilio sahihi wa vipashio vinavyounda lugha ya kiswahili ni upi
  1.                 Mofimu, kishazi, kirai, neno na sentensi
  2.                Mofimu, neno, kirai, sentensi na kishazi
  3.                 Neno, kirai, kishazi,  sentensi na mofimu
  4.                Neno, mofimu, kirai, kishazi na sentensi
  5.                 Mofimu, neno, kirai, kishazi na sentensi
  1. Ni jambo gani linalodhihirisha upekee wa kazi Fulani ya kifasihi


  1.                 Muundo wa kazi husika
  2.                Wahusika wa kazi husika
  3.                 Jina la kazi husika
  4.                Jina la mtunzi husika
  5.                 Mtindo wa kazi husika


  1. Ipi ni sehemu Ndogo sana ya lugha?


  1.                 Mofimu
  2.                Neno
  3.                 Herufi
  4.                Silabi
  5.                 Mofoloji


 

  1. Ni taratibu zipi zinazofuatwa na lugha fasaha:
  1.                 Kimaana, kimatamshi, kilafudhi, kimuundo
  2.                Kimatamshi, kimofolojia, kiufundi, kimaana
  3.                 Kimatamshi, kimaana, kimuundo, kimantiki
  4.                Kimantiki, kifonolojia, kimaana, kilafudhi
  5.                 Kilafudhi, kimuundo, kiufundi, kimaana

 

  1. Kwa nini lugha ni sauti za nasibu____________
  1.                 Kwa sababu inatumia ishara
  2.                Kwa sababu intumia sauti
  3.                 Kwa sababu inabeba maana
  4.                Kwa sababu inatumiwa na wanyama
  5.                 Kwa sababu inatumiwa na binadamu

 

  1. Ni sifa ipi hutofautisha fasihi simulizi na fasihi andishi?


  1.                 Ukubwa
  2.                Ueneaji
  3.                 Uwasilishaji
  4.                Uhifadhi
  5.                 Utamkaji


 

  1. Mhakiki wa kwanza katika kazi ya fasihi simulizi mfano wa igizo ni:


  1.                 Mtunzi
  2.                Mtazamaji
  3.                 Msomaji
  4.                Mwigizaji
  5.                 Mfasili


 

 

  1.                Oanisha maana za dhana za uandishi zilizo katika orodha A kwa kuchagua herufi ya dhana husika katika Orodha B, Kisha andika herufi husika katika karatasi yako ya kujibia:

ORODHA A

ORODHA B

  1. Irabu
  2. Sarufi
  3. Sentensi sahili
  4. Kidahizo
  5. Chagizo
  1.              Kiwakilishi cha a – unganifu
  2.               Tanzu ya lugha
  3.               Maana ya msingi
  4.              Inaotamkwa huwa hakuna kizuizi chochote kwenye mkondo wa hewa
  5.               Ina hadhi ya kishazi huru
  6.                Kitomeo na taarifa zake
  7.              Ni maneno yanayotokea baada ya kitenzi na kufanya kazi kama kielezi.

 

 

 

SEHEMU B (Alama 40)

 

  1.                Kwa kutumia mifano dhabiti fafanua dhana zifuatazo
  1.                 Urudufishaji
  2.                Uambishaji
  3.                 Kutohoa maneno
  4.                Ngeli

 

  1.                Maneno huweza kubadilika kutoka aina moja na kuwa aina nyingine “Dhihirisha kaulli hii kwa kubadili maneno yafuatayo kwa kuzingatia maelekezo yaliyo katika mabano
  1.                 Kwenda (Badili kuwa nomino)
  2.                Ogopa (Badili kuwa kivumishi)
  3.                 Mzazi (Badili kuwa kitenzi)
  4.                Linda (Badili kuwa nomino)
  5.                 Bisha (Badili kuwa kivumishi)
  6.                 Bora (Badili kuwa kitenzi)
  7.                Refu (Badili kuwa kitenzi
  8.                Kabati (Badili kuwa kielezi)

 

  1.                Kwa kutumia mifano kuntu fafanua tabia zisizopungau nne (4) za vitenzi vya kiswahili

 

  1.                Wewe na msaidizi wako mmehudhruria kikao cha kupanga mahafali ya kidato cha nne.  Andika kumbukumbu ya kikao kilichofanyika katika shule yenu.

 

  1.                Baada ya kiswahili kuteuliwa kuwa lugha ya Taifa vyombo mbalimbali viliundwa kwa lengo la kukuza na kueneza kiswahili dhibitisha dai hilo kwa kutumia asasi tatu (03)

 

  1.                Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata

 

  1.                Korona ugonjwa gani umezua taharuki;

Chanjo haipatikani Ulaya hakukaliki,

Tiba haijulikani, Dunia haifurukutu,

Korona ni maafa kujikinga lazima,

 

  1.                Hofu kubwa imetanda, wakubwa kwa wadogo;

Mafua, homa kupanda utaona uki”gugo”,

China mpaka mpanda, korona haina vigo,

Korona ina maafa kujikinga lazima

 

  1.                Walakini juu ya yote, mapenzi yameoteshwa,

Karantini kwa wotee, makapera wameoa,

Mabinti wasiopenzini, huu msimu wa ndoa

Korona ina maafa kujinginga lazima

 

 

 

  1.                Hakika baniani mbaya Kiatu chake dawa,

Wanandoa walishane penzi bila taabu,

Nao wapenzi wachanga, wasubiri janga lipite

Korona ina maafa kujikinga lazima

 

  1.                Mungu atasaidia Korona itaisha,

Elimu tazingatia Wizara wanakumbushia,

Tunawe yetu mikono, epuka msongamano

Koroana ina maafa kujikinga lazima

MASWALI

  1.                 Pendekeza kichwa cha habari kisichozidi maneno matatu
  2.                Unafikiri kwa nini mshairi anatuasa kuwa Korona ina maafa kujikinga lazima?
  3.                 Mashairi wa shairi hili anawashauri nini wanafunzi kuhusiana na suala la mapenzi?
  4.                Kutokana na shairi ulilosoma eleza njia tano unazozijua utakazotumia kuepukana na ugonjwa wa Korona

 

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii

  1.                Fasihi simulizi ndio fashihi ya awali iliyoanza wakati binadamu alipoanza kutumia lugha mara kwa mara inapowasilishwa kwa hadhira huchukua sifa muhimu ambazo sirahisi kuziona katika fasihi Andishi.  Dhibitisha ukweli huu kwa kutumia hoja tano.

 

  1.            Nyimbo ni mbinu ya kifasihi ambayo wasanii wengi hutumia ili kufikisha ujumbe uliokusudiwa kwa hadhira.  Dhibitisha usemi huu kwa kutumia waandishi wawili wa riwaya ulizosoma.

 

  1.            Taswira ni kibebeo cha ujumbe wa mwandishi katika jamii.  Jadili kauli hii kwa kutumia thamthiliya mbili ulizosoma.

 

  1.            “Mshairi siku zote hukemea uonevu katika jamii “dhibitisha kauli hii wa kutoa hoja tatu kutoka katika kila diwani kati ya Diwani mbili (2) ulizosoma.

 

ORODHA YA VITABU

USHAURI

Wasakatonge    - M.s Khatibu (DUP)

Malenga wapya  - Takiluki (DUP)

Mashairi ya chekacheka - T. A Mvungi (EP & D. LTD)

RIWAYA

Takadini   - Benj. Hanson (MBS)

Watoto wa mama ntiliye - E. Mbogo (H.P)

Joka la mdimu   - A.J Safari  (H.P)

TAMTHILIYA

Orodha Steven Reynolds (MA)

Ngoswe penzi kitovu cha uzembe -E. semzaba

Kilio chetu     -Medical Aid foundation 

Page 1 of 4

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 65  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 65  

THE PRESIDENT'S OFFICE

MINISTRY OF REGIONAL GOVERNMENT AND LOCAL GOVERNMENT

AUGUST-SEPTEMBER   EXAMINATION SERIES

KISWAHILI  FORM-3

2020

TIME: 2:30 HRS

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).
  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali matatu (3) kutoka sehemu C.
  3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na ya kila swali.
  4. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.
  5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

SEHEMU A (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo katika kijitabu chako cha kujibia.

(i) Neno lipi kati ya maneno haya linaweza kudokeza mtenda au mtendwa?

  1. Kiunganishi   
  2. Kivumishi
  3. Kihisishi 
  4. Kiwakilishi 
  5. Kielezi

(ii) Shamba letu li kubwa neno “Li” ni aina gani ya neno? 

  1. Kiwakilishi 
  2. Kielezi 
  3. Kivumishi 
  4. Kiunganishi 
  5. Kitenzi kishirikishi

     (iii) Lugha fasaha hufuata taratibu za lugha, taratibu hizo ni pamoja na 

A       fonolojia, mofolojia, semantiki na sintaksia

B        maana, matamshi, muundo na maumbo

C        maana, matamshi, muundo na mantiki

D        kiimbo, shada, mkazo na toni

E.       fonolojia, mkazo, shada na semantiki

(iv) Kamati ya lugha ya Afrika ya Mashariki (the interteritorial Swahili language committee) iliteua lahaja moja na kuisanifisha, lahaja hiyo ilikuwa ni

A         kimvita             

 B       kiunguja

C         kimtang’ata       

D        kisiu

E         kivumba

(v). Watoto hawa wanacheza vizuri neno “Vizuri” ni aina gani ya neno? 

  1. Kivumishi 
  2. Kielezi 
  3. Kiwakilishi 
  4. Kivumishi cha sifa 
  5. Kihisishi 

 

(vi) Kiswahili ni kibantu kwa kuwa:- 

  1. Kinaongewa na wabantu wengi 
  2. Ni lugha ya Taifa 
  3. Kina maneno mengi ya kibantu 
  4. Kimethibitishwa kiisimu na kihistoria 
  5. Wasomi wengi wamethibitisha hivyo.  


(vii) Ni jambo gani linalodhihirisha upekee wa kazi fulani ya kifasihi? 

  1. Muundo 
  2. Mtindo 
  3. Wahusika 
  4. Jina la mtunzi  
  5. Jina la kazi husika 


(vii) Ipi ni fasili sahihi kuhusu tungo? 

  1. Maneno yanayoonesha uhusiano baina ya neno moja na jingine. 
  2. Kipashio kidogo katika lugha kinachotumika kama dhana ya kuchambulia lugha Fulani. 
  3. Matokeo ya kuweka na kupanga pamoja vipashio sahili ili kujenga vipashio vikubwa zaidi. 
  4. Kipashi cha kimuundo chenye neno moja na kuendelea 
  5. Maneno yenye kutoa maana kamili


(viii) Nini maana ya sentensi sahili. 

  1. Ni sentensi yenye kishazi kuu kimoja au zaidi pamoja na kishazi tegemezi.
  2. Ni sentensi yenye kishazi huru 
  3. Ni sentensi yenye kuonesha masharti 
  4. Ni sentensi yenye maana nyingi 
  5. Ni sentensi yenye vishazi vingi 


(ix) Zifuatazo ni sifa za pijini isipokuwa 

A.      Pijini huwa na maneno kutoka lugha mbili au zaidi

B.      Pijini hutokea kurahisisha mawasiliano baina ya watu ambao kila mmoja 

         ana lugha yake

C.      Miundo ya maneno na tungo katika pijini imerahisishwa ili kukidhi 

         mawasiliano

   D.     Pijini haina msamiati mwa kutosha, hivyo wazungumzaji hutumia sana 

        ishara

  E.    Pijini ina watu ambao kwao hiyo ni lugha yao ya kwanza


2. Katika kila sentensi uliyopewa, orodhesha vishazi huru katika Safu A na vishazi tegemezi katika safu B.
(a) Ngoma hailii vizuri kwa kuwa imepasuka.
(b) Watoto walioandikishwa watakuja kesho.
(c) Kiongozi atakayefunga mkutano amepelekewa taarifa.
(d) Mtawatambua walio wasikivu.
 (e)       Kitabu ulichopewa kina kurasa nyingi. 

 

3. Taja aina za sentensi zifuatazo kisha eleza muundo ujengao kila sentensi.

  1. Maisha ni safari ndefu.
  2. Ukisoma kwa bidii utafaulu kwa kiwango cha juu.
  3. Mtoto aliyelazwa hospitalini ameruhusiwa kwenda nyumbani.
  4. Nitakuja leo ingawa nitachelewa sana.
  5. Alinunua madaftari lakini kitabu cha Kiswahili alipewa na mwalimu.

4. Andika maneno matano ambayo yameundwa kutokana na kufananisha sauti. Kwa kila neno tunga sentensi moja.

5. Eleza dhima za mofimu "li" kama ilivyotumika katika sentensi zifuatazo:

  1. Shamba letu li kubwa sana.
  2. Wlishelewa kurudi.
  3. Tunalifuatilia.
  4. Limeharibika.
  5. Shikilia.

6. Andika sentensi zifuatazo katika hali ya ukanushi:

  1. Ameshiba sana.
  2. Watoto wengi wanaogelea.
  3. Mvua ilinyesha kwa wingi sana.
  4. Kijana anakula chakula kingi.
  5. Mimi nasoma polepole.

7. Bainisha mzizi wa asili kwa kila neno katika maneno yafuatayo:

  1. Anawaandikisha
  2. Mkimbizi
  3. Mlaji
  4. Muumbaji
  5. Nisingelipenda
  6. Kuburudika
  7. Sadifu
  8. Aliokota
  9. Walichopoka
  10. Kipambanuliwe

1. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:

Karibu masikio ya watu wa mahali pengi yalijaa habari za Karama na mashtaka yake. Umaarufu wake wa ghafla ulizungumzwa karibu na mbali. Mtu yeyote wa desturi anapozuka katika umaarufu, huyavuta masikio na macho ya watu wengi kwa sababu jambo kama hili hutokea nadra sana kwa watu ambao bahati mbaya imeshughulika kuwaweka nyuma. Kwa hiyo, siku ya tatu ya baraza ilihudhuriwa na mfalme, watu wenye vyeo mbalimbali, pamoja na nusu moja ya umati mkubwa wa Kusadikika. Fikra zilizochanganyika ziliushika umati huu. Baadhi ya watu walimwajabia Karama wakamhesabu kama mtu bora wa karne yao. Hawa walitumaini ataokoka lakini wengine waliwaza kuwa Karama alikuwa kama mjinga aliyekuwa akicheza na hatari kubwa iliyofunua taya mbele yake.

Waliokuwa wakimtazamia kuokoka walikuwa na wasiwasi wao; na wale waliokuwa wakimtazamia kuanguka walikuwa na fadhaa yao. Walakini hapana mtu hata mmoja aliyepata kulisema wazo lake.

Bila ya kujua alivyoajabiwa Karama aliendelea kusema mbele ya baraza, “Watu wanaoteswa ndio wanaoyajua mateso yao.” Kusadikika ilikuwa chini ya mateso makubwa sana. Maisha yao yalizungukwa na maradhi na mauti, uadui usiokwisha, nchi iliyokaribia kugeuka jangwa na mwamba na madhila mengine mazito yaliyowakabili watu. Wanakusadikika walitaka faraja katika mateso haya. Kila jitihada ilijaribiwa ili kuirekebisha saa ya maendeleo ya nchi, lakini mara kwa mara majira yake yalirudishwa nyuma. Kama hili lilifanywa kwa makosa ama kwa makusudi ni siri iliyo ng’ambo ya fahamu zangu hata sasa. Lakini kama siri njema hufichika, ile iliyo mbaya haifichiki hata kidogo. Uchaguzi wa wajumbe ulikuwako lakini hathibitisho ya matokeo ya ujumbe hayakupatikana.

Kusadikika iliishi kuona mjumbe baada ya mjumbe kuadhiriwa na kuadhibiwa vibaya. Kama washauri hawakudhuriwa na hili lakini watu wengine walidhuriwa sana. Kazi njema za wajumbe wawili zilipotea bure. Manung’uniko ya lawama hii yalikuwa katika hewa yote ya Kusadikika.

Hili lilipotokea serikali iliombwa ima faima kufanya ujumbe mwingine. Basi mjumbe wa tatu alitakikana ajitolee mwenyewe kwa ujumbe wa Kusini. Wito wa mjumbe wa tatu uliitikiwa na Kabuli; mtu mwenye busara, haya na mcheshi. Yeye alipatikana upesi kabisa kuliko ilivyokuwa kwa mara ya pili na ya kwanza. Misiba ya Buruhani na Fadhili ilikuwa mikubwa ya kutosha kuikongoa mioyo ya bidii katika bawaba zake. Kabuli aliyajua haya yote lakini alikuwa mtu wa moyo wa namna nyingine kabisa. Alikuwa na bidii kubwa kama ile ya siafu athubutiye kukivuka kijito kwa daraja iliyofanywa kwa maiti ya siafu wengine walioelea majini huko na huko. Maji yalijulikana kuwa na asili ya rutuba, mvuke na umeme. Nguvu nyingine za namna mbalimbali zipo pia katika maji. Kama siafu mdudu mdogo na kipofu wakati mwingine haogopi kuzikabili nguvu hizo pamoja na hatari zake kwa sababu njema, basi ni dhahiri kuwa viongozi wa wanadamu wanapoteswa bure bidii za wafuasi wao hutanuka ajabu.

Hapana tishio liwezalo kuukomesha mwendo huu. Kwa hakika utafululiza kuwako duniani mpaka mateso yakome kabisa, na labda wakati huo dunia hii itakuwa njema kama itamaniwavyo kuwa.

Buruhani na Fadhili walitoa sadaka zao bora ili kuyahimiza majilio ya wakati uliotakikana sana. Kabuli aliwaona watu wawili hawa kama wafadhili wakubwa wa ulimwengu. Alitaka kuwa mshirika wao kwa thamani yoyote ya maisha yake.

Kama ilijulikanavyo, Kusini na upande wa dunia yatokako matufani makubwa na baridi kali sana. Kabuli aliyakabili mashaka haya bila ya kigeugeu. Naam, alikuwa kama mtu aliyekuwa akinywa uchungu bila ya kigegezi. Mara mbili alikamatwa akafanywa mahabusu.

Maswali

(a) Eleza maana ya maneno yafuatayo kama yalivyotumika katika kifungu cha habari:

  1. Fadhaa
  2. Madhila
  3. Kuadhiriwa
  4. Ima faima
  5. Kigeugeu
  6.  Kigegezi.

(b) Eleza mchanganyiko wa fikira walizonazo wana wa Kusadikika kuhusu Karama.

(c) Kwanini bidii ya mjumbe wa Kusini imelinganishwa na bidii ya siafu? Toa sababu mbili.

(d) Ujumbe wa mwandishi wa kifungu hiki unahusu nini?

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii.

8. Andika insha isiyozidi maneno mia tatu (300) na isiyopungua mia mbili na hamsini (250) kuhusu faida za televisheni kwa jamii.

ORODHA YA VITABU USHAIRI

Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP)

Malenga   Wapya - TAKILUKI (DUP)

Mashairi   ya   Chekacheka - T.A. Mvungi (EP & D.LTD)

RIWAYA

Takadini - Ben J. Hanson (MBS)

Watoto   wa   Maman’tilie - E. Mbogo (H.P)

Joka   la   Mdimu - A.J. Safari (H.P)

TAMTHILIYA

Orodha - Steve Reynolds (MA)

Ngoswe Penzi Kitovu   cha   Uzembe - E. Semzaba (ESC)

Kilio   Chetu - Medical Aid Foundation (TPH)

10. "Fasihi ya Kiswahili imemweka mwanamke katika hadhi tofauti tofauti." Thibitisha usemi huu kwa kutumia hoja tatu kwa kila riwaya kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.

11. (a) Vigano ni nini?

(b) Tunga vigano kwa kutumia methali isemayo "Umdhaniaye siye kumbe ndiye!"

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 28  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 28  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256