FORM THREE KISWAHILI ANNUAL EXAMS

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

JAMUHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA

MTIHANI WA MWISHO MWAKA

KIDATO CHA TATU

KISWAHILI NOVEMBA 2023

Muda 2:30

MAELEKEZO

  1. Jibu maswali yote
  2. Mtihani huu una sehemu A. B na C (Jumla ya maswali 9)
  3. Simu za mkononi haziruhusiwi

SEHEMU A (16)

  1. Chagua jibu sahihi katika maswali yafuatayo
  1. Neno lipi kati ya haya ni mofimu huru
  1. Uji
  2. Uzuri
  3. Uchache
  4. Ufa
  5. Upweke
  1. Ni kauli inayotumia maneno ya kawaida lakini hutoa maana tofauti na iliyopo kwenye maneno yale.
  1. Mafumbo
  2. Nahau
  3. Misemo
  4. Semi
  5. Hadithi
  1. Utokeji wa misimu katika jamii hutegemea na
  1. Uchaguzi wa viongozi
  2. Mabadiliko ya Kijamii
  1. Shughuli itendekayo
  2. Utani uliopo miongoni mwa wanajamii
  3. Kutumia na kudumu kwa muda mrefu
  1. Nyenzo kuu za lugha ya Mazungumzo ni
  1. Usimuliaji
  2. Mdomo
  3. Maandishi
  4. Vitendo
  5. Ishara
  1. Kipi kipengele kinachohusu mjengeko wa kazi za fasihi?
  1. Muundo
  2. Wahusika
  3. Mtindo
  4. Mandhari
  5. Lugha
  1. Kikundi cha maneno kinachoonesha jambo lililotendwa na mtenda katika sentensi hujulikanaje?
  1. Kikundi kivumishi
  2. Kikundi kitenzi
  3. Nomino
  4. Chagizo
  5. Shamirisho
  1. ni kauli ipi iliyotumika katika uundaji wa neno “Nitamfitinisha”
  1. Kutendeana
  2. Kutendesha
  3. Kutenda
  4. Kutendea
  5. Kutendewa
  1. Dhima Kuu ya Misima katika lugha ni ipi?
  1. Kuficha jambo kwa wasiohusika
  1. Kuongeza ukali wa maneno
  2. Kupatanisha maneno
  1. Kutambulisha aina za maneno
  2. Kuhimiza shughuli za maendeleo
  1. Ipi ni jozi sahihi ya vipera vya semi?
  1. Soga, nyimbo na nahau
  2. Methal mizungu na vitendawili
  3. Mafumbo, soga, maghani
  4. Misemo, mafumbo na vigano
  5. Mashairi mafumbo na mizungu
  1. Shule zetu zimeweka mikakati kabambe ya kutokomeza daraja la pili ili zibaki na daraja la kwanza pekee. Neno ‘ili’ katika tungo hii ni aina gani ya neno?
  1. Kiunganishi
  2. Kivumishi
  3. Kielezi
  4. Kitenzi
  5. Kihusishi
  1. Oanisha maelezo yaliyo katika Orodha A na dhana husika katika Orodha B. Kisha andika herufi husika katika karatasi ya majibu.

ORODHA A

ORODHA B

  1. Mada, Uhusiano, Malengo na Muktadha
  2. Umeupiga mwingi
  3. Nani Ugali mbuzi choma
  4. Baba Juma amefariki
  5. Hupokea mabadiliko ya papo hapo
  6. Kutumia lugha kulingana na kaida za jamii
  1. Tungo tata
  2. Utumizi wa lugha
  3. Lugha ya mazungumzo
  4. Simo
  5. Rejesta
  6. Humsaidia mzungumzaji kuteua lugha kwa usahihi
  7. Sababu ya utata
  8. Lahaja
  9. Lugha ya maandishi

SEHEMU B (ALAMA 54)

  1. (a)Unaelewa nini dhana ya misimu

(b) Onesha vyanzo viwili vya Msimu

(c) Misimu huweza kuundwa kwa njia tofauti tofauti

  1. Demu
  2. Kumzimikia
  3. Disco
  4. Ferouz ni twiga
  5. Mataputapu
  1. Batuli alitaka kuhifadhi methali na vitendawili kwa njia ya Kichwa tu kwa ajili ya kizazi kijacho. Lakini Kibutu alimkataza asifanye hivyo badala yake atumie njia nyingine
  1. Toa hoja nne (4) kama sababu ya katazo hilo
  2. Taja njia tano (5) sahihi ambazo unahisi kibuyu angemshawishi batuli atumie.
  1. Eleza kinagaubaga tofauti zilizopo kati ya lugha ya mazungumzo na lugha ya maandishi kwa kuzingatia vipengele vifuatavyo.
  1. Uwasilishaji
  2. Uhifadhi
  3. Manadiliko
  1. Lugha ina tabia ya kujiongeza msamiati wake kwa njia kadha wa kadha; kwa kuthibitisha dai hilo, tambulisha njia zilizotumika kuunda maneno yafuatayo.
  1. Kuku
  2. Mpangaji
  3. Kifaurongo
  1. TATAKI
  2. Fedha
  3. Msikwao
  1. Kitivo
  2. Pilipili

ix. Imla, mali, mila, lami

  1. Maendeleo ya Sayansi na Teknologia ni ndumi la kuwili kwa fasihi simulizi. Kwa hoja sita thibitisha ukweli wa kauli hii kwa kutoa hoja mbili.

8. Soma kifungu habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:

"Ndugu wazazi, kumbe safari yenu inahusu harusi ya Maria ?".Mkuu wa shule aliwauliza wazazi."Ndiyo," wazazi walijibu kwa Pamoja bila aibu."inategemewa kufugwa lini ."Mkuu aliendelea kuhoji. Harusi hii ilikuwa ifanyike wakati Maria anapofika kidato cha nne, Lakini Maria huyu ametufanyia uhuni na vituko visivyoelezeka. Nasi sasa tunachukiwa kijiji kizima na kudharauliwa na kila mtu.Hii imetuudhi sana, tumetungiwa nyimbo na kufanyiwa kila shutuma. Hatuna raha ;hivyo tumeonelea bora tuje kukuomba umfukuze shule ili kiburi kimwishie .Nasi tupo tayari kukulipa kiasi chochote cha fedha ukitimiza haja yetu hii,"Mzee Abdallah alieleza." Muda wote mkuu wa shule alikuwa akimtazama Mzee kwa chati sana .Kisha akauliza swali la kuchochea zaidi: Maria ana kiburi kumbe?"

Mama Maria hakutaka hilo limpite ,hima hima akatoa maelezo yake ."Mama wewe ,Maria usimuone hivi. Maria mwanangu hataki kufuata utamaduni wetu wa kuolewa. Maria ati achague mchumba mwenyewe, ati mahari haiyoni kama ni kitu cha msingi. Kiburi hicho kinatokana na elimu mliyompa.

Mtoto sasa ameharibika .Anafanya apendavyo elimu gani isiyojali adabu.wala utii?" Mama Maria alimaliza huku jasho na machozi yanamtoka".

Hapa mkuu wa shule aliona kwanza awaelimishe kabla hajawatolea kauli ya mwisho.Alikwishatambua kwamba wazazi wa Maria walikuwa wameachwa nyuma na wakati .Kila upya wa mawazo waliuita kiburi.

Maswali

(i)Bainisha dhima nne (04) zilizotokana na habari uliyosoma.

Fupisha habari hiyo kwa maneno yasiyopungua 70 na kuzidi 80.

SEHEMU C: (ALAMA 30)

Jibu maswali mawili katika sehemu hii swali la 11 ni lazima

ORODHA YA VITABU

ORODHA YA VITABU.

USHAIRI.

  • Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP).
  • Malenga wapya -TAKILUKI (DUP)
  • Mashairi ya Chekacheka - T.A.Mvungi(EP&D.LTD)

RIWAYA.

  • Takadini -Ben J.Hanson (MBS)
  • Watoto wa Mama N'tilie - E.Mbogo(HP)
  • Joka la Mdimu - A.J.SaiTari (HP)

TAMTHILIYA

  • Orodha - Steve Reynolds(MA)
  • Ngoswe Penzi Kitovu Cha uzembe - E. Semzaba (ESC)
  • Kilio chetu - Medical Aid Foundation (TPH)
  1. Fasihi ya Kiswahili imemuweka mwanamke katika hadhi tofauti tofauti. Thibitisha Usemi huu kwa kutumia hoja tatu kwa kila riwaya
  2. Lugha ni mhimili katika kazi yoyote ya fasihi. Watunzi hutumia lugha kiufundi ili kufikisha ujumbe kwa jamii husika. Kwa kutumia jazanda au taswira tatu kutoka katika diwani mbili ulizosoma na uonyeshe namna zinavyofikisha ujumbe kwa jamii.
  3. “Ukiona mtu mzima analia ujue kuna jambo au mambo hayapo sawa. Kauli hii inaweza kuwiana na waandishi wa riwaya Juu ya jamii inavyowazunguka, kwa kutoa hoja tatu kutoka kila riwaya katika riwaya mbili ulizosoma, jadili kwa nini wasanii hao hulia?

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 152  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 152  

OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA 2020

021KISWAHILI

(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)

MUDA: SAA 3 DECEMBER 2020


Maelekezo

1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).

2. Jibu maswali yote kutoka sehemu A, B na chagua maswali matatu (03) kutoka sehemu C.

3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na kila swali.

4Andika kwa kutumia kalamu ya wino wa bluu au nyeusi

5. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa haziruhusiwi katika chumba cha mtihani.

6. Andika namba yako ya mtihani katika kila karatasi yako ya kujibia.

SEHEMU A, (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo katika karatasi yako ya kujibia.

(i) Ni kanuni, sheria na taratibu zipi zinazozingatiwa na wazungumzaji wa lugha fulani?

A Mofimu, Neno, Kirai, Kishazi na Sentensi

B Herufi, Sauti, Mofimu,Silabi na neno.

C Sarufi Maana, Sarufi Miundo, Sarufi Maumbo na Sarufi Matamshi.

 Sarufi maana, Mofimu, Neno na Kirai

E Silabi, Neno, Kirai na Sentensi.

(ii)………………. Ni sauti zinazotamkwa mara moja na kwa pamoja kama fungu moja la sauti.

 A Sauti B Herufi

 C irabu D  Silabi

 E Konsonanti

(iii)  Zipi ni nyenzo za lugha yoyote duniani?

A Sarufi na Fasihi B Irabu na Konsonanti

C Sarufi, Irabu na KonsonantiD Fasihi, Irabu na Konsonanti

E Sarufi, Fasihi, Irabu na Konsonanti

(iv) Mpangilio sahihi wa ngeli za kisintaksia ni upi?

A YU/A-WA, I-ZI,LI-YA,U-I,KI-VI,U-ZI,U-YA, KU,PA-MU-KU

B U-ZI, I-ZI,LI-YA,U-I, KU, YU/A-WA,U-YA, KI-VI, PA-MU-KU

C YU/A-WA, I-ZI, LI-YA,U-YA, KI-VI,U-ZI,U-I, KU,PA-MU-KU

D YU/A-WA,I-ZI, LI-YA,U-I,KI-VI, U-ZI,U-YA, PA-MU-KU, KU

E YU/A-WA, I-ZI,LI-YA, U-I, KI-VI,U-ZI, U-YA,KU, PA-MU-KU

(v)  Ni upi mpangilio sahihi wa mjengo wa Tungo?

A Kirai, Neno, Sentensi na Kishazi

B Neno, Kirai, Kishazi na Sentensi

 Kishazi, Kirai, Sentensi na Neno

E Sentensi, Neno. Kishazi na Kirai

(vi)  Ni lugha mseto ya muda inayozuka pindi makundi mawili yenye lugha mbili tofauti yakutanapo.

 Lugha ya vizalia B Pijini

C Kibantu D Kiswahili

E Kiunguja

(vii)Mambo muhimu yanayopatikana katika maana ya lugha ni kama yafuatayo, isipokuwa;

A Ni sauti za nasibu B Ni mfumo

C Lugha hufurahisha na kufundisha D Lugha inamuhusu binadamu

E Lugha ni chombo cha mawasiliano

(viii)  Ni sentensi ipi sio sentensi huru?

A Juma anacheza mpira B Anaimba vizuri

C Mtoto aliyepotea jana amepatikana. D Asha ni mtoto mzuri

EYule alikuwa anataka kucheza mpira.

(ix)  ……………. Ni kipashio kidogo kabisa cha lugha chenye maana. Maana hiyo yaweza kuwa ya kisarufi au kileksika;

 Isimu B Shina

C Mzizi D Kiimbo

E Mofimu

(x) Ni seti ipi inawakilisha kikamilifu wahusika wa fasihi simulizi?

A Vitu, mahali, wanyama, binadamu, fanani na maleba.

B Hadhira, wanyama, maleba, binadamu na fanani.

C Fanani, vitu, mahali, binadamu, maleba na wanyama.

 Wanyama, manju, binadamu, vitu, mahali na maleba

E Hadhira, binadamu, wanyama, vitu, mahali na fanani.

2. Oanisha maelezo yaliyo katika orodha ‘’A’’ ambayo ni aina ya tungo na orodha ‘’B’’ ambazo ni aina za maneno yanayounda tungo hizo kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika karatasi yako ya kujibia.

ORODHA “A”

ORODHA “B”

i.Wale waliamini maneno yangu

 ii. Salama alikuwa mwanafunzi wangu

 iii. Walikuwa wanataka kwenda kulima

 iv.Alikuwa anajisomea darasani polepole

 v. Loo! Yule anapenda ugomvi

A. N + t +N +V

B. H + w +T + N

C. W + T + N + V

D. Ts + T + E +E

E. Ts + Ts + Ts + T

F. N + V + t +E

G. N + U+ N+ T

SEHEMU B (Alama 40)

Jibu maswaliyote katika sehemu hii

3.Tunga sentensi moja kwa kila alama kuonesha matumizi ya alama zifuatazo.F4

i. Mkato

ii. Mabano

iii. Alama za mtajo

iv. Nukta pacha

4.Andika maana ya methali zifuatazo;

  1. Kikulacho ki nguoni mwako.
  2. Mtaka cha uvunguni sharti ainame.
  3. Mchumia juani hulia kivulini.

5.(a) Tenga kiima na kiarifu katika sentensi zifuatazo. Tumia alama ya mkwaju (/) na kuweka herufi “K” juu ya kiima na herufi “A” juu ya kiarifu.

i. Mdogo wangu anaongea sana

ii. Yule kijana aliyekuja hapa juzi amefariki dunia

iii. Frank ni kijana mpole sana

iv. Mama amelala sakafuni

(b) Changanua sentensi zifuatazo kwa njia yamatawi kwa kutumia mkabala wa kimapokeo

i. Fisi mkubwa ameuawa kichakani jana alfajiri.

ii. Mtoto aliyekuwa anacheza uwanjani amevunjika mguu.

6.(a) Kwa kutumia mifano miwili kwa kila kipengele, fafanua kwa ufupi jinsi vipengele vifuatavyo vinavyoonesha kuwa vitenzi vya Kiswahili na lugha za kibantu vina asili moja.

  1. Mpangilio wa viambishi katika vitenzi
  2. Kiambishi tamati katika vitenzi

b) Eleza kwa ufupi juu ya nadharia zifuatazo kwa jinsi zinavyoelezea asili ya Kiswahili

a)Kiswahili ni pijini au krioli

b)Kiswahili ni kiarabu

7. Kwa kutumia mifano, fafanua dhana zifuatazo kama zinavyotumika katika fasihi

a)Tashibiha

b)Takriri

c)Sitiari

d)Tashihisi

e)Mubaalagha

8. Soma kifungu cha habari kifuatacho, kisha jibu maswali yanayofuata;

Wanangu, toka zamani bara letu la Afrika lilikuwa na mambo yaliyohitilafiana na haya tunayoyaona sasa. Hadithi, vitimbi, na visa vilivyotokea zamani katika bara letu vinatofautiana sana na mabara yoyote mengine. Vyetu ni vitamu na bora kuliko vyote vile vilivyotokea katika mabara hayo.

Miujiza ya mambo yaliyotokea ina mizizi ambayo viini vyake hubenua waziwazi mila na desturi za asili tangu zamani, hivyo, hadithi hizo zina tija ya makumbusho ya daima milele. Kwa hiyo, katika hali yoyote yatupasa kuhifadhi hazina za mila zetu. Mila zetu zidumishwe; kwa mfano watu kuzunguka moto huku kizee kikongwe au ajuza akisimulia hadithi za mambo ya kale liwe ni jambo la kawaida kabisa. Katika dunia ya leo simulizi hizo za ujasirina uzalendo zimeenea kutoka vizazi hadi vizazi. Mambo mengi yamebadilika kutoka mitindo aina aina, hivyo mabadiliko hayo yasitufanye sisi kusahau simulizi zetu katika mitindo yetu. Ni wajibu utupasao kuendeleza tabia hizi ili tubenue mbinu za masimulizi hata kwa vitabu.

Maswali

  1. Pendekeza kichwa cha habari hii kisichozidi maneno matatu.
  2. Bara la Afrika lina mambo gani mawili mazuri.
  3. Mwandishi anatuhimiza tudumishe mila ipi?
  4. Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua 50 na yasiyozidi 60.

SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu(3) kutoka katika sehemu hii.

9.Wewe kama afisa Manunuzi wa kiwanda cha mbao cha Mshikamao S. L. P 100 Chamwino, andika barua kwa mfanyabiashara yeyote mashuhuri wilayani kwenu kuhusu agizo la vifaa vifuatavyo; Misumeno 5, gundi ya mbao lita 20, misumari ya nchi sita Kg 25, na kofia ngumu 40. Jina lako liwe Shukrani Kazamoyo.

10. Kwa kutumia diwani mbili ulizosoma, eleza jinsi taswira tatu kutoka kila diwani zilivyotumiwa na msanii kuwasilisha ujumbe kwa jamii.

11. “Kazi ya fasihi ina radha kwa sababu inamzungumzia pia mwanamke kwa namna tofautitofauti” Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu katika riwaya mbili ulizosoma.

12. Chagua wahusika wawili katika tamthiliya teule mbili ulizosoma na uoneshe ujumbe unaowasilishwa na waandishi kupitia matendo yao.

ORODHA YA VITABU 

USHAIRI

Wasakatonge ---------------------------- M. S Khatibu (DUP)

Malenga wapya-------------------------- TAKILUKI (DUPU)

Mashairi ya Chekacheka---------------- T. A. Mvungi (EPdD.LTD)

RIWAYA

Takadini ----------------------------------- Ben J. Hanson (MBS)

Watoto wa Mama Ntilie ----------------- E. Mbogo (H.P)

Joka la Mdimu ---------------------------- A. J. Safari ( H.P)

TAMTHILIYA

Orodha ------------------------------------ Steve Reynolds ( M. A)

Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe ----- E. Semzaba (ESC)

Kilio Chetu --------------------------------- Medical Aid Foundation (TPH)

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 37  

FORM THREE KISWAHILI EXAM SERIES 37  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256