?> HISTORIA STANDARD THREE EXAMS SERIES
HISTORIA STANDARD THREE EXAMS SERIES
JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA RAISI
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
DARASA LA TATU
MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA
SOMO: HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI
1. Chagua jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu katika kisanduku 
i. Eneo lipi kati ya haya yafuatayo paligundulika masalia ya fuvu la binadamu wa kale? 
A. Isimila 
B. Kondoa Irangi 
C. Bonde la Oldupai
D. Isimila 
ii. Ushirikiano wa kibiashara baina ya wafanyabiashara kutoka Mashariki ya Mbali na Kati  na jamii zetu ulisababisha kukua na kuenea kwa lugha gani? 
A. Kiingereza 
B. Kibantu 
C. Kifaransa
D. Kiswahili 
iii. Ipi kati ya hizi zifuatazo ni haki ya mtoto? 
A. Kuajiriwa
B. Kusoma kwa bidii 
C. Kucheza 
D. Kuwaheshimu wakubwa 
iv. Mfalme au mtawala wa nchi katika utawala wa kiarabu aliitwa nani? 
A. Mwinyi
B. Sultani 
C. Mtemi 
D. Chifu 
v. Jambo ambalo kila mtu anapaswa kulitimiza huitwaje? 
A. Maadili
B. Sheria 
C. Haki 
D. Wajibu 

2. Oanisha maneno yaliyopo katika ORODHA A na yale yaliyopo katika ORODHA B kwa kuandika herufi ya jibu sahihi katika mabano 


3. Jibu maswali yafuatayo kwa kuchagua jibu sahihi katika kisanduku kisha uliandike  katika sehemu iliyoachwa wazi 
 Urithi, Husuni, Utumwa, Makumbusho, Magofu 

i. Jumba lililotumiwa na wafalme au sultani kama makazi lilijulika kama 
 ___________________________________________________________________ 
ii. Mfumo ambao binadamu alitumikishwa bila malipo na kumilikiwa na mtu mwingine  uliitwaje?____________________________________________________ 
iii. Mabaki ya majengo ya kale yanayoonekana huitwaje?________________________ 
iv. Vitu vyenye thamani na kumbukumbu zilizohifadhiwa au kuwepo katika katika eneo  fulani kutoka vizazi vilivyopita huitwaje?__________________________________ 


4. Bainisha matendo yasiyofaa na yanayofaa kwa kuweka alama ya vema katika  sehemu sahihi: (i) kimefanyika kama mfano. 




5.Chunguza kwa makini picha ifuatayo kisha jibu kipengele cha (i)- (iv) kwa  kuandika  majibu sahihi  katika nafasi zilizoachwa wazi. 


Maswali 
i. Urithi gani wa kihistoria unaoneshwa katika picha hii? 
__________________________________________________________ 
ii. Je, urithi wa kihistoria unaooneshwa katika picha hii unapatikana katika eneo gani  hapa Tanzania?________________________________________ 

iii. Eneo ulilolitaja katika kipengele cha (ii) hapo juu linapatikana katika mkoa gani? 
__________________________________________________________ 
iv. Je, urithi wa kihistoria unaooneshwa katika picha hii una umuhimu gani?  _____________________________________________________________


6. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata 
Kufanya kazi kwa bidii ni jambo linalosisitizwa katika maadili ya jamii. Tabia ya kupenda  na kufanya kazi ni miongoni mwa matendo ya kimaadili katika jamii. Hivyo, kila mtu  anapaswa kupenda na kufanya kazi kwani kazi ni msingi wa maendeleo. Tangu kale,  uvivu ulipingwa na jamii nzima. Watu katika jamii walithaminiwa kutokana na uwezo  wao wa kufanya kazi. Mtu mvivu alipingwa kwa kukiuka maadili ya jamii. Viongozi  walichaguliwa kwa kuzingatia uwezo wao wa kufanya kazi. 
Maswali 
i. Tabia gani inatajwa katika kifungu hiki cha habari kuwa ni miongoni wa matendo ya  kimaadili katika jamii? 
______________________________________________________________________ 
ii. Kwanini kila mtu anapaswa kufanya kazi? 
______________________________________________________________________ 
iii. Tabia gani ilipingwa na jamii nzima tangu kale? 
______________________________________________________________________ 
iv. Hapo kale viongozi walichaguliwa kwa kuzingatia nini? 
______________________________________________________________________

LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD THREE EXAM SERIES 127

 OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MUHULA WA PILI MWEZI

SOMO: HISTORIA NA MAADILI YA TANZANIA DARASA: TATU 

MUDA: SAA 1:00 SEHEMU

A: Chagua jibu sahihi zaidi na uandike herufi katika sehemu husika.

1. i. Ipi kati ya zifuatazo huonesha Amani na uhuru wa mtu na mali zake?

  1.  Wimbo wa Taifa 
  2. bendera ya Mahakama 
  3. Mwenge wa uhuru 
  4. Bendera ya Taifa [     ]

ii. Maadilia mazuri hufanya mtu kusaidia na ________________ watu. 

  1. haikubaliki 
  2. sisiti 
  3. kuheshimu
  4. kutoheshimu [     ]

iii. Mambo yafuatayo hupatikana kwenye mazingira ya nyumbani isipokuwa ______. 

  1. samani 
  2. vifaa mbalimbali
  3.  wanyama wa ndani 
  4. Reli [     ]

iv. Mtu mwenye mamlaka ya kufanya moja kwa moja na kusimamia wengine ni ______________. 

  1. mwalimu
  2. wazazi 
  3. kiongozi 
  4. polisi [     ]

v. Kujiunga na vyama na kikundi bila vikwazo nchini hujulikana kama ___________. 

  1. haki ya maisha 
  2. haki ya kuabudu
  3.   uhuru wa mgawanyo
  4.  uhuru wa chama [     ]

SEHEMU B:

2. Oanisha fungu A na Fungu B ili kupata maana sahihi iliyokusudiwa.

NA

KIFUNGU A

MAJIBU

KIFUNGU B

i.

Mfano wa mawasiliano mabaya katika jamii

[     ]

  1. Kazi ya watoto
  2. Kushiriki
  3. Rasilimali ya asili
  4. Uonevu
  5. Kanuni na sheria za shule
  6. Unyanyasaji wa mtoto

ii.

Kitendo cha kumdharau mtoto

[     ]

iii.

Njia inayotusaidia kushiriki katika kutatua matatizo ya wengine

[     ]

iv.

Kitu chochote kinachofaa kutokana na mazingira asili

[     ]

v.

Mwongoza na kanuni za maadili ambazo zinadhibiti tabia ya mtoto shuleni.

[     ]

SEHEMU C:

3. Tumia maneno ya kwenye kisanduku kujaza nafasi zilizoachwa wazi.

Majukumu, uvumilivu, ustahimilivu, haki, uaminifu.

i. Kuwa mkweli na muwazi ________________________.

ii. Vitu ambavyo mtu anastahili na anapaswa kupewa ________________________.

iii. Uwezo wa kuishi na watu hata kama mnatofautiana kimawazo ______________________.

SEHEMU D:

4. Kamilisha jedwali lifuatalo na kujaza maana ya rangi za bendera ya Taifa

NA

RANGI YA BENDERA

MAANA YAKE

i.

Kijani


ii.

Manjano


iii.

Samawati


iv.

Nyeusi


5. Angalia mchoro ufuatao kwa makini kisha jibu maswali yanayofuata

image

Maswali

i. Taja alama ya Taifa ambayo imeoneshwa hapo juu _________________________________________. 

ii. Umuhimu wa alama hii ni _____________________________________________________________. 

iii. Alama hii utaipata wapi mara nyingi? ____________________________________________________.

iv. Taja alama nyingine mbili za taifa ambazo unaziona hapo juu ______________________________ na _____________________________

6. Soma kifungu cha habari kwa makini kisha jibu maswali yafuatayo::

Ni muhimu sana kutunza mwili wako, akili na nafsi kila siku na sio tu wakati unaumwa. Hili linawezekana kwa kula vyema, kufanya mazoezi, kupunguza mawazo na kwenda mapumzikoni mwili unapohitajika. Mambo haya yatafanya ukae mwenye furaha, mwenye afya na mstahimilivu.

Maswali

i. Kifungu hiki kinahusu nini? ______________________________________________________.

ii. Njia tatu za kutunza miili yetu ni _________________________________________________, _________________________________ na ______________________________________.

iii. Taja vitu vitatu tunapaswa kuzingatia ili kuwa na afya. 

(a) _______________________________________

 (b) ________________________________________

 (c) _______________________________________.

iv. Unafikiri nini kitatokea tukishindwa kutunza miili yetu? ___________________________________________.

LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD THREE EXAM SERIES 114

OFISI YA RAIS-TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MTAA

MTIHANI WA NUSU MUHULA AGOSTI 2025

MTIHANI WA  DARASA LA III 

HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

1. Andika herufi ya jibu sahihi kwenye mabano

(i). Elimu inayohusu matukio yaliyotokea nchini Tanzania tangu mwanzo wa maisha ya watu mpaka leo inaitwaje? 

  1. maadili 
  2. Historia ya Tanzania 
  3. Fizikia 
  4. mazingira [   ]

(ii). Kipi kati ya vitendo vifuatavyo ni kitendo cha maadili mema? 

  1. kuiba vipande vya nyama nyumbani
  2. kudanganya
  3. kutukana
  4. kuwapokea wakubwa mizigo [   ]

(iii). Mfululizo wa mambo yaliyotokea katika maisha yetu katika vipindi tofauti huitwaje?

  1. historia 
  2. mazingira 
  3. maadili 
  4. uadilifu [   ]

(iv). Hayati John Pombe Magufuli alifariki tarehe 17 mwezi Machi 2021. Je, katika Maisha yetu hili ni tukio gani? 

  1. la kimaadili 
  2. la kihistoria 
  3. la kufurahisha 
  4. lisilofaa [   ]

(v). Ipi ni faida mojawapo ya vitendo vya kimaadili? 

  1. hujenga tabia ya kuheshimiana
  2. husababisha kubaguana 
  3. huleta ugomvi 
  4. kudharau wengine [   ]

2. Oanisha fungu A na fungu B ili kupata maana kamili

Fungu A

Fungu B

(i). Tukio la kihistoria [   ]

(ii). Kumpa pole rafiki yako aliyejikwaa [   ]

(iii). Kufanya kazi kwa ushirikiano [   ]

(iv). Kusema uongo [   ]

A. Tendo la huruma

B. Tendo lisilo la maadili

C. Uhusiano mwema

D. Mwaka wa kuzaliwa

 3. Jaza nafasi zilizo wazi kwa kuchagua neno kwenye mabano

(i). Kusaidiana katika jamii huleta ................................................. (umoja na mshikamano/chuki)

(ii). Kusalimia wakubwa ni tendo la ........................................................................... (adabu/huruma)

(iii). Kupigana shuleni ni tendo la ............................................................................... (upendo/ukatili)

(iv). Historia huelezea matukio ............................................................................ (yajayo/yaliyopita)

4. Chunguza matendo kwenye jedwali lifuatalo kisha weka alama ya vema (√) kwenye sehemu inayohusika kuainisha kama ni tendo linalofaa au lisilofaa.

Tendo

Tendo linalofaa

Tendo lisilofaa

(i). Kuwasalimia wazazi

 

 

(ii). Kuiba matunda

 

 

(iii). Kuomba msamaha unapokosea

 

 

(iv). Kutukana wenzako

 

 

5. Soma habari kisha jibu maswali

Vyanzo vya taarifa za Historia ya Tanzania ni vitu mbalimbali vinavyotuwezesha kupata taarifa za matukio yaliyowahi kitokea hapa nchini. Vyanzo hivyo ni kama kusikiliza masimulizi, kusoma vitabu na makumbusho ya Taifa. Vyombo vya habari na tovuti vinaweza pia kuwa ni vyanzo vya kupata taarifa za kihistoria. Vyanzo vya taarifa ya Historia ya Tanzania hutusaidia kupata taarifa za matukio yaliyowahi kutokea katika nchi yetu. Mfano wa tukio la kihistoria ni muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao ulifanyika tarehe 26 Aprili 1964.

MASWALI

(i). Je, ni upi umuhimu wa vyanzo vya taarifa za historia ya Tanzania? . . . . . . . . . . . . ...

(ii). Chanzo cha taarifa za historia ya Tanzania ambacho huhusisha mazungumzo ya mdomo kinaitwajwe? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ...

(iii).Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulifanyika lini? . . . . . . . . . . . . . . . . . . ... . . .

(iv). Taja vyanzo viwili tu vya historia ya Tanzania. 

(i) . . . . . . . . . .. . .. ii. . . . . . . . . . .....

6. Tizama picha ifuatayo, kisha jibu maswali

image

 (i).Picha hiyo inaonesha mazingira ya wapi? . . . . . . . . . . . . . . . ...

(ii).Je, ni akina nani unawaona kwenye picha hiyo? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

(iii).Hao Watoto unaowaona kwenye picha wamesimama. Unadhani kwanini wamesimama? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ...

(iv).Unafikiri tendo wanalolitenda kwa kusimama ni la heshima au dharau? . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . ..

LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD THREE EXAM SERIES 102

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA KUJIPIMA KWA SHULE ZA MSINGI 

MACHI 2025

DARASA LA TATU HISTORIA YA TANZANIA NA MAADILI

 

  1. Tumia maneno yafuatayo kujaza swali la 1 hadi 5 

 

  1.   Raisi wa kwanza wa Tanganyika alikua anaitwa 
  2.  Kabla ya mungano Tanzania ilikua inaitwa 
  3. Kusaidiai kuwatunza, kuwatharnini na kuwalea wazee ni  
  4. Taifa la kwanza kuitawala na kufanya koloni lake Tanganyika 
  5.  Tanganyika na Zanzibar ziliungana mwaka 1964 na kuunda jamuhtiriya

2. Andika majibu matendo yasiyofaa au yanayofaa 

i. Kutokupenda kufanya kazi  

ii. Kuwahi shuleni  

iii. Kuchelewa kurudi nyumbani  

iv. Kutoroka shuleni 

v. Kuwasaidia wasiojiweza  

3. Toa majibu katika maswali yafuatayo 

i.  Historia ya Tanzania ni elimu kuhusu matukio yaliyojitokea nchini 

ii. Maadili ni nini?  ……………………….

iii. Historia inaweza kuhusu maisha yetu binafsi, familia au ………………

iv. Raisi wa awamu ya pili wa Jamuhuri ya muungano alikuwa anaitwa………… 

v. Kuwasaidia mzigo watu wazee ni miongoni mwa matendo  katika jamii ………………..

SEHEMU B: 4. JIBU NDIYO AU HAPANA 

i. Kuwathamini na kuwalea wazee ni matendo ya kimaadili 

ii. Kuwaheshimu watu waliokuzidi umru sio jambo la kimaadili 

iii. Kusema ukweli ni jambo la kimaadili   

iv. Sehemu mojawapo ya vyanzo vya historia ya Tanzania ni makumbusho ya taifa  

v. Kuwanyanganya na kuwadhalilisha ni jambo la kimaadili 

 

LEARNINGHUBTZ.CO.TZHISTORIA STANDARD THREE EXAM SERIES 99

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256