JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA
MTIHANI WA KUHITIMU KIDATO CHA INNE
021 KISWAHILI
(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)
Muda: Saa 3 Mwaka: 2024
Maelekezo
Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na moja (11).
Jibu maswali yote katika sehemu A na B, na maswali mawili (2) kutoka sehemu C ambapo swali la tisa (9) ni la lazima.
Sehemu A ina alama kumi na sita (16), sehemu B alama hamsini na nne (54) na sehemu C ina alama thelathini (30).
Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi.
Vifaa vya mawasiliano na vitu visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.
Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.
SEHEMU A (Alama 16)
Jibu maswali yote katika sehemu hii.
l . Katika kipengele (i) hadi (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo kwenye kijitabu chako cha kujibia.
(i) Vifuatavyo ni vyanzo vya misimu, isipokuwa
Tanakali sauti au milio
Sayansi na Teknolojia
Shughuli maalumu
Utani katika jamii
Mabadiliko ya kihistoria
Choose Answer :
(ii) Neno lenye mofu ya mtendwa ni lipi kati ya haya?
Aliyetembelea
Alimtembelea
Alivyotembea
Atakayetembea
Ametembea
Choose Answer :
(iii) Msaada wako umenifaa sana. Asante! Nena "Asante!" ni aina gani ya neno?
Nomino
Kivumishi
Kielezi
Kitenzi
Kihisishi
Choose Answer :
(iv) Tamathali ipi ya semi hukipa kitu kisicho binadamu sifa ya ubinadamu?
Taniaba
Tashihisi
Tashibiha
Takriri
Tabaini
Choose Answer :
(v) "Wanafunzi wa Kidato cha Pili wamepigiwa ngoma." Kauli hii inaonesha hali gani?
Kutendana
Kutendeka
Kutendewa
Kutendwa
Kutendea
Choose Answer :
(vi) Tanzu sahihi za Fasihi simulizi ni zipi kati ya zifuatazo?
Ngonjera, mashairi, nyimbo na tenzi
Tarihi ngano, visasili na soga
Semis hadithi, maigizo na ushairi
Methali, misemo, nahau na vitendawili
Michezo, vichekesho, majigambo na ngofijera
Choose Answer :
(vii) Mpangilio mzuri wa muundo wa insha ni upi?
Kichwa, mwanzo, wazo na kiini
Mwanzo, kiini, hitimisho na wazo
Kichwa, wazo, hitimisho na kiini
Kichwa, mwanzo, wazo na hitimisho
Kichwa, mwanzo, kiini na hitimisho
Choose Answer :
(viii) Kwa nini lugha ya mazungumzo ni halisi zaidi?
Wahusika huwasiliana kwa simu
Wahusika huwasiliana ana kwa ana
Wahusika huwasiliana kwa mtandao
Wahusika huwasiliana kwa barua
Wahusika huwasiliana kwå barua pepe
Choose Answer :
(ix) Methali isiyosisitiza uvumilivu naji!ihada katika kazi ni ipi?
Afiriti hafichiki
Mvumilivu hula mbivu
Acha koko uangue koma
Aali hupatikana kwa ghali
Abadi abadi kamba hukata jiwe
Choose Answer :
(x) Tungo ipi ina kiambishi rejeshi kati ya hizi?
Anaondoka
Ameondoka
Aliondoshwa
Amejiondoa
Ameondokewa
Choose Answer :
2. Oanisha fasili za Vipera vya semi zilizopo katika Orodha A na Vipera husika kutoka Orodha B, kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kijitabu chako cha kujibia.
Orodha A
Orodha B
(i) Semi fupi Zinazoeleza kwa emuhtasari fikra au mafunzo mazito yaliyotokana na uzoefu wajamii.
(ii) Semi fupi za mafumbo zinazotumia lugha ya picha na zinazotolewa kwa hadhira zikieleza jambo lenye kuhitaji jibu.
(iii) Semi zilizojengwa kwa pichå kwa kutumia maneno ya kawaida lakini hutoa maana tofauti na maneno yaliyotumika.
(iv) Semi zenye maonyo au mawaidha ambazo maana zake za ndani zimefichika.
(v) Semi zenye picha za mafumbo zinazoonesha ukinzani wa fikra au matukio.
(vi) Semi zinazotumia picha, ishara na tamathali kueleza kitu au wazo kwa ufupi.
4. Ujio wa Waarabu, Wajerumani na Waingereza ulikuwa na mchango mkubwa katika kukuza na kueneza Lugha ya Kiswahili nchini Tanzania kabla ya uhuru. Eleza umuhimu wao kwa kutoa hoja mbili kwa kila taifa.
6. Kwa kutumia hoja şita, fafanua mafanikio sita ya Kamati ya Lugha ya Afrika Mashariki ya mwaka 1930 katika kusimamia usanifishaji wa lugha ya Kiswahili.
8. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata.
Kulikuwa na kiongozi mmoja maarufu aliyekuwa amebobea na kusifika sana katika ukanda wenye misitu minene. Siku zote alikuwa anasisitiza umuhimu wa kupanda miti kabla ya kukata miti. Aidha, kila mara alikuwa anawahamasisha watu juu ya umuhimu wa kupanda miti kuzunguka maeneo yao yote kwa kuamini kuwa akiba haiozi.
Siku moja alialikwa katika shule ya Sekondari Twaweza kuhudhuria mahafali ya kuhitimu Kidato cha Nne. Kabla ya shamrashamra kuanza, alihakikisha kwanza miti inapandwa katika eneo lote la kuzunguka shule. Katika wosia Wake, aliwashawishi wanafunzi kuwa mabalozi wa upandaji miti, utunzaji miti na usafi. Aliwasisitiza kuwa safi kwani usafi ndiyo njia pekee ya kulinda afya zao kwa kuwa afya njema ni mtaji wa mafanikio yao. Vilevile, alikemea vikali tabia ya kutiririsha maji machafu, kutupa takataka ovyo na kujisaidia sehemu zisizostahili.
Aliwasihi wahitimu kuwa, miongoni mwao watapatikana viongozi ambao watakuwa na moyo wa kuendeleza kazi ambayo viongozi waliokuwepo waliithamini sana. Hii itasaidia kuinusuru nchi yetu isije ikavamiwa na madhara ya jangwa baada ya kipindi si kirefu. Ukataji wa miti holela huathiri uoto wa asili, kufukuza mvua na kukaribisha ukame.
Aliendelea kueleza kuwa, hatuna budi kuelewa kwamba ukosefu wa mvua siku zote ndicho chanzo kikuu cha madhila kwa binadamu, wanyama wa mwituni, wanyama wafugwao na hata wadudu na mimea Pia. Kila mmoja akikariri kauli mbiu panda miti kata mti tutakwepa ukame. Hivyo, kila mwanajamii. anapaswa kuienzi kwa dhati kabisa kauli mbiu hii kwani mchelea nzwana kulia, hulia yeye.
Maswali
(a) Andika kichwa cha habari hii kwa maneno matatu.
(b) Eleza maana ya methali zifuatazo kama zilivyotumika katika habari uliyosoma.
Akiba haiozi.
Mchelea mwana kulia, hulia yeye.
(c) Kutokana na habari uliyosoma, taja athari mbili za kukosa mvua kwa binadamu, wanyama, wadudu na mimea.
(d) Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua sitini na yasiyozidi sabini.
SEHEMU C (Alama 30)
Jibu maswali mawili (2) kutoka katika sehemu hii. Swali la tisa (9) ni la lazima na kila swali lina alama 15.
ORODHA YA VITABU
USHAIRI
Wasakatonge - M. S. Khatibu (DUP)
Malenga Wapya - TAKILUKI (DUP)
Mashairi ya Chekacheka - T. A. Mvungi (EP & D. LTD)
10. "Mapenzi ya dhati huleta faraja miongoni mwa wanajamii." Thibitisha kauli hii kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila riwaya kati ya riwaya mbili ulizosoma.
11. Kwa kutumia hoja tatu kwa kila kitabu katika tamthiliya mbili ulizosoma, eleza namna wasanii walivyotumia dhamira mbalimbali ili kuakisi jamii ya leo.