FORM FOUR KISWAHILI NECTA 2015

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL

CERTIFICATE OF SECONDARY EDUCATION EXAMINATION

021 KISWAHILI

(Kwa Watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)

Muda: Saa 3:00 Jumatatu, 02 Novemba 2015 asubuhi

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B, C, D na E.

  1. Jibu maswali yote katika sehemu A, B na D, swali moja (1) kutoka sehemu C na maswali matatu (3) kutoka sehemu E. Swali la 15 ni lazima.

  1. Zingatia maagizo ya kila sehemu na ya kila   swali.

  1. Simu za mkononi haziruhusiwi katika chumba cha mtihani.

  1. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

SEHEMU A (Alama 10) UFAHAMU

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Soma kwa makini kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata.

Ustaarabu ni jambo jema ambalo hupendwa na kila jamii yenye utashi hapa duniani. Kila jamii yenye ustaarabu mambo yake huendeshwa kwa kuzingatia kanuni na taratibu zinazoeleweka. Maamuzi na mafanikio mbalimbali miongoni mwa wanajamii hutolewa bila hamaki wala kukurupuka. Kanuni na taratibu hizo huiongoza jamii kufikia upeo wake kimaendeleo kuanzia ngazi za chini kabisa ambayo ni familia mpaka ngazi ya juu kabisa ambayo ni taifa. Taratibu na kanuni hizo huwekwa katika chombo kimoja maalumu kinachoitwa katiba.

Katiba ni jumla ya sheria, kanuni na taratibu fulani zilizokubaliwa kuwekwa na jamii au taifa fulani kama dira ya maisha ya kila siku ya jamii au taifa hilo. Taifa bila katiba ni sawa na behewa la garimoshi bila injini. Hivyo katiba ina umuhimu wa kipekee katika taifa lolote lile.

Katika nchi zenye utamaduni wa kidemokrasia, katiba huundwa kutokana na maoni ya wananchi wake kwa utaratibu maalumu uliowekwa na serikali. Aghalbu, maoni na mawazo yaliyotolewa na wananchi huwa ni chimbuko la katiba hiyo. Wananchi hujiona ni sehemu ya utawala. Kwa upande wa pili wa sarafu, nchi zenye utaratibu wa kiimla, katiba hutayarishwa na watawala kwa maslahi yao binafsi. Katiba hutumiwa kama sera kwa maslahi ya watawala. Maoni na mawazo ya wananchi hayazingatiwi katika kuunda katiba.

Umuhimu wa katiba huonekana na kujidhihirisha waziwazi katika maisha ya kila siku ya nchi yoyote ile. Kwanza, katiba huelekeza wajibu wa ila mwanajamii kwa taifa lake na wajibu wa viongozi walio madarakani kwa wananchi au raia. Pili, katiba huonesha na kuainisha haki ambazo kila raia anastahili kupata na pia taratibu za kufuata katia kudai au dupewa haki hizo. Mbali na hayo, katiba hutoa utaratibu wa jinsi ya kuwapata viongozi wetu katika ngazi mabalimbali za kisiasa na kijamii. Pia uhuru wa mtu binafsi hulindwa na katiba. Hivyo, katika nchi ambayo ina katiba inayokidhi matarajio ya wananchi wote mambo huwa mazuri na kamwe chombo hakiwezi kwenda mrama.

Aidha, wananchi hawana budi kuelewa maana ya katiba ili waweze kutoa maoni na mapendekezo ya kuunda katiba mpya au kuimarisha iliyopo. Ni muhali kwa mtu asiyejua maana ya katiba kutoa maoni kuhusu katiba. Wananchi hupaswa kuelimishwa kupita semina, warsha na makongamano mbalimbali ili kujua katiba zao na kutoa maoni kuhusu uundaji wa katibu mpya.

Hata hivyo, wananchi wengi hasa vijana hawajitumi katika kuzijua katiba za nchi zao au kutoa maoni ya uundaji wa katiba mpya. Athari zake ni kutojua haki zao za msingi na kuburutwa kama mkokoteni na watawala katika mambo mbalimbali. Vilevile hulalamikia mambo ambayo hawakuchangia mawazo.

Hivyo basi, ni vizuri kwa wananchi kutambua, kuthamini na kuheshimu uwepo wa katiba kama kiongozi kizuri katika kuonesha njia muafaka ya kujiletea maendeleo kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni kwa nchi husika.

Maswali

(a)  Toa maana ya maneno yote yaliyokolezwa wino kama yalivyotumika katika habari uliyosoma.

View Ans


(b) Kwa mujibu wa habari uliyosoma, taja mambo mazuri mawili yatokanayo na uwepo wa katiba katika nchi.

View Ans


(c)  Kwanini mwandishi anasema katiba hutumiwa kama sera kwa maslahi ya watawala?

View Ans


(d) Je, ni hofu gani aliyonayo mwandishi dhidi ya vijana kuhusu katiba?

View Ans


(e) Andika kichwa cha habari uliyosoma kisichozidi maneno matano (5).

View Ans


2. Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua mia moja (100).

View Ans


SEHEMU B (Alama 25) SARUFI NA UTUMIZI WA LUGHA

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

3. Watumiaji wa lugha ya Kiswahili hufanya makosa mengi bila ya kudhamiria. Taja aina mbili za makosa hayo kwa kutoa mfano wa sentensi mbili kwa kila kosa.

View Ans


4. (a) Eleza maana ya rejesta.

View Ans


(b) Kwa kutoa mifano, taja mambo muhimu matatu yanayomwongoza mtumiaji wa lugha katika uteuzi wa rejesta.

View Ans


5. Katika kila sentensi andika neno moja lenye maana sawa na maelezo ya sentensi husika.

  1. Mtu anayechunguza uhalifu.

  2. Ng’ombe dume aliyehasiwa.

  3. Chombo cha usafiri kinachopita juu ya vyuma.

  4. Mti unaozaa matunda yanayotengenezwa kinywaji cha kahawa.

  5. Sehemu ndogo ya nchi iliyochongoka na kuzungukwa na bahari katika sehemu zake tatu.

View Ans


6. Eleza dhima za mofimu "li" kama ilivyotumika katika sentensi zifuatazo:

  1. Shamba letu li kubwa sana.

  2. Wlishelewa kurudi.

  3. Tunalifuatilia.

  4. Limeharibika.

  5. Shikilia.

View Ans


7. Andika sentensi zifuatazo katika hali ya ukanushi:

  1. Ameshiba sana.

  2. Watoto wengi wanaogelea.

  3. Mvua ilinyesha kwa wingi sana.

  4. Kijana anakula chakula kingi.

  5. Mimi nasoma polepole.

View Ans


SEHEMU C (Alama 10) UANDISHI

Jibu swali moja (1) kutoka sehemu hii.

8. Jifanye wewe ni Gudhah Mukish anayeishi mtaa wa Tandamti - Gerezani Kariakoo na unataka kuuza gari yako aina ya TOYOTA CARINA. Andika tangazo kwenye gazeti la Mwananchi.

View Ans


9. Andaa kadi ya mwaliko kwa rafiki zako ili washiriki katika mahafali ya kumaliza Kidato cha Nne yatakayofanyika shuleni kwako siku ya Jumamosi tarehe 21/11/2015, kisha kufuatiwa na tafrija fupi itakayoandaliwa na wazazi wako katika ukumbi wa Kijiji mnamo saa 10.00 jioni. Jina lako liwe Sili Silali wa SHule ya Sekondari Kiriche.

View Ans


SEHEMU D (Alama 10) MAENDELEO YA KISWAHILI

Jibu swali la kumi (10)

10. Chama cha Kiswahili cha Afrika (CHAKA) ni miongoni mwa taasisi zilizojitahidi katika kukuza na kueneza Kiswahili Barani Afrika. Eleza majukumu matano ya chama hiki katika kufanikisha azma hiyo.

View Ans


SEHEMU E (Alama 45) FASIHI KWA UJUMLA

Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii. Swali la 15 ni la lazima.

ORODHA YA VITABU

Ushairi

Wasakatonge - M.S. Khatibu (DUP)

Malenga Wapya - TAKILUKI (DUP)

Mashairi   ya   Chekacheka - T.A. Mvungi (EP & D.LTD)

Riwaya

Takadini - Ben J. Hanson (MBS)

Watoto   wa   Maman’tilie - E. Mbogo (H.P)

Joka la Mdimu - A.J. Safari (H.P.)

Tamthiliya

Orodha - Steve Reynolds (MA) Ngoswe Penzi Kitovu   cha   Uzembe - E. Semzaba (ESC) Kilio Chetu - Medical Aid Founda

11. Kwa kutumia mifano, fafanua kanuni muhimu nne za utunzi wa mashairi ya kimapokeo.

View Ans


12. "Kazi za fasihi hufichua mivutano iliyopo katika jamii." Kwa kutumia hoja tatu kwa kila diwani fafanua mivutano hiyo kutoka katika diwani mbili ulizosoma.

View Ans


13. "Mandhari iketeuliwa vizuri humsaidia mwandishi katika kufikisha yale aliyokusudia kwa jamii yake" Thibitisha hoja hiyo kwa kutoa mifano mitatu toka katika kila kitabu kati ya riwaya mbili zilizoorodheshwa.

View Ans


14. Kwa kutumia tamthiliya mbili miongoni mwa zilizoorodheshwa eleza jinsi waandishi walivyoonesha athari za utamaduni wa kigeni katika maadili ya jamii ya kiafrika.

View Ans


15. (a) Vigano ni nini?

(b) Tunga vigano kwa kutumia methali isemayo "Umdhaniaye siye kumbe ndiye!"

View Ans


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256