FORM TWO KISWAHILI NECTA 2024

 Namba ya Upimaji Ya Mwanafunzi . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI

021 KISWAHILI

Muda: 2:30 Mwaka: 2024

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi (10).
  2. Jibu maswali yote kwenye nafasi ulizopewa.
  3. Sehemu A na C zina alama kumi na tano (15) kila moja na sehemu B ina alama sabini (70).
  4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
  5. Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi.
  6. Vifaa vya mawasiliano visivyoruhusiwa havitakiwi kafika chumba cha upimaji.
  7. Andika Namba yako ya Upimaji katika kila ukurasa sehemu ya juu upande wa kulia.

KWA MATUMIZI YA MTAHINI TU

NAMBA YA SWALI ALAMA SAHIHI YA MTAHINI
1.

2.

3.

4.

5.

6.

7.

8.

9.

10.

JUMLA

SAHIHI YA MHAKIKI

SEHEMU A (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

l . Katika vipengele (i) hadi (x), chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika kisanduku ulichopewa.

(i) Mtunzi wa mashairi hutumia miundo ya aina mbalimbali ili kuipa upekee kazi yake. Upi ni muundo wa 'tarbia' kati ya ifuatayo?

  1. Mistari miwili kwa kila ubeti 
  2. Mistari mitatu kwa kila ubeti
  3. Mistari minne kwa kila ubeti 
  4. Mistari mitano kwa kila ubeti
Choose Answer :


(ii) Kati ya vipengele vifuatavyo ni kipi hakihusiani na maudhui ya kazi ya fasihi?

  1. Mafunzo 
  2. Mtazamo
  3. Msimamo
  4. Msisitizo
Choose Answer :


(iii) Sentensi ipi kati ya zifuatazo imeundwa kwa kuunganisha sentensi mbili?

  1. Mwalimu ameingia darasani kufundisha.
  2. Mama alichota maji lakini yamemwagika. 
  3. Shule yetu ya msingi ni kubwa na nzuri. 
  4. Mvua na mawingu hutegemeana daima.
Choose Answer :


(iv) Kwa kawaida, habari iliyofupishwa huwa na idadi ipi ya maneno kati ya haya?

  1. Nusu ya maneno yote
  2. Theluthi ya maneno yote
  3. Robo ya maneno yote
  4. Robo tatu ya maneno yote
Choose Answer :


(v) Neno lipi linadhihirisha kauli ya kutendwa katika kitenzi?

  1. Pikia 
  2. Pikiwa 
  3. Pikika 
  4. Pikwa
Choose Answer :


(vi) Ni seti ipi inawakilisha kikarnilifu muundo wa mfumo wa lugha-yoyote? 

  1. Sauti, silabi, maneno na sentensi
  2. Sauti, silabi, irabu na maneno
  3. Silabi, irabu, maneno na sentensi
  4. Sauti, irabu, konsonanti na maneno
Choose Answer :


(vii) Katika maneno yafuatayo, ni orodha ipi yenye aina moja ya maneno? 

  1. Bata, nyumba, uvivu, Kigoma
  2. Bata, nyumba, kula, Kigoma
  3. Nyumba, nywele, uvivu, pika
  4. Nywele, pika, andika, bata
Choose Answer :


(viii) Tamathali ya semi inayolinganisha Vitu au hali mbili tofauti kwa kutumia viunganishi huitwaje?

  1. Takriri 
  2. Sitiari 
  3. Tashihisi 
  4. Tashbiha
Choose Answer :


(ix.) Jambo lipi kati ya yafuatayo ni muhimu kuzingatiwa katika uandishi wa insha?

  1. Kujua jina halisi la mwandishi wa insha
  2. Kujua barabara jambo linaloandikiwa insha
  3. Kujua wahusika wanaoandikiwa insha
  4. Kujua barabara mahali pa kuandikia insha
Choose Answer :


(x) ni sifa mahususi ya lugha ya mazungumzo?

  1. Matumizi ya ishara
  2. Matumizi ya alama
  3. Matumizi ya ala
  4. Matumizi ya lahaja
Choose Answer :


2. Oanisha maana ya dhana za kisarufi zilizo katika Orodha A na dhana husika kutoka Orodha B, kisha andika jibu sahihi katika kisanduku ulichopewa.

Orodha A

Orodha B

(i) Sehemu ya neno ambayo haibadiliki.

(ii) Umbo linalowakilisha mofimu.

(iii) Kipashio kidogo kabisa chenye maana katika neno.

(iv) MäUmbo ambayo hayawezi kujitegemea yakiwa pekee.

(v) Kipashio kinachoweza kuambatishwa kwenye mzizi wa neno na kuunda neno jipya.

  1. Mofu
  2. Mofu huru
  3. Mofimu
  4. Kiambishi
  5. Mofu tegemezi
  6. Mzizi
  7. Sarufi
View Ans


SEHEMU B (Alama 70)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

3. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:

Miti ina faida nyingi sana katika maisha ya binadamu. Nchi isiyo na miti ni sawa na mtu atembeaye bila kuvaa nguo. Ipo miti ya asili na mingine ni ya kupandwa, yote hiyo ina faida lukuki kwa maisha ya binadamu.

Ongezeko la watu duniani na kutokuwa na nishati mbadala kama vile gesi na umeme hasa sehemu za vijijini kumesababisha matumizi lufufu ya kuni na mkaa. Matumizi haya yametokana na ukosefu wa elimu ya utunzaji wa mazingira. Hali hii imesababisha jangwa kwa kuwa waswahili husema, "chovya chovya humaliza buyu la asali.'

Miti ina faida kadhaa katika maisha ya kiumbe yeyote duniani. Miti hutupatia hewa safi tunayoivuta kila sekunde ya uhai wetu, kutengenezea fanicha, kutupatia matunda ili kutukinga na magonjwa na harufu ya miti ni dawa dhidi ya maadui mbalimbali kama vile nyoka.

Ukataji miti ovyo una madhara kama vile ukame, mmomonyoko wa udongo, uhaba wa hewa safi ya oksijeni na athari nyingine nyingi zinazoondoa uwepo wa viumbe hai na viumbe visivyo hai.

Kwa sasa serikali yetu imeanzisha kampeni mbalimbali za kulinda mazingira kama vile, "kata mti panda mti", "mti wa milenia" na "mtu mmoja miti mingi." Kampeni hizo hutolewa katika redio, runinga na vyombo vingine vya habari. Ni jukumu la kila mtu kuitunza na kuilinda misitu yetu.

Maswali:

(a) Kutokana na habari uliyosoma;

  1. Andika kichwa cha habari kwa maneno yasiyozidi matano.
  2. Unafikiri kwa nini kumekuwa na wimbi kubwa la ukataji wa miti?
  3. Bainisha matumizi manne ya miti.

(b) Kulingana na habari uliyosoma, kampeni mbalimbali zinazotolewa katika vyombo vya habari Zina umuhimu gani katika jamii?

(c) Fupisha habari uliyosoma kwa maneno yasiyopungua 60 na yasiyozidi 70.

View Ans


4. Katika kipengele (a) — (e), bainisha dhima mbili kwa kila kiambishi kilichokołeżwa wino.

(a) Babu atakuja kesho asubuhi.

(b) Ukuta umeanguka.

(c) Mwalimu alimfundisha Bahati.

(d) Ninakupenda.

(e) Sitaimba wimbo kesho.

View Ans


5. Bainisha shina la neno katika vitenzi vifuatavyo:

  1. Analima 
  2. Alipiga .
  3. Wanacheza
  4. Kilianguka
  5. Atachapa
View Ans


6. Fafanua sifa tano za lugha.

View Ans


7. Eleza dhima tano za rejesta katika lugha.

View Ans


8. Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata:

Mada iliyo moyoni, hii ninawaletea,
Watoto wa mitaani, mada nimeshafungua,
Wanapata mitihani, katika hii dunia,
Nawaonea huruma, imewatupa dunia.

Wanashinda jalalani, hayo ndiyo mazoea,
Umkute kituoni, anaomba abiria,
Ni njaa mwake tumboni, ndiyo inamsumbua,
Ataomba kwa imani, huku anakulilia.

Wapo pia maaluni, vibaya wamezoea,
Hawaombi wala nini, kazi yao kukwapua,
Husimama vituoni, abiria kuvizia,
Abiria wanalia, kila kitu kimekombwa.

Twajenga taifa gani, watoto kuachilia?
Wazurure mitaani, na sisi twachekelea,
Tunadhania utani, na mwishowe tutalia,
Kwani mzaha mzaha, huutumbua usaha.

Maswali

(a) Bainisha;

(i) Muundo wa shairi:

(ii)Mtindo wa shairi:

(b) Eleza dhamira ya mwandishi katika ubeti wa pili.

(c) Eleza kwa kifupi ujumbe wa shairi hili.

(d) Toa methali nyingine moja yenye maana sawa na methali "Mzaha mzaha, hutumbua usaha" kama ilivyotumika katika shairi.

(e) Andika kichwa cha habari cha shairi hili kisichozidi maneno matano na kisichopungua maneno matatu.

View Ans


9. Bainisha tofauti tano zilizopo kati ya fasihi simulizi na fasihi andishi.

View Ans


SEHEMU C (Alama 15) 

Jibu swali la kumi (10).

10. Badili barua ifuatayo kuwa simu ya maandishi kwa kutumia maneno yasiyozidi kumi (10).

Shule ya Sekondari Busega,

S.L.P 1010,

KASULU.

10/11/2015.

Mpendwa kaka Haruna Mashaka, kwanza shikamoo!

Habari za hapo nyumbani? Wazazi wetu na wengine wote huko hawajambo? Mimi huku shuleni sijambo naendelea vizuri na masomo yangu.

Dhumuni la barua hii ni kukufahamisha kuwa nilipokuwa safarini kutoka nyumbani kuja shuleni, kwa bahati mbaya niliibiwa fedha za karo ya shule ulizonipa, hivyo bado nadaiwa karo ya shule. Tafadhali kaka nisamehe kwa usumbufu ninaokusababishia, nitumie fedha zingine kwa ajili ya karo ya shule.

Kwa leo ni hayo tu.

Mdogo wako

Neema Mashaka.

View Ans


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256