FORM TWO KISWAHILI NECTA 2022

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI

021 KISWAHILI

Muda: 2:30 Mwaka : 2022

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B, na C zenye jumla ya maswali kumi (10)
  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na swali moja (1) kutoka sehemu C.
  3. Sehemu A na C zina alama kumi na tano (15) kila moja na sehemu B ina alama sabini (70)
  4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
  5. Majibu yote yaandikwe kwenye nafasi ulizopewa
  6. Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi
  7. Vifaa vyote vya mawasiliano visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha upimaji.
  8. Andika Namba yako ya Upimaji katika kila ukurasa sehemu ya juu upande wa kulia

KWA MATUMIZI YA MPIMAJI TUU

NAMBA YA SWALI

ALAMA

SAHIHI YA MPIMAJI

1.

2.

3.

4.

5.

6.

7.

8.

9.

10.

JUMLA

SAHIHI YA MHAKIKI


SEHEMU A (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Katika vipengele (i) hadi (x) chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo katika kisanduku ulichopewa.

(i) Seti ipi ni sahihi kuhusu vipengele vya fani katika fasihi simulizi?

  1. Dhamira, migogoro, mtindo na mafunzo.
  2. Ujumbe, matumizi ya lugha, wahusika, mtindo na muundo
  3. Wahusika, matumizi ya lugha, muundo, mtindo na mandhari
  4. Migogoro, ujumbe, wahusika, mafunzo na mtindo.
Choose Answer :


(ii) Ni muundo upi wa ushairi wa fasihi simulizi unaundwa na mistari/mishororo mitano?

  1. Sabilia
  2. Takhmisa
  3. Tathmisa
  4. Tathilitha
Choose Answer :


(iii) Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia yana athari chanya na hasi katika ukuaji wa fasihi simulizi. Zipi ni athari hasi zinazoikabili fasihi simulizi?

  1. Hupunguza hadhi na ubora wa kazi fasihi
  2. Huhifadhi kazi za fasihi simulizi kwa muda mrefu.
  3. Huboresha uwasilishaji wa kazi za fasihi simulizi
  4. Hutunza kiini au maana ya ujumbe wa fasihi simulizi
Choose Answer :


(iv) Sababu zifuatazo husababishwa kutokea kwa utata katika tungo, isipokuwa:

  1. Neno kuwa na maana zaidi ya moja
  2. Kuzingatia taratibu za uandishi
  3. Kutumia maneno yenye maana ya picha
  4. Kutotamka neno ulilokusudia kwa usahihi
Choose Answer :


(v) Juma huimba vizuri sana. Nneo linalopigiwa msitari linafanya kazi ya aina ipi ya neno?

  1. Kielezi
  2. Kivumishi
  3. Kitenzi
  4. kihisishi
Choose Answer :


(vi) Wewe na rafiki yako mmepewa kazi ya kubainisha sentensi yenye vivumishi vya a-unganifu katika tungo. Je ni sentensi ipi katika ya zifuatazo itakuwa sahihi?

  1. Juma anacheza kwa madoido
  2. Halima mrefu amefika
  3. Abdul na Zuberi wameondoka jana
  4. Janeth wa Dodoma ameingia darasani
Choose Answer :


(vii) Kati ya kanuni zifuatazo mojawapo si sahihi kuhusu usimulizi wa matukio

  1. Kutamka matamshi kwa usahihi
  2. Mpangilio mzuri wa mawazo
  3. Kujua muundo wa matukio kwa usahihi
Choose Answer :


(viii) Kati ya alama zifuatazo, alama ipi hutumika badala ya kiunganishi cha kuunga tungo mbili

  1. Nukta (.)
  2. Nukta pacha (:)
  3. Mkato (,)
  4. Alama ya mshangao (!)
Choose Answer :


(ix) Ipi ni dhima sahihi ya kutumia picha na michoro katika kamusi?

  1. Hufanya kamusi kutambulika kwa haraka
  2. Hufanya kamusi kupendwa na wasomaji
  3. Hupunguza umakini na idadi ya watumiaji
  4. Husaidia wasomaji kuwa na kumbukumbu
Choose Answer :


(x) Ipi ni maana sahihi ya shina la neno kati ya zifuatazo?

  1. Sehemu ya neno yenye mzizi na viambishi awali na tamani
  2. Sehemu ya neno yenye mzizi na viambishi awali pekee
  3. Sehemu ya neno yenye mzizi na viambishi tamati pekee
  4. Sehemu ya neno yenye mzizi na kiambishi tamati vijenzi.
Choose Answer :


2. Oanisha dhima za nyimbo za fasihi simulizi zilizo katika Orodha A na aina za nyimbo kutoka Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi katika kisanduku ulichopewa.

Orodha A

Orodha B

  1. Nyimbo zinazoimbwa ili kuburudisha watu
  2. Nyimbo za kuaga mwaka
  3. Nyimbo za kuaga mwaka
  4. Nyimbo zinazoimbwa kwenye maombolezo kama misiba
  5. Nyimbo zinazoimbwa kwenye shughuli za kilimo
  6. Nyimbo zinazoimbwa kwenye jando na unyago
  1. Nyiso
  2. Kimai
  3. Bembezi
  4. Mbolezi
  5. Tumbuizo
  6. Wawe
  7. Kongozi
View Ans


SEHEMU B (Alama 70)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

3. Soma kifungu cha habari kifuatacho kisha jibu maswali yanayofuata:

Baba mmoja aliishi na mkewe na mwanae wa pekee wa kike. Baba huyu alikuwa mtu wa kufuata maadili, mila na desturi za kiafrika. Alitamani kila mmoja ndani ya nyumba aishi maisha ya kimalaika. Hakupenda mtu yeyote kwenda kinyume na mawazo yake ili maisha yake yasiende mrama., hasa mwanae aliyekuwa mboni ya jicho lake.

Binti yule akawa mtoto wa getikali, hakuna cha disko wala ufukweni, mama yake naye hakuruhusiwa kujipamba kiasi ch kupitiliza, ikiwemo kusuka nywele kwa mitindo ya kisasa. Mama na binti yake walilazimika kutii kwa kumuogopa baba yule wa miraba minne, mwenye kuongea kwa mrindimo.

Siku moja binti yake aliwazua, akabaini kwamba pale nyumbani hapakuwa na maisha anayoyahitaji, akaamua kufanya uamuzi mbaya wa kutoroka usiku. Baba na mama hawakujua mtoto alikokwenda. Mama akashikwa na kihoro akaumwa sana hatimaye umauti ukamfika.

Baba alisikitika sana, akatafakari na kutafakari, hatimaye akagundua kuwa msimamo wake haukuwa sahihi na kwamba alitakiwa kupokea mawazo na kusikiliza ushauri toka kwa wengine. Vilevile akagundua kuwa hakuna mtu aliyemkamilifu kwan binadamu wote tuna upungufu.

Maswali 

(a) Pendekeza kichwa cha habari kinachofaa kwa habari uliyosoma kisichozidi maneno matano.

(b) Eleza maana ya maneno/vifungu vya maneno vifuatavyo kama vilivyotumika katika habari uliyosoma.

  1. Mrama
  2. Mboni ya jicho lake
  3. Geti kali
  4. Miraba minne
  5. Kihoro

(c) (i) Unadhani kwa nini yule binti aliamua kutoroka nyumbani kwao?

(ii) Baba wa familia hii alikuwa na tabia gani?

(d) Andika funzo linalopatikana katika habari hii

View Ans


4. Bainisha umbo linalodhihirisha kauli katika maneno yafuatayo kisha taja kauli husika kwa kila neno.

Mfano: Anasomea

(i) Umbo la kauli - e -

(ii) Kauli yenyewe - kauli ya kutendea

(a) Wanapigana

  1. Umbo la kauli
  2. Kauli yenyewe

(b) Atatusomesha

  1. Umbo la kauli
  2. Kauli yenyewe

(c) Limelimwa

  1. Umbo la kauli
  2. Kauli yenyewe

(d) Amechomewa

  1. Umbo la kauli
  2. Kauli yenyewe

(e) Amepigika

  1. Umbo la kauli
  2. Kauli yenyewe
View Ans


5. Bainisha viwakilishi katika tungo zifuatazo na kwa kila moja onesha ni kiwakilishi cha aina gani.

Mfano: Hili limeoza.

  1. Kiwakilishi -hili
  2. Aina-kiwakilishi cha kuonesha.

(a) Yule hapendi ugali

  1. Kiwakilishi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  2. Aina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

(b) Sisi tunapenda kusoma.

  1. Kiwakilishi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  2. Aina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

(c) Mtoto wangu amerudi, wako hajarudi.

  1. Kiwakilishi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  2. Aina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

(d) Wengi wamepokelewa vizuri

  1. Kiwakilishi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  2.  Aina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

(e) Mrefu wa kimo amefika

  1. Kiwakilishi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
  2. Aina . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .
View Ans


6. Eleza dhima tano za lugha

View Ans


7. Fafanua sifa tano za misimu katika lugha ya kiswahili

View Ans


8. Ni mafunzo gani yanayopatika katika methali zifuatazo?

  1. Samaki mkunje angali mbichi
  2. Mchumia juani hulia kivulini
  3. Akiba haiozi
  4. Safari ni hatua
  5. Akili ni nywele kila mtu ana zake.
View Ans


9. Kazi za fasihi huhifadhiwa kwa njia mbalimbali. Fafanua njia tnao za kuhifadhi kazi hizo.

View Ans


SEHEMU C (Alama 15)

Jibu swali la kumi (10)

10. Kwa maneno yasiyopungua 150 na yasiyozidi 200, andika insha yenye hoja nne kuhusu umuhimu wa Michezo.

View Ans


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256