FORM THREE ELIMU YA DINI YA KIISLAMU EXAMS SERIES

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA OFISI YA WAZIRI MKUU-TAMISEMI

MTIHANI WA MUHULA WA KWANZA KIDATO CHA TATU MEI 

MSIMBO: 015 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU 

Muda: Saa 3

MAELEKEZO 

  • Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na moja (11).
  • Jibu maswali yote katika sehemu A na B, na maswali mawili (2) kutoka sehemu C.
  • Sehemu A ina alama kumi na sita (16), sehemu B ina alama hamsini na nne (54) na sehemu C ina alama thelathini (30).
  • Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
  • Vifaa vya mawasiliano na vitu visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha Mtihani.
  • Andika jina lako katika kila ukurasa wa karatasi ya kujibia.

SEHEMU A (Alama 16)

Jibu maswali yote kutoka katika sehemu hii 

1. Katika kipengele (i) – (x) chagua jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu hilo kwenye karatasi ya kujibia.

(i) “Amemfundisha mwanadamu mambo aliyokuwa hayajui.” (96:5). Aya hii inathibitisha kitu gani?

  1. Kusoma ni amri ya Allah (S.W)
  2. Chanzo cha elimu zote ni Allah (A.S) (S.W) 
  3. Elimu ni faradhi kwa Waislamu wote
  4. Allah (S.W) alimfundisha Adam
  5. Mwanadamu ameumbiwa elimu.

(ii) Firauni katika Maisha yake alikuwa akikanusha uwepo wa Allah (S.W), lakini siku alipokuwa anazamishwa baharini akakiri uwepo wake. Ni jambo gani lilimfanya kutambua hilo?

  1. Hisia za kumjua Allah alizopandikizwa kwenye maumbile yake
  2. Uzito wa umauti aliokuwa akiupata wakati anaangamia
  3. Mateso ya kifo aliyokuwa akiyapata wakati anazama
  4. Wakati anazama alioneshwa Allah wazi wazi
  5. Malaika mtoa roho alimjia na kumuonesha ukweli juu ya Allah.

(iii)Watu wa Nabii Lut (A.S) waliangamizwa kutokana na maovu mbalimbali. Maovu gani utakayowakataza watu wa jamii yako ili wasikutwe na yaliyowakuta watu hawa? 

  1. Ujambazi na zinaa 
  2. Kupunja vipimo na ujambazi
  3. Ujambazi na kumshirikisha Allah 
  4. Kuingiliana wanaume kwa wanaume na ujambazi
  5. E. Kumshirikisha Allah na kuingiliana (S.W) wanaume kwa wanaume.
(iv) Nyonda ni kijana aliyejitenga na jamii kwa ajili ya kufanya ibada, amesema hataoa wala kutafuta mali ili awe karibu zaidi na Mola wake. Kijana huyu atakuwa ni mfuasi wadini gani?
  1. Upagani 
  2. Ukafiri 
  3. Ushirikina
  4. Utawa
  5. Uislamu
(v) “Bali hii ni Qur’an tukufu. Katika ubao uliohifadhiwa.” Qur’an (85:21-22). Baada ya hatua hii nihatua gani iliyofuata katika ushukaji wa Qur’an?
  1. Kuhifadhiwa kwenye vifua vya Maswahaba wa Mtume
  2. Kushuka moja kwa moja kwa Mtume wa watu wote
  3. Kushuka yote mpaka kwenye uwingu wa kwanza wa dunia
  4. Kuandikwa kwenye karatasi na ngozi za wanyama
  5. Kushuka kwa Jibril na kumfundisha Mtume.
(vi) Kabla ya kuzaliwa Mtume wa mwisho hali ya maadili ya jamii yake ilikuwa sio ya kutamanika. Ni tabia zipi kwa sasa zinaweza kutumika kuelezea hali hizo?
  1. Uunganishaji wa nywele, zinaa na usagaji
  2. Uvaaji mbaya, viduku na zinaa 
  3. Uvutaji wa sigara, ulevi na ukabaji 
  4. Kurithiwa wanawake, zinaa na usagaji 
  5. Kukithiri kwa kamari, ulevi na uzinifu

(vii) Ukiwa unaongoza swala ya maiti unatakiwa ufanye nini baada ya kumswalia Mtume Muhammad (S.A.W)?

  1. Kuleta takbira ya pili 
  2. Kuleta Takibira ya tatu 
  3. Kumuombea maiti
  4. Kuleta Takbira ya nne
  5. Kutoa salamu.

(viii) Umemkuta rafiki yako ameghadhibika kiasi cha kutaka kumdhuru aliyemghadhibisha. Utamsihi afanye nini ili aondokane na hali hiyo?

  1. Kumlani Sheitwani
  2. Kumtukuza Allah (S.W)
  3. Kumswalia Mtume (S.A.W)
  4. Kusoma Ikhlas
  5. Kusoma An Naas.

(ix) Ikiwa umemkuta mtu anayejuta kwa kuua bila ya kukusudia utamshauri afanye nini kwa mujibu wa Uislamu?

  1. Afunge siku hamsini na tisa au sitini
  2. Afunge siku sitini kwa hali yoyote
  3. Afunge miezi miwili mfululizo
  4. Afunge miezi miwili kwa hali yoyote
  5. Afunge siku sitini mfululizo.

(x) Wakati gani Ijtihad inatumika kama msingi wa sheria ya Kiislamu?

  1. Wanachuoni wanapotofautiana katika Qur’an na Sunnah
  2. Wanapokosekana wanachuoni walio wajuzi wa Qur’an na Sunnah
  3. Wanachuoni wanaposhindwa kutumia Qur’an na Sunnah katika hukumu
  4. Jambo linapokosa hukumu kabisa ndani ya Qur’an na Sunnah
  5. Jambo linapokosa hukumu ya wazi ndani ya Qur’an na Sunnah.
  1. Oanisha matendo ya Hijjah yaliyo katika Orodha A na nyakati au maeneo panapofanyika matendo hayo yaliyo katika Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihi sambamba na namba ya kirumi ya swali katika karatasi ya kujibia.

ORODHA A 

ORODHA B 

  1. Mahujaji husimama kuleta dhikri na kuomba dua mchana kutwa.
  2. Mahujaji hutia nia ya Hijjah na kuvaa Ihram
  3. Mahujaji hutembea au hukimbia katika kufanya ibada ya Sa’i
  4. Mahujaji huchinja, hunyoa na kufanya tawaf ya nguzo
  5. Mahujaji huzunguka Ka’aba wakiwa wamefunika bega la kushoto na kuacha wazi la kulia
  6. Mahujaji hufanya ibada ya kulenga mawe minara yote mitatu
  1. Mwezi 10 – Dhul-Hijjah
  2. Muzdalifah
  3. Mara waingiapo tu Makkah
  4. Miiqat
  5. Siku za Tar-wiyah
  6. Mwezi 9-Dhul Hijjah
  7. Siku za Tashriq
  8. Saffa na Mar-wa

SEHEMU B (Alama 54)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

3. Katika kongamano la wazazi Sheikh Mundele alitakiwa kuwasilisha mada ya malezi ya Watoto kimaadili. Bainisha dondoo tatu atakazoweza kuzitumia Sheikh huyu katika kufikisha mada yake hii.

4. Uislamu baada ya kuenea na kuongoza sehemu mbali mbali, ilikuwa ndio mwanzo wa kukomesha biashara ya utumwa na kumkomboa mwanaadamu kiutu, (kiroho), kifikra na kisaikolojia. Thibitisha kauli hii kwa kutumia hoja sita.

5. Maisha ya furaha na amani ya kweli hupatikana kwa kusimama misingi ya haki na Uadilifu katika jamii. Bainisha misingi hiyo kwa kutumia hoja tatu.

6. ‘Kwa hakika Kitabu cha Qur’an hakikaribiwi na batili mbele yake wala nyuma yake.’Kwa mujibu wa kauli hii, toa tofauti tatu kati ya Qur’an na Vitabu vilivyotangulia.

7. “Kwa hakika shirki ni dhulma kubwa” Qur’an (31:13). Kutokana na aya hii, onesha kina cha uovu wa shirki kwa mwenye kushirikisha.

8. Suala la kuamini kuwepo Mwenyezi Mungu si la ububusa na kufuata mkumbo, bali linahitaji ushahidi na dalili. Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu kuu sita.

SEHEMU C (Alama 30)

Jibu maswali mawili tu katika sehemu hii

9. Utafiti uliofanyika katika maeneo mbalimbali umebaini kuwa wapo Waislamu wanaoswali lakini bado wanashiriki katika kufanya maovu mbalimbali. Wewe kama mtaalamu wa Elimu ya Dini ya Kiislamu bainisha sababu tano zinazoweza kupelekea hali hii ili watu wachukue tahadhari na kuiepuka.

10. Katika hukumu za Kiislamu baada ya Qur’an kigezo kinachofuata ni Hadith sahihi za Mtume Muhammad (S.A.W). Wabainishie watu wa Msikitini kwako sifa tano zinazoitofautisha na aina nyingine za kigezo cha usahihi ili watu waweze kufanyia kazi mafundisho yaliyo sahihi tu.

11. Eleza kwa hoja tano kwanini Khalifa Uthman bin Affan (r.a) alinakili upya Quran kutoka kwenye Msahafu wa Mtume(s.a.w) baada ya kufariki kwake.

FORM THREE EDK EXAM SERIES 276  

FORM THREE EDK EXAM SERIES 276  

OFISI YA WAZIRI MKUU-TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA MUHULA KIDATO CHA TATU 

ELIMU YA DINI YA KIISLAMU

MUDA: SAA3:00 MEI 2026

SEHEMU A (ALAMA 20) 

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1.Chagua herufi ya jibu sahihi kisha andika katika kisanduku (i)sanda ya watoto wadogo wakike na wakiume ambao hawajafikia baleghe ina majamvi mangapi? ni 

  1. Matano. 
  2. Matatu 
  3. Manne
  4. Mawili

(ii)Uislamu ndio dini ya pekee inayostahiki kuchaguliwa na kufuatwa kama mwongozo sahihi wa maisha na watu kwa sababu?

  1. Uislamu ndio dini yenye ujuzi unaomwezesha mwanadamu kutenda inavyotakikana.
  2. Uislamu ndio dini yenye ibada nzuri
  3. Uislamu unaeleza ukweli juu ya maumbile na nafasi ya mwanadamu hapa duniani
  4. Uislamu ni dini nyepesi.

(iii)Zifuatazo ni aina za shirki isipokuwa.

  1. shirki fiy dhaat
  2. shirk fiy sifaat
  3. shirki fiy rubbubiya
  4. shirki fiy Ah kaam

(iv)mojawapo ya kazi za malaika ni ......

  1. kuwasaidia waumini katika vita vya kupambana na maadui wa Allah ,(s.w). 
  2. kuwasaidia waumini kufanya ibada mbalimbali.
  3. kuuandamiza usiku na mchana.
  4. kuwasaidia waumini kuwa na maisha mazuri

(v)Zaburi ni kitabu alichoteremshiwa nabii......

  1. Musa (a.s). 
  2. Issa (a.s) 
  3. Ibrahim (a.s). 
  4. Daud (a.s). 

(vi)mambo anayo fanyiwa mtu mara baada kufa ni..........

  1. kumlaza ubavu wa kulia na kumwelekeza kibla
  2. kumwogesha,kumpigisha mswaki na kumpaka manukato.
  3. kulainisha viungo kwa kukunja na kukunjua
  4. kutamka Laila ha ilalah bila kumuashiria na yeye atamke.

(vii)Mtu aliyeelimika anatofautiana vipi na yule ambaye hajaelimika?.

  1. Hatua za kielimu alizofikia
  2. wingi wa tafiti alizofanya
  3. Idadi ya miaka aliyotumia vyuoni
  4. Ufanisi katika utendaji wake.

(viii)Kwa mujibu wa uislamu ,kwanini haiwezekani mtu kuishi bila kuwa na dini?.

  1. Sisi sote ni viumbe mwenyezimungu
  2. Dini ni utaratibu wa maisha ya mwanadamu
  3. Dini ni imani ya kuwepo mola muumba
  4. Mila inayofuatwa na watu katika jamii

(ix).Njia ipi inakamilisha kupatikana kwa jitihaad kama msingi wa sheria za kiislamu.

  1. Qiyas +ijimaa + tafsir ya wanazuoni 
  2. Qur'an + sunna + tafsir za wanazuoni 
  3. sunna + Qiyas + tafsir za wanazuoni. 
  4. Qur'an + Qiyas + tafsir za wanazuoni

(x) Ni yapi makusudio ya kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhan?

  1. kuwawezesha watu wote kuonja ladha ya njaa.
  2. Kujifunnza kuchunga mipaka ya Allah (s.w).
  3. Kuweza kufanana na umma zilizopita.
  4. Kuweza kufutiwa dhambi zetu.

2.Oanisha sentensi katika orodha A na maneno katika orodha B kisha jaza herufi yake katika karatasi ya kujibia.

Orodha A.  Orodha B

(i)kutembea baina ya vilima viwili vya saffa na marwa mara saba.

(ii)Kuwatii kwa kufuata maamurisho yao na kuacha makatazo yao na kuacha makatazo yao katika kila kipengele cha maisha ya kibinafsi na kijamii.

(iii).Shafii ,Abuhanifa ,Ahmed bin Hambal na Malik.

(iv).Wala siabudu mnachokiabudu ,wala nyinyi hamuabudu ninaye mwabudu . (v).Kuzunguka kaa'ba mara saba.

(vi).Huyu ni yule ambaye ananyanyasa yatima ,wala hajihimizi yeye wala wengine katika kuwalisha masikini.

  1. kuamini mitume 
  2. kaafirun 
  3. tawafu. 
  4. Quraish 
  5. Kusai 
  6. kuamini malaika 
  7. Maa'un 
  8. Maimam wanne waongofu 
  9. Makhalifa wanne wa mtume (s.a.w).

SEHEMU B. (Alama 64). 

jibu maswali yote katika sehemu hii

3.(a)Tofautisha elimu yenye manufaa na elimu isiyo na manufaa.

(b)kwanini uisilamu umeipa elimu nafasi ya kwanza? toa hoja tatu

4.Kwanini uislamu ndio dini pekee inayostahiki kuchaguliwa na kufuatwa kama mwongozo sahihi wa maisha. toa hoja tano

5.Mwanadamu pamoja na ujuzi alionao hawezi kujiundia mfumo (dini)sahihi wa maisha .Thibitisha kauli hii kwa hoja tano.

6.Ainisha matunda yatakayopatikana kwa uislamu kusimama na kuongoza maisha jamii. toa hoja nne tu. 

7.Bainisha dalili tano zinazothibitisha uwepo wa Allah (s.w) pasina shaka yeyote. 

8. (a).Taja sifa tano za malaika wa Allah(s.w).

(b).Bainisha kazi tatu za malaika wa Allah (s.w).

SEHEMU C (ALAMA 20) 

Jibu maswali yote katika sehemu hii

9."Mungu hayupo kwasababu milango ya fahamu haitambui " hii ni kauli ya Charles Darwin na wenzake juu ya kupinga uwepo wa mungu muumba.Onyesha madai yao na madhaifu ya kila dai.

10. Suala la kuamini kuwepo Allah (s.w) si la kibubusa na kufuata mkumbo bali linahitaji ushahidi na dalili za kielimu .Thibitisha kauli hii kwa kutoa sababu kuu tano.

FORM THREE EDK EXAM SERIES 275  

FORM THREE EDK EXAM SERIES 275  

JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA RAIS TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA 

MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA WA PILI

ELIMU YA DINI YA KIISLAMU

KIDATO CHA TATU 

MUDA: SAA 2:30 NOVEMBER 2025

Maelekezo:

  1. Mtihani huu Una sehemu A, B na C
  2. Jibu maswali yote kutoka sehemu zote.
  3. Udanganyifu wa Aina yeyote ni haramu.
  4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na kila swali.
  5. Andika jina lako kamili katika kila ukurasa wa karatasi yako ya majibu. 

SEHEMU A (Alama 16) 

Jibu maswali yote.

1. Katika kipengele i -x chagua jibu sahihi kisha andika herufi ya jibu lako katika kijitabu chako cha kujibia.

SEHEMU A

1.(i) Ni upi mtazamo wa Uislamu juu ya maada ya ‘ibada’?

  1. Ni kufuata amri za Allah zote kwa kuchunga mipaka yake katika maisha ya kila siku
  2. kipengele cha maisha yake ya kila siku kibinafsi na kijamii.
  3. ina maaana ya utumwa
  4. ina maaana ya unyenyekevu 

(ii) Nini maana ya Dini. 

  1. Ni njia ya maisha
  2. Ni mzunguko wa maisha
  3. Ni utaratibu wa wanadamu
  4. Ni mfumo wa maisha ya mwanadamu

(iii) Nini maana ya shirki. 

  1. kulinganish
  2. kufananisha
  3. Shirk ni kinyume cha Upweke au Umoja (Tawhiid)
  4. Ni dhulma kubwa kuliko zote.

(iv) Ni ipi maana halisi ya kumuamini Mwenyezi Mungu (s.w) katika maisha ya kila siku? 

  1. kusali sana na kufunga.
  2. Ni kufuata amri za Allah zote kwa kuchunga mipaka yake katika maisha ya kila siku. 
  3. kutoa zaka ya mali
  4. kwenda kuhiji kwa mwenye uwezo

(v) Matendo ya ibada ya Hijjah.

  1. Twawafu na kusai
  2. kusai na kusoma Qur an
  3. Twawafu na kusali sunnah
  4. kuzuru makkah

(vi) Bainisha nafasi ya Zakat katika Uislamu. 

  1. Ni amri ya Allah
  2. Ni nguzo ya imani
  3. Ni nguzo ya ihsani
  4. ni nguzo ya swala

(vii) Eleza maana ya swaumu kisheria 

  1. Ni amri ya Allah.
  2. ni nguzo ya imani
  3. kujizuia kula na kunywa
  4. kujizuia na kazi

(viii) Wengi wafungao mwezi wa Ramadhan hawafikii malengo ya funga zao. Sababu ya ni ? 

  1. kuto futuru mapema
  2. kuto Sali tarawehe
  3. kuto kula daku
  4. kuto zingatia masharti ya swala

(ix) Miongoni mwa haki katika Uislamu ni. 

  1. Haki za kitaifa
  2. Haki za Viumbe na Mazingira.
  3. Haki za kustarehe
  4. Haki za kutembea

(x) Hii ni haki kisheria ili kuwa mwanafamilia halali.

  1. haki ya nasaba
  2. Haki ya kuishi
  3. Haki ya kujenga
  4. Haki ya urafiki


i

ii

iii

iv

v

vi

vii

viii

ix

x











2. Oanisha kifungu cha maneno kilichopo kutoka ORODHA "A" na kile kinachowiana kutoka ORODHA "B" kisha andika herufi ya jibu lako katika kijitabu chako cha kujibia.

ORODHA A

ORODHA B

  1. Malaika mkuu anaye mhusika na kupeleka wahyi
  2. Kumchunga na Kumlinda kila mtu na kuandika amali zake nzuri na mbaya.
  3. Kutoa roho za viumbe.
  4. Kuzihoji, kuzistarehesha au kuziadhibu roho za wafu kaburini.
  5. Kupuliza Parapanda siku ya Qiyama. 
  6. Kuwaliwaza na kuwakaribisha watu wema peponi.
  1. Mikail
  2. Ridhwani
  3. Israfil
  4. Munkar na Nakir
  5. Malakul Mauti
  6. Raqibu na atidi
  7. Jibril


i

ii

iii

iv

v

vi







SEHEMU B

3. Dhihirisha matunda ya kusimamisha ibada ya swala kikamilifu.

4. . Kwa kutumia ushahidi wa Hadith, onesha hatua tatu za kuondosha uovu katika mazingira ya jamii yako.

5. Orodhesha itikadi ya makundi ya dini za wanaadamu zifuatazo; 

  1. Ukafiri 
  2. Ushirikina 
  3. Utawa

6. Kutokana na ushahidi wa kihistoria, eleza uwepo wa ufufuo baada ya kufa.

7. Ni lipi lengo la kuletwa Mitume na Manabii?

8. Ainisha mafunzo matano yatokanayo na mkataba wa Hudaibiyah kwa muhtasari.

 SEHEMU C

9. Eleza hatua alizochukua Mtume (s.a.w) katika kuihifadhi na kuilinda Qur’an.

10. Mwanaadamu pamoja na ujuzi alionao, hawezi kujiundia mfumo sahihi wa maisha. Thibitisha kauli hii kwa hoja tano tu.

11. Mtume (s.a.w) alitumia njia za ulinzi, usalama na diplomasia katika kuilinda serikali ya Kiislamu Madinah. Fafanua kauli hii.

FORM THREE EDK EXAM SERIES 253  

FORM THREE EDK EXAM SERIES 253  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256