JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
MTIHANI WA NUSU MUHULA
KIDATO CHA KWANZA
021 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU
Muda Saa: 2:30 Septemba, 2026
Maelekezo
SEHEMU A (ALAMA 15)
Jibu maswali yote katika sehemu hii
1. Chagua jawabu sahihi kisha Andika herufi ya jawabu katika kitabu chako cha kujibia
(i) Kwa mujibu wa uislamu, mtu aliye elimika anajitofautisha na wasioelimika kwa sifa hii
(ii) Hutokea iwapo Nun-sakinah na Tanwiin zitakuja kabla ya herufi sita za idh-haar
(iii) Katika uislamu kufuata sunnah ni utekelezaji wa shahada ya pili . Ni ipi kati ya zifuatazo ni dhana sahihi kuhusu sunnah?
(iv) Jambo gani ni lazima kutekeleza katika mchakato wa kumuosha maiti
(v) Wahyi wa kwanza kumshukia Mtume (S.A.W) ulisisitiza juu ya jambo gani
(vi) Bwana Bakari anajizuia na vyakula vizuri, anavaa nguo chakavu na kuishi katika nyumba isiyo na sakafu, akiamini kuwa kufanya hivyo ni kujikurubisha zaidi kwa Mungu . Bwana Bakari atakuwa ameathiriwa na mfumo gaani wa maisha?
(vii) Mwanaadamu analazimika kuisoma Qur’an kwa kuzingatia lengo kuu. Ni lipi lengo la kitabu hicho ?
(viii) Ni nguzo ya tano miongoni mwa nguzo za Uislamu ambayo hufanywa katika miezi maalum kwa mwenye uwezo
(ix) Sentensi ipi inabainisha njia zilizotumika kuhifadhi Qur’an wakati wa Mtume (S.A.W)
(x) Hadithi ndio njia kuu inayotumika kuhifadhi sunnah ya Mtume (S.A.W) Katika zama hizi. Ni ipi kati ya dhana zifuatazo ni sahihi kuhusu hadithi
MAJIBU
| i | ii | iii | iv | v | vi | vii | viii | ix | x |
| . |
2. Oanisha nyakati mahsusi za swala kulingana na mwenendo wa jua katika orodha A na majina ya swala zinazotekelezwa katika nyakati hizo katika orodha B kisha Andika herufi ya jawabu sahihi kwa kila kipengele.
| ORODHA | ORODHA B |
|
|
MAJIBU
| ORODHA A | i | ii | iii | iv | v |
| ORODHA B |
SEHEMU B (Alama 70)
Jibu maswali yote katika sehemu hii
3. Aya zifuatazo za suratul-Ikhlasw (112:1-4) zimechanganywa . Pangilia kwa usahihi kama ilivyoshuka katika Qur’an.
4.a) Allah anasema “Na anayetaka dini nyengine isiyokuwa Uislamu basi haitokubaliwa kwake. Naye akhera atakuwa katika wenye khasara” Qur’an (al-Imran :85). Aya hii inaonyesha dini zilizobuniwa na watu. Bainisha dini hizo
b) Elezea hatua za kushuka Qur’an
5. a) Eleza kwa kutoa hoja mbili(02) kwa nini ni muhimu kufauta sunnah ya Mtume (S.A.W) katika maisha ya kila siku
b) wewe kama mtaalamu wa sunnah na hadithi elezea tofauti tatu(03) zilizopo baina ya sunnah na hadithi
6.a) Suratul-faatihah imepewa majina mbalimbali kutokana na maudhui yanayopatikana ndani yake. Bainisha Majina Matano ya suratul-faatiha
b) Wanafunzi wengi wanaosoma elimu ya dini ya kiislamu hawaelewi uhusiano uliopo baina ya elimu ya dini ya kiislamu na masomo mengine. Wewe kama mtaalamu wa kidato cha kwanza wawafafanulie uhusiano uliopo kwa hoja tatu
c) Elezea sababu mbili zinazoruhusiwa na uislamu kwa mtu kutayammamu
7.a) Mtume (S.A.W) ametufahamisha kuwa uislamu umejengwa juu ya nguzo tano . Fafanua nguzo hizo kwa mpangilio.
b) Wakati ukiwa shule mzazi wako alipaiga simu kwa Mwalimu wako na kumtaarifu kuwa Jirani yenu amafarki na hakuna mwenye elimu ya kuosha maiti isipokuwa wewe mtaani kwenu, mama akaomba ruhusa ya wewe Kwenda kuosha maiti. Elezea hatua kwa hatua namna utakavyomuosha maiti huyo.
8.a) Bainisha makundi ya najisi na mifano yake
b) Bainisha namna ya kujitwaharisha kwa kila kindi
c) Elezea maana ya hedhi, nifasi na janaba
9. a) Shirki imegawanyika katika makundi mawaili. Bainisha makundi hayo
b) Mtu anae mshirikisha Allah (S.W) atajidhihirisha maeneo matatu. Fafanua maeneo hayo
SEHEMU C (ALAMA 15)
Jibu swali la kumi (10)
10. Juma hatekelezi ibada ya swala kwa sababu anasumbuliwa na maradhi mbalimbali. Kama mwanafunzi wa kidato cha kwanza, toa elimu kwa Juma namna gani mgonjwa anaweza kutekeleza swala za faradhi.
FORM ONE EDK EXAM SERIES 284
FORM ONE EDK EXAM SERIES 284