FORM FOUR ELIMU YA DINI YA KIISLAMU EXAMS SERIES

OFISI YA WAZIRI MKUU TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA ROBO MUHULA WA PILI KIDATO CHA NNE

015 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU

(Kwa watahiniwa walioko na wasiokuwa shuleni)

Muda: Saa 3 — SEPTEMBA 2026

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na moja (11).
  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali mawili (2) kutoka sehemu C.
  3. Sehemu A ina alama kumi na sita (16), sehemu B ina alama hamsini na nne (54) na sehemu C ina alama thelasini (30).
  4. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihiani.
  5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

SEHEMU A (Alama 16)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua jibu sahihi katika kipengele cha (i) – (x) kisha andika herufi yake katika kijitabu chako cha kujibia.

(i) Mtu aliyeelimika anatofautiana vipi na yule ambaye hajaelimika?

A. Hatua za kielimu alizofikia
B. Wingi wa tafiti alizozifanya
C. Uzoefu wa mambo aliyokuwa nao
D. Ufanisi katika utendaji wake
E. Uwezo wa kujenga hoja na kuchambua.

(ii) Ni kwa namna gani wanadamu wanahisi uwepo wa Allah (S.W) katika maisha yao?

A. Kwa kuwa na akili ya kutatua haja zao
B. Kwa kukutana na changamoto mbalimbali
C. Kwa kukosa kupata majibu kuhusu asili yao
D. Kwa kifikiria kuumbwa kwake na mwisho wake
E. Kwa kuibuka watu wanaotoa habari za Allah (S.W).

(iii) Kwa mujibu wa Uislamu, kwanini haiwezekani mtu kuishi bila ya kuwa na dini?

A. Sote ni viumbe wa Allah (S.W)
B. Dini ni utaratibu wa maisha.
C. Watu wote wanazaliwa na Dini
D. Dini ilifundishwa na Mitume
E. Dini ni Imani ya Mungu muumba.

(iv) Njia ipi inakamilisha kupatikana kwa Ijtihadi kama msingi wa sharia za Uislamu?

A. Qiyas+Ijmaa+ Tafsiri ya wanazuoni
B. Qur’an+ Sunnah +Tafsiri ya wanazuoni
C. Sunnah+ Tafsiri ya wanazuoni+ Qiyas
D. Tafsiri ya wanazuoni+ Qur’an+ Qiyas
E. Sunnah+ Rai+ Tafsiri ya wanazuoni.

(v) Ni lipi lengo kuu la kuamrishwa kusimamisha nguzo tano za Uislamu?

A. Kujua baina ya wakweli na wanafiki
B. Kupata thawabu na Pepo ya Allah (S.W)
C. Kumuabudu Allah katika maisha yote
D. Kuwafanya waislamu kuwa imara kiimani
E. Kuimarisha uhusiano wetu na Malaika.

(vi) Muandaaji wa sanda ya mtoto anapaswa kuzingatia jambo gani kati ya haya?

A. Jinsi ya mtoto aliyefariki
B. Kuwa na vipande vitatu
C. wepesi na aina ya kitambaa
D. Kuwa na vipande vitano
E. Masharti na nguzo za kuoga.

(vii) Nuun Sakna au Tan wiin inapokutana na Yaaun inapatikana hukumu gani?

A. Iq-lab
B. Idh-har
C. Id-gham
D. Ish-mam
E. Ikh-fau

(viii) Bwana Mikebe anamiliki dhahabu gramu 150 iliyokidhi vigezo vyote vya kutolewa Zakat. Gramu ngapi za dhahabu anapaswa kutoa kama Zakat?

A. 3.75
B. 1.5
C. 2.25
D. 2.5
E. 3.0

(ix) Ni yapi makusudio ya kufunga mwezi mtukufu wa Ramadhani?

A. Kuwezesha watu wote kuonja ladha ya njaa
B. Kuwezesha kufanana na umma uliopita
C. Kuadhimisha kushuka kwa Qur’an
D. Kujifunza kuchunga mipaka ya Allah (S.W)
E. Ili waweze kuwa wachamungu.

(x) Bani israil ni kizazi cha nabii yupi?

A. Is-haqa
B. Yusuf
C. Musa
D. Daud
E. Yaquub

2. Oanisha sifa za swala za Sunnah zilizo katika Orodha A na swala za Sunnah husika zilizo katika Orodha B. kisha jaza herufi yake katika kijitabu cha kujibia.

ORODHA A
ORODHA B
  1.  Ina Sunnah ya kugeuza nguo wakati waku iswali.
  2.  Ina rakaa mbili visimamo vinne, rukuu nne na khutba baada ya swala.
  3.  Ina rakaa mbili, takbira kumi na mbili, rukuu mbili, huswaliwa baada ya kuchomoza kwa jua na kupanda kidogo na khutba baada ya swala.
  4.  Ina rakaa mbili, rukuu mbili huswaliwa wakati wowote wa halali na dua baada ya swala.
  5.  Ina rakaa kuanzia mbili, rukuu mbili, sijda mbili na hamna dua baada ya swala.
  6. Ina rakaa mbili na inaswaliwa wakati wowote baada ya Ishaa na kabla ya Alfajir.
A. Swalatu dhuhaa
B. Swalatul Kusuf
C. Swalatul Haajah
D. Walaatul Witr
E. Swalatul-Istisqaa
F. Swalatul Tawbah
G. Swalatul Idd
H. Swalatul Istikharah

SEHEMU B (Alama 54)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

3. Uislamu ulileta mageuzi makubwa kuhusu utumwa ukizingatia hali ilivyokuwa mbaya kabla ya Mtume Muhammad (SAW). Ukiwa kama mwanahistoria ya dini ya Kiislamu, thibitisha Kwa hoja sita namna hali ilivyokuwa kipindi hicho kabla ya mjumbe wa Allah (S.W) kuletwa kufanya ukombozi.

4. Baada ya kusikia watu wakisema kuwa Uislamu haumthamini mwanamke, Zainabu alimuuliza mwalimu wake ili kutaka kufahamu kama kweli mwanamke hathaminiwi katika Uislamu. Kama mwanafunzi wa dini ya Kiislamu, eleza hoja sita alizopewa Zainab na mwalimu wake.

5. Baada ya Mtume Muhammad (S.A.W) kufariki, makundi mbalimbali ya harakati yaliibuka kuhuisha Uislamu. Kwa kutumia makundi yaliyoanzishwa mnamo Karne ya 20 A.D, chambua mafunzo matatu ambayo Waislamu wa zama za sasa wanapaswa kuishi nayo.

6. Baadhi ya watu katika jamii wanadai kwamba mkataba wa Hudaybiya haukuwanufaisha Waislamu. Kosoa madai ya watu hao kwa kutumia hoja sita.

7. Wanafunzi wa kidato cha nne wanajadili uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba 2025 nchini Tanzania. Mwalimu wao anawaelekeza kutazama uchaguzi huo kwa jicho la Kiislamu, kwa kuzingatia sifa za viongozi wanaofaa kuchaguliwa ili kuongoza kwa haki na uadilifu. Eleza sifa sita za kuzingatia katika kuwachagua watu hao.

8. Wanafunzi wa kidato cha nne wanajadili sababu zinazomfanya Muislamu ajiepushe na shirki. Mwalimu anasisitiza umuhimu wa kuelewa dhana ya shirk na aina zake ili kuimarisha Tauhidi. Fafanua aina tatu za dhana hiyo.

SEHEMU C (Alama 30)

Jibu maswali mawili (2) tu katika sehemu hii.

9. Baada ya kusoma Suratul Asr, Zuberi alijiuliza: “Je, sura hii fupi ina ujumbe gani mkubwa kwa Waislamu? Tumia nukta nne kumueleza mafunzo yanayopatikana katika Suratul hiyo.

10. Katika kikao cha vijana wa Kiislamu, mmoja wao alidai kwamba kwa kuwa kuna kitabu cha Qur’ani hakuna ulazima wa kufuata mwenendo wa Mtume Muhammad (S.A.W) katika maisha ya kila siku. Kwa kutumia hoja nne, kosoa dai hilo kwa kuonesha umuhimu wa kufuata mwenendo huo katika maisha ya Muislamu.

11. Katika hotuba ya Swala ya Ijumaa, khatibu aliwasisitiza Waislamu kuwa funga si tu ni ibada ya kujizuia kula na kunywa, bali pia ni njia ya kukuza ucha- Mungu na maadili ya jamii. Kwa kutumia hoja nne, fafanua namna ibada hiyo inavyosaidia kukuza ucha-Mungu na maadili ya jamii.

FORM FOUR EDK EXAM SERIES 265  

FORM FOUR EDK EXAM SERIES 265  

OFISI YA WAZIRI MKUU, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MTIHANI WA NUSU MUHULA - KIDATO CHA NNE 

015 ELIMU YA DINI YA KIISLAMU 

(Kwa watahiniwa walioko na wasiokuwa shuleni)

Maelekezo

  1. Kratasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na moja (11).
  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali mawili (2) kutoka sehemu C.
  3. Sehemu A ina alama kumi na sita (16), sehemu B alama hamsini na nne (54) na sehemu C ina alama thelathini (30).
  4. Zingatia maelekezo ya kila sehemu na ya kila swali.
  5. Majibu yote yaandikwe kwa kalamu yenye wino wa bluu au mweusi.
  6. Vifaa vya mawasiliano na vitu visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.
  7. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa karatasi zako za kujibia.

SEHEMU A (Alama 16)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Katika kipengele (i) – (x), chagua jibu sahihi kisha andika herufi yake katika kijitabu chako cha kujibia.

i) Kwanini Waislamu wa leo wanapaswa kuipa elimu kipaumbele?

  1. Wapate kuitumia kutafuta riziki ya halali
  2. Ndio nyenzo kuu ya kuwa khalifa wa kweli
  3. Waweze kushiriki kwenye mambo ya kielimu
  4. Wawe wengi katika nafasi za kazi serikalini
  5. Kuleta ushindani na wawe wasio waislamu

ii) Umeombwa kuwaelezea wanafunzi wenzio kuhusu historia ya madhehebu ya Ki-Fiqh. Utachagua yapi kati ya haya kutekeleza jambo hilo?

  1. Ahlus Sunnah Wal Jamaa 
  2. Shia, Ibadh na Sunni 
  3. Hanbaliyah na Hanafiyah
  4. Salafus Swaleh na Bakwata
  5. Ahmadiyah na Ismailiyah

iii) Kosa gani walilofanya watu wa Madyan tu ambalo hadi sasa linafanywa?

  1. Kupunguza vipimo 
  2. Kufanya ufisadi 
  3. Uharamia njiani
  4. Uzinifu na ufuska 
  5. Kiburi na majivuno

iv) Mwalimu amekusimamisha useme ulichojifunza kutokana na maandalizi ya kimafunzo ya Mtume wa mwisho. Utasema lipi kati ya haya yafuatayo?

  1. Umuhimu wa Hadith za Mtume 
  2. Umuhimu wa historia 
  3. Nafasi ya dua katika Da’wa
  4. Ukombozi wa fikra kwa vijana
  5. Nafasi ya swala za Usiku

v) Bwana Mbundu ni mwanasayansi anayetaka kuanzisha mfumo wa maisha utakaowasaidia watu wote kuishi kwa raha kwa kutumia ujuzi wake, lakini akaambiwa hawezi kufanya hivyo. Kwanini bwana huyu asiweze?

  1. Kuna tafiti za kisayansi hajazikamilisha
  2. Nyenzo atakazozitumia haziwezi kumsaidia
  3. Hawezi kukubaliwa na wanasayansi wengine
  4. Anahitaji ujuzi mwingine baada ya huu alionao
  5. Anahitaji kushirikiana na wenzake na si peke yake

vi) Kwa ujumla kanuni zinazotumika kuweka sheria za Kiislamu hujulikana kwa jina gani?

  1. Usuul Thalathah 
  2. Usuul Hadith 
  3. Usuul Sunnah
  4. Usuul Fiqh 
  5. Usuul Ibada

vii) Bwana Ngugu ametokewa na jambo fulani mchana wa Ramadhani lakini

akaambiwa funga yake haijaharibika. Bwana huyu ametokewa na nini?

  1. Kutia nia ya kula tu
  2. Kunyweshwa dawa 
  3. Kutokwa na manii
  4. Kutapishwa na daktari 
  5. Kutia nia ya kunywa tu.

viii) Muandaaji wa sanda ya mtoto wa kike anapaswa kuzingatia jambo gani kati ya haya?

  1. Jinsia ya mtoto aliyefariki
  2. Kuwa na vipande vitano
  3. wepesi na aina ya kitambaa
  4. Kuwa na vipande vitatu
  5. Masharti na nguzo za sanda

(ix) imageNuun Sakna ) ((Ù† au (Tan wiin) inapokutana na Qaaf yenye fat-ha inapatikana hukumu gani?

  1. Iq-lab 
  2. Idh-har 
  3. Id-gham 
  4. Ish-mam 
  5. Ikh-fau

x) Bwana Ng’ombo anamiliki mbuzi na mbuzi 40. Baada ya kupinduka mwaka nini anapaswa kutoa kama Zakat katika hiki alichonacho?

  1. Mbuzi mmoja 
  2. Kondoo na mbuzi watatu 
  3. Kondoo mmoja wa miaka miwili
  4. Ndama mmoja
  5. Kondoo na mbuzi mmoja.

2. Oanisha maelezo ya shahada yaliyo katika Oradha A na aina za shahada zilizo katika Orodha B kisha andika herufi ya jibu sahihih katika kijitabu chako cha kujibia.

ORODHA A

ORODHA B

  1. Kuishi kwa kufuata Qur’an na Sunnah.
  2. Kitambulisho cha Muislamu aliye sahihi.
  3. Hudhihirisha ualimu wa Mtume wa mwisho.
  4. Hupatikana kwa aliye na mapenzi ya dhati ya Allah na Mtume wake.
  5. Kuishi kwa kumtii Allah daima.
  6. Hupatikana faida ya kujua walioongezeka katika Dini ya Allah.
  1. Shahada ya moyoni
  2. Shahada ya matamshi
  3. Shahada ya kwanza
  4. Shahada ya kusilimu
  5. Shahada mbili
  6. Shahada ya ahadi
  7. Shahada ya matendo
  8. Shahada ya pili

SEHEMU B (ALAMA 54)

Jibu maswali yote katika sehemu hii

Jibu maswali yote katika sehemu hii. Andika majibu yako kwa ufupi na ufasaha.

3. Wewe kama Muislamu unapaswa kuvifanyia nini viungo vyako vifuatavyo? 

  1. a) Kiwiliwili
  2. b) Mdomo na ulimi
  3. c) Mikono na miguu

4. Tumia hoja tatu kuwafafanulia wanajamii wa mtaani kwako ni kwa namna gani mahari inaweza kushusha hadhi ya mwanamke?

5. Umekutana na vijana watatu wanaotetea sheria zilizotungwa kwenye mabunge mbalimbali kuwa hazina kasoro.

  1. a) Waeleweshe vijana hawa chimbuko la sheria wanazozitetea.
  2. b) Tumia hoja nne kukosoa msimamo wao huu.

6. Wayahudi walifanya jitihada kubwa ya kuuzima Uislamu Madinah kwa kufanya vitimbi mbalimbali dhidi ya Dola na Waislamu. Wewe kama khatibu wa Ijumaa wafahamishe Waumini wa msikitini hapo mambo sita hayo ili waweze kuchukua tahadhari na wanaofanana na hao.

7. Umekaribishwa katika mjadala wa wasioamini siku ya mwisho kwa kutoa hoja zao mbalimbali. Wathibitishie ulazima wa kuwepo siku hiyo kwa kuwabainishia hoja tatu ili waondokane na fikra yao hiyo potofu.

8. Katika jamii ya Waislamu wapo watu wasiokubali ukhalifa wa Khalifa wa kwanza kwa kutokana na mitazamo tofauti juu ya uchaguzi wake. Tumia hoja mbili madhubuti kuwafafanulia waislamu hao mitazamo hiyo ili wasije kuingia kwenye makosa.

SEHEMU C (Alama 30)

Jibu maswali mawili (2) kutoka sehemu hii

9. Miongoni mwa hoja wanazozitumia wasio waislamu katika kuichafua Qur’an ni kudai kuwa ni kitabu cha mashairi ya Mtume Muhammad (Sallallahu Alayhi Wasallam). Toa hoja nne kuwadhihirishia watu hawa kuwa wanachokidai si sahihi.

10. Umealikwa kutoa semina kwa mahujaji watarajiwa juu ya utekelezaji wa ibada ya Hijjah. Waambie namna watakavyoweza kufikia kumpenda Allah kikwelikweli kwa kupitia utekelezaji wa ibada hiyo? (Hoja tano)

11. Mwalimu ameingia darasani kufundisha usahihi wa hadith za Mtume Muhammad (Sallallahu Alayhi Wasallam) kwa kuangalia matini yake. Atatumia hoja gani kuelezea mada hii? (Hoja tano)

FORM FOUR EDK EXAM SERIES 244  

FORM FOUR EDK EXAM SERIES 244  

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256