STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2012

 KISWAHILI-2012

SEHEMU A

SARUFI

Chagua herufiyajibu lililo sahihi kisha andika katika karatasiyakoya kujibia.

1. Katika maneno yafuatayo ni lipi ambalo ni nomino dhahania?

  1. Unakuja
  2. Umeenea
  3. Utalima
  4. Uelewa
  5. Ulisoma
Chagua Jibu


2. Wingi wa neno "paka" ni upi?

  1. Mipaka
  2. Paka
  3. Mapaka
  4. Vipaka
  5. Wapaka
Chagua Jibu


3."Akiondoka Sulubu kazi zote zitalala." Neno "sulubu" ni la aina ipi?

  1.  Kielezi 
  2.  Kivumishi 
  3.  Kiwakilishi 
  4.  Nomino 
  5.  Kiunganishi
Chagua Jibu


4."Ili tuendelee.... ..... kufanya kazi kvva bidii." Neno lipi limekosekana kukamilisha sentensi hiyo?

  1.  ni budi 
  2.  hatuna budi 
  3.  tuna budi 
  4.  kuna budi 
  5.  Hapana budi
Chagua Jibu


5."Mvua ilinyesha jana usiku kucha. " Katika sentensi hiyo kikundi kielezi ni kipi?

  1.  Mvua ilinyesha jana 
  2. Usiku kucha 
  3.  Ilinyesha jana 
  4. Mvua ilinyesha 
  5. Jana usiku kucha
Chagua Jibu


6."Baba alilimiwa shamba." Sentensi hii ipo katika kauli gani?

  1.  Kutenda 
  2. Kutendewa 
  3.  Kutendwa
  4. Kutendeka E. Kutendea
Chagua Jibu


7."Adili alikuwa anaimba tangu ujana wake." Neno "alikuwa" ni aina gani ya kitenzi? 

  1.  Kisaidizi 
  2.  Jina 
  3.  Kishirikishi
  4. Kitegemezi 
  5. Kikuu
Chagua Jibu


8."Mchungaji alivaa suti maridadi sana."Katika sentensi hii neno lipi limetumika kama kivumishi?

  1.  Suti 
  2. Alivaa 
  3.  Maridadi 
  4. Mchungaji 
  5. Sana
Chagua Jibu


9.Kitenzi " anapigwa" kipo katika kauli gani?

  1.  Kutenda 
  2. Kutendewa 
  3. Kutendwa 
  4. Kutendeka 
  5. Kutendesha
Chagua Jibu


10.Kisawe cha neno "bahati" ni kipi kati ya maneno yafuatayo?

  1.  Tunu 
  2. Sudi 
  3.  Shani
  4. Hiba 
  5. Hidaya
Chagua Jibu


11."Maandishi yanasomeka vizuri." Sentensi hii ipo katika wakati gani?

  1.  Ujao 
  2. Uliopita 
  3. Mazoea 
  4. Uliopo 
  5. Timilifu
Chagua Jibu


12. "Makubi ni mtoto wa mjukuu wangu." Makubi ni nani kwangu?

  1.  Kilembwekeza 
  2. Kijukuu 
  3. Kilembwe 
  4. Kitukuu 
  5. Mtukuu
Chagua Jibu


13."Sipendi uongo." Sentensi hii ipo katika nafsi ipi?

  1.  Nafsi ya kwanza wingi 
  2. Nafsi ya tatu umoja 
  3. Nafsi ya kwanza umoja 
  4. Nafsi ya tatu wingi
  5. Nafsi ya pili umoja.
Chagua Jibu


14.Neno "poni" lina maana sawa na neno lipi kati ya maneno?

  1.  Posho 
  2. Rahani 
  3. Mali 
  4. Mkopo 
  5. Pesa
Chagua Jibu


15. "Shuleni kwetu kuna upungufuwa . Ni neno lipi hukamilisha tungo hiyo kwa usahihi?

  1.  thamani 
  2. thamini 
  3. dhamini
  4. zamani 
  5. samani
Chagua Jibu


16. "Mtoto ametengeneza toroli Ia mti." Wingi wa sentensi hii ni upi?

  1.  Watoto wametengeneza toroli za miti
  2.  Watoto wametengeneza matoroli ya mti
  3.  Watoto ametengeneza matoroli ya miti
  4.  Watoto wametengeneza toroli za mti
  5.  Watoto wametengeneza matoroli ya miti
Chagua Jibu


17. "Muda mfupi atakuwa anaingia uwanjani." Sentensi hii ipo katika wakati gani?

  1. Uliopo
  2. Uliopita
  3. Wa mazoea
  4. Ujao
  5. Timilifu
Chagua Jibu


18.

Ni neno lipi kati ya haya yafuatayo halilandani na mengine?

  1. Fikiria
  2. Dodosa
  3. Uliza
  4. Hoji
  5. Saili
Chagua Jibu


19. Juma aliondoka hivi punde. Maneno "hivi punde" yana maana ipi?

  1. Haraka
  2. Muda mrefu
  3. Karibuni
  4. Kwa pupa
  5. Kwa haraka
Chagua Jibu


20. Neno lipi ni kisawe cha neno adili?

  1. Ujinga
  2. Wema
  3. Uovu
  4. Ujasiri
  5. Ukatili
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256