STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2011

KISWAHILI 2011

SEHEMU A

SARUFI

Katika swali la (1 - 20) andika herufi ya jibu sahihi katika karatasi yako ya kujibia.

1. Neno "jenga" likinyumbulishwa katika kauli ya kutendeka litakuwa neno lipi?

  1. Jengwa
  2. Jengea
  3. Jengeka
  4. Jengesha
  5. Jengewa
Chagua Jibu


2. Neno "wamewalisha" linadokeza hali gani ya kitenzi?

  1. Kuendelea
  2. Mazoea
  3. Masharti
  4. Matarajio
  5. Timilisho
Chagua Jibu


3. "Yeye hupenda sana kusoma Kiswahili". Katika sentensi hii ni neno lipi limetumika kama kiwakilishi?

  1. Hupenda
  2. Kiswahili
  3. Sana
  4. Yeye
  5. Kusoma
Chagua Jibu


4. Katika sentensi zifuatazo ni ipi ipo katika hali ya mazoea

  1. Roda alisoma gazeti la Mtanzania.
  2. Roda atasoma gazeti la Mtanzania.
  3. Roda husoma gazeti la Mtanzania.
  4. Roda amesoma gazeti la Mtanzania.
  5. Roda anasoma gazeti la Mtanzania.
Chagua Jibu


3. Sara alimwambia Heri kwamba hakusafiri bali alikuwepo pale pale. Kauli halisi itakuwa ipi?

  1. Sara alimwambia Heri, "Sikusafiri nipo hapa hapa".
  2. Sara alimwambia Heri, "Sitasafiri nipo hapa hapa".
  3. Sara alimwambia Heri, "Sisafirinipo hapa hapa".
  4. Sara alimwambia Heri, "Hajasafiri yupo hapa hapa".
  5. Sara alimwambia Heri, "hakusafiri yupo hapa hapa".
Chagua Jibu


6. "Alikuwa anajibu kihuni". Neno "kihuni" limetumika kama aina gani ya neno?

  1. Kielezi
  2. Kiwakilishi
  3. Kivumishi
  4. Kitenzi
  5. Kihisishi
Chagua Jibu


7. "Mtu anayetaka msaada wa aina nitampa". Neno linalofaa kukamilisha tungo hiyo ni lipi?

  1. wowote
  2. yoyote
  3. yeyote
  4. vyovyote
  5. lolote
Chagua Jibu


8. "Wanafunzi wanaendelea kusoma Kiswahili ingawa hawana mwalimu". Neno "wanaendelea" limetumika kama aina gani ya kitenzi?

  1. Kikuu
  2. Kishirikishi
  3. Jina
  4. Kisaidizi
  5. Kitegemezi
Chagua Jibu


9. Mahali pale panatisha. Neno "pale" ni aina gani ya neno

  1. Kivumishi
  2. Kiwakilishi
  3. Kiunganishi
  4. kihisishi
  5. Kielezi
Chagua Jibu


10. "Kinyonga anatembea". Ukanushi wa sentensi hii ni upi?

  1. Kinyonga hakitembei
  2. Kinyonga hakutembea
  3. Kinyonga hajatembea
  4. Kinyonga haternbei
  5. Kinyonga hatatembea
Chagua Jibu


11. "Mama anapika lakini baba abapangamawe". Neno lakini limetumika kama aina gani ya neno?

  1. Kivumishi
  2. Kiwakilishi
  3. Kielezi
  4. Kitenzi
  5. Kiunganishi
Chagua Jibu


12. "Kiburi si maungwana". Neno "si" limetumika kama aina gani ya kitenzi

  1. Kikuu
  2. Kishirikishi
  3. Jina
  4. Kisaidizi
  5. Kitegemezi
Chagua Jibu


13. "Baba yangu ni mwenyekiti wa lopp". Neno "mwenyekiti ni nomino ya aina gani?

  1. Dhahania
  2. Kawaida
  3. Pekee
  4. Jumla
  5. Mguso
Chagua Jibu


14. Wingi wa neno chuma ni upi kati ya maneno yafuatayo?

  1. Machuma
  2. Mavyuma
  3. Vichuma
  4. Vyuma
  5. Michuma
Chagua Jibu


15. "Wanafunzi walitumiana salamu". Sentensi hii ipo katika kauli gani?

  1. Kutendeana
  2. Kutendana
  3. Kutendewa
  4. Kutendea
  5. Kutendeka
Chagua Jibu


16. Kinyume cha neno "elea" ni kipi?

  1. [buka
  2. Ibukia
  3. Zamia
  4. Zama
  5. Zamisha
Chagua Jibu


17. "Huyu mwanangu mpendwa". Neno lipi ni sahihi iii kukamilisha sentensi hiyo.

  1. ndiye
  2. ndio
  3. ndiyo
  4. ndie
  5. ndiwe
Chagua Jibu


18. "Mbwa ameonekana". Neno lipi ni sahihi kukamilisha tungo hiyo?

  1. aliyepotea
  2. aliopotea
  3. alipotea
  4. amepotea
  5. alivyopotea
Chagua Jibu


19. Hall ya kuwa na fedha au mall nyingi huitwaje?

  1. Ukachero
  2. Ukapa
  3. Ukata
  4. Ubahili
  5. Ukwasi
Chagua Jibu


20. Ni sentensi ipi inawakilisha kauli ya kutendwa?

  1. Nyumba imeharibiwa na mvua.
  2. Nyumba imeharibishwa na mvua.
  3. Nyumba imeharibika na mvua.
  4. Nyumba imeharibika kwa mvua.
  5. Nyumba imeharibiwa kwa mvua.
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256