STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2008

KISWAHILI 2008 

SEHEMU A

SARUFI

Katika swali la 1 - 15 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasiyakoya kujibia.

1. Neno lipi linakamilisha sentensi isemayo, "Humu . . alimoingia yule nyoka"

  1. ndiye
  2. ndio 
  3. ndiyo 
  4. ndimo 
  5. ndiko
Chagua Jibu


2. Badala ya kusema, "mimi sijambo". Ninaweza kusema, "mimi .. kamilisha sentensi hiyo kwa neno sahihi.

  1. wa afya 
  2. ahueni 
  3. heri
  4. buheri 
  5. mzima
Chagua Jibu


3. Ala kumbe! Kihisishi ni kipi kati ya yafuaatayo?

  1. Ameondoka 
  2. Leo 
  3. Ala kumbe
  4. Ala 
  5. Kumbe
Chagua Jibu


4. Kisawe cha neno kati ya yafuatayo?

  1. Hadharani 
  2. Mafichoni 
  3. Pembezoni
  4. Waziwazi 
  5. Kivulini
Chagua Jibu


5. Mtoto aliyepotea amepatikana. Hii ni aina ipi ya sentensi?

  1. Sahili
  2. Tegemezi
  3. Changamano
  4. Changamano
  5. Shurutia
Chagua Jibu


6. Yule msichana anaimba vizuri. Neno lililopigiwa mstari limetumika kama aina ipi ya maneno?

  1. Nomino 
  2. Kielezi 
  3. Kitenzi
  4. Kivumishi 
  5. Kiwakilishi
Chagua Jibu


7. Sentensi ipi kati ya zifuatazo ipo katika kauli halisi?

  1. Mimi siendi 
  2. Alisema haendi 
  3. Ameenda 
  4. Alisema hataenda
  5. Alisema anaenda
Chagua Jibu


8. Nomino inayotokana na kitenzi "Vaa" ni ipi?

  1. Nguo
  2. Valisha
  3. Kivalo 
  4. Kivazi 
  5. Vazi
Chagua Jibu


9. Neno lipi linakamilisha sentensi isemayo, Timu ya Taifa ingalicheza vizuri . mchezo

A. ingelishinda B. ingeshinda C. ingashinda

D. ingalishinda E. itashinda

Chagua Jibu


10. Siku ya Mei Mosi wafanyakazi walipita mbele ya Waziri Mkuu wakishikilia ......... yenye maneno ya kuhimiza kazi. Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?

  1. mabango 
  2. libango 
  3. kibango
  4. vibango
  5. bango
Chagua Jibu


11- "Nguo yangu imechafuka sana.” Wingi wa sentensi hii ni upi?

  1. Nguo yangu imechafuka sana 
  2. Nguo zetu zimechafuka sana
  3. Nguo yetu zimechafuka sana 
  4. Nguo zao zimechafuka sana 
  5. Nguo yetu zimechafuka sana
Chagua Jibu


12. Lipi kati ya maneno yafuatayo halina uhusiano na mengine?

  1. Ng'ombe 
  2. Mbuzi
  3. Simba 
  4. Chiriku
  5. Nyani
Chagua Jibu


13. Samaki, dagaa na nyama. Kwa neno moja huitwaje?

  1. Kitoweo 
  2. Mboga 
  3. Mchuzi
  4. Mlo 
  5. Chakula
Chagua Jibu


14. Sentensi isemayo, ”ltakapofika mchana .... kuondoka” inakamilishwa kwa usahihi na neno lipi kati ya yafuatayo?

  1. tuliruhusiwa
  2. tataruhusiwa
  3. tumeruhusiwa
  4. hurusiwa 
  5. tunaruhusiwa
Chagua Jibu


15. Kinyume cha neno "duni” ni kipi?

  1. Thamani
  2. Kidogo
  3. Hafifu
  4. Kikubwa 
  5. ?mara
Chagua Jibu


SEHEMU B

MSAMIATI

Katika swali la 16 - 25 andika herufiyajibu lililo sahihi katika karatasi yakoya kujibia.

16. Mzee Jumbe aliwapa wanae mavvaidha juu ya maisha yao. Neno lilipogiwa mstari lina maana gani?

  1. Mawazo 
  2. Urithi
  3. Maonyo
  4. Mahubiri
  5. Hotuba
Chagua Jibu


17. Mtu anayesimamia kazi za shambani huitwaje?

  1. Nokoa 
  2. Mnyapara 
  3. Msimamizi
  4. Kiongozi 
  5. Kiranja
Chagua Jibu


18. Pondamali ni kijana mwenye hila sana. Kisawe cha neno ”hila l'ni kipi?

  1. Hasira 
  2. Ulafi 
  3. Udanganyifu
  4. Ukorofi 
  5. Ukabila
Chagua Jibu


19. "Jioni bahari ilikuwa . kwa hiyo wavivu walivua samaki bila wasiwasi. Neno lipi linakamilisha sentensi hiyo kwa usahihi?

  1. kupwa 
  2. shwari 
  3. kavu
  4. Baridi
  5. joto
Chagua Jibu


20. Mama alijifunza kuendesha gari lakini bado hajafuzu. Neno "Hajafuzu” lina maana ipi kati ya zifuatazo?

  1. Hajajua kuendesha 
  2. Hajamaliza mafunzo hayo 
  3. Hajapata leseni 
  4. Hajahitimu mafunzo hayo
  5. Hatamaliza mafunzo haya
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256