SURA YA KWANZA

ALAMA ZA USALAMA KATIKA MAZINGIRA

Msamiati

  • Eksirei- aina ya mionzi yenye uwezo mkubwa wa kupenya katika vitu yabisi
  • Kilipuzi- kitu kinachoweza kulipuka kwa urahisi
  • Viuatilifu- kemikali zinazotumika kuua kufukuza au kuzuia viumbe wanaosababisha madhara kwa wanyama na mimea

Dhana ya alama za Usalama katika mazingira

  • Katika mazingira tunayoishi, zipo alama au michoro inayotoa ishara au tahadhari. Alama au michoro hiyo hujulikana kama alama za usalama.
  • Alama za usalama ni alama ambazo hutoa taarifa kuhusu hatari iliyopo kwenye vitu au mazingira.
  • Vilevile, alama hizo hutoa maelekezo ambayo hupelekea kulinda usalama wa vitu na viumbe hai katika mazingira.
  • Baadhi ya michoro au alama za usalama huongezewa maneno iii ziweze kutafsiriwa kwa urahisi.
  • Hata hivyo, michoro na alama nyingi hazina maneno, na watumiaji wa eneo husika hupaswa kuelewa maana ya michoro na alama hizo.
  • Alama za usalama hutumika kimataifa katika nchi zote duniani, na huwekwa kwenye vifaa kama vile chupa za dawa au kemikali.
  • Huwekwa pia kwenye vyombo vya usafiri kama vile mabasi, ndege, meli, boti au magari ya kubebea mafuta.
  • Vilevile, huwekwa kwenye majengo kuelekeza njia za kutokea wakati wa dharura, sakafu inayoteleza, vifaa vyenye kemikali au vinavyoweza kusababisha madhara.
  • Aidha, alama hizi huwekwa kwenye transfoma na kwenye nguzo za msongo mkubwa wa umeme.
  • Alama za usalama ni muhimu kwa sababu huwezesha kuchukua hatua zinazostahili wakati wa kutumia vifaa vyenye alama hizo.
  • Hutahadharisha pia kuepuka mazingira hatarishi, kwa mfano, kucheza au kupita chini ya nyaya zenye msongo mkubwa wa umeme.

Aina za alama za usalama

Zipo aina kuu nne za alama za usalama, ambazo ni alama za:

  1. Kuzuia au kukataza;
  2. Onyo au tahadhari;
  3. Lazima au amri; na
  4. Dharura.
  • Kila aina ya alama za usalama huwasilishwa kwa rangi na umbo maalumu. Rangi na maumbo ya alama hizi huongozwa na taratibu za kiusalama za kimataifa kama inavyobainishwa katika Jedwali namba 1.

Jedwali

Na

Aina za alama za usalama

Rangi

Maelekezo.

Sifa.

Mfano.

1

Alama za Nyekundu kuzuia au

kukataza

  1. Hatari
  2. Simama
  3. Zima
  4. Hama
  5. Hairuhusiwi kuingia kwa asiyehusika

Zina umbo la duara au pembe nne, picha nyeusi kwenye msingi mweupe na

kingo nyekundu. Baadhi ya alama hizi zirla mstari mwekundu wa

kiegema

C:UsersKYAMBODocumentsmaarifa 3png-transparent-turn-on-red-traffic-sign-u-turn-road-regulatory-sign-traffic-signs-text-trademark-logo.png

2

Alama za onyo au tahadhari

Njano.

  1. Kuwa makini
  2. Chukua tahadhari
  3. Hatari katika eneo jirani

Zina umbo la pembe tatu, picha nyeusi kwenye msingi wa nano na kingo nyeusi

C:UsersKYAMBODocumentsmaarifa 3isolated-warning-sign-high-voltage-260nw-1032558436.jpg

3

Alama za lazima au amri

bluu

Husisitizatabia

au vitendo fulani

Zina umbo la

duara, picha nyeupe kwenye

msingi wa bluu

C:UsersKYAMBODocumentsmaarifa 3download.png

4

Alama za dharura

Kijani.

  1. Mlango wa kutokea wa dharura
  2. Njia ya kutokea wakati wa hatari

Huduma ya kwanza au vifaa vya kujiokoa

Zina umbo la pembe nne (mstatili au mraba), picha nyeupe kwenye msingi wa kijani

au picha ya kijani ______

kwenye msingi
mweupe

C:UsersKYAMBODocumentsmaarifa 3images.png

  • Baadhi ya alama za usalama huweza kuoneshwa kwa rangi nyingine tofauti kulingana na kiwango cha madhara yanayoweza kutokea usipozingatia tahadhari hiyo.
  • Mfano, alama ya hatari huweza kuwa na rangi nyekundu, rangi ya machungwa au njano. Rangi nyekundu huonesha madhara makubwa sang ikifuatiwa na rangi ya machungwa na njano.
  • Alama ya hatari hutumika mahali ambapo kuna madhara makubwa ambayo husababisha majeraha makubwa au kifo endapo tahadhari haitachukuliwa.
  • Alama ya hatari yenye msingi wa rangi nyekundu na maandishi meupe hutumika endapo kuna mazingira ya hatari yanayoweza kusababisha madhara makubwa.

Tafsiri za alama za usalama

Alama za usalama hubeba ujumbe ambao hutoa tahadhari kwa walengwa. Ni vema kutambua alama hizo na tafsiri zake, iii kuepuka hatari au ajali zinazoweza kutokea kwa kutozingatia tahadhari iliyotolewa. Miongoni mwa alama hizo ni kama zinavyooneshwa kwenye Jedwali namba 2.

1. Hairuhusiwi kuingia

C:UsersKYAMBODocumentsmaarifa 3istockphoto-1083284330-612x612.jpg

Alama zinapatikana wapi?

Sehemu ambazo haziruhusiwi kuingia au kupita, mfano, maabara

Athari ya kutochukua tahadhari

Huweza kupata madhara ya kiafya endapo mtu ataingia au kupita

2. Hairuhusiwa kuvuta sigara

C:UsersKYAMBODocumentsmaarifa 3download.jpg

Alama zinapatikana wapi?

Kwenye vituo vya kujaza mafuta ya magari, kwenye ndege, kwenye migahawa, shule na katika maeneo mengine ya umma

Athari ya kutochukua tahadhari

Moto huweza kutokea mtu akivuta sigara sehemu hiyo. Husababisha madhara ya kiafya kwa mtu asiyevuta ambaye yupo karibu na mvutaji wa sigara.

Matumizi ya alama za usalama katika mazingira

Alama za usalama hutumika katika maeneo na vitu mbalimbali vilivyopo kwenye mazingira yetu, Miongoni mwa matumizi ya alama za usalama ni haya yafuatayo:

Kuonesha hatari

Kuna maeneo au vitu ambavyo huwekwa alama za usalama, iii kuonesha hatari ambayo mtu huweza kukutana nayo endapo hatachukua tahadhari. Kwa mfano, alama zinazotahadharisha kuwa kung mionzi ya eksirei, kemikali yenye kulipuka au mkondo unaopitisha umeme mkubwa. Alama hizi humfanya mtu achukue tahadhari anapokaribia mazingira hayo.

Kuepusha magonjwa

Alama za usalama hutumika kuonesha namna mtu anavyoweza kuepuka
magonjwa au kutoathiri afya yake akizingatia tahadhari iliyotolewa. Mfano, vitu vyenye alama ya vimelea vya magonjwa, kama vile mapipa ya taka za hospitali hutahadharisha kutovigusa. Alama hiyo huepusha magonjwa yanayosababishwa na vimelea.

Kuepusha ajali

Alama nyingine za usalama husaidia kuepusha ajali. Mfano, gari linalobeba mafuta huwa na alama ya usalama inayoonesha vitu vinavyoshika moto na kuwaka kwa haraka. Hivyo, matumizi ya alama hii husaidia kuepusha ajali za moto ambazo zingeweza kutokea.

Kutoa tahadhari na maelekezo

Alama nyingine hutahadharisha na kutoa maelekezo ya namna ya kutumia au kufanya kitu fulani kwa uangalifu. Kwa mfano, vitu vinavyovunjika kwa urahisi huwekewa alama ya maelekezo kumsaidia anayebeba kuwa mwangalifu. Baadhi ya vivatilifu vya kuua wadudu au magugu huwekwa alama ya sumu au hatari. Alama hizi humfanya mtumiaji kutumia vifaa vya kujikinga wakati wa kutumia kemikali hizo ill asidhurike. Vifaa hivyo ni pamoja na glovu, miwani, vazi maalumu au ovalori, buti na kofia ngumu. Vilevile, kwenye chupa za dawa za kupuliza za kuua wadudu na manukato huwekwa alama ya kushika moto. Hivyo, hutahadharisha kukaa mbali na vyanzo vya moto wakati wa kutumia vitu hivyo.

www.learninghubtz.co.tz

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256