FORM FOUR KISWAHILI NECTA 2019

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

MTIHANI WA KUHITIMU KIDATO CHA INNE

021          KISWAHILI

(Kwa watahiniwa Walioko na Wasiokuwa Shuleni)

Muda: Saa 3                            Alhamisi 07 Novemba 2019 mchana

Maelekezo

  1. Karatasi hii ina sehemu A, B na C zenye jumla ya maswali kumi na mbili (12).
  2. Jibu maswali yote katika sehemu A na B na maswali matatu (3) kutoka sehemu C.
  3. Zingatia maagizo ya kila sehemu na ya kila swali.
  4. Simu za mkononi na vitu vyote visivyoruhusiwa havitakiwi katika chumba cha mtihani.
  5. Andika Namba yako ya Mtihani katika kila ukurasa wa kijitabu chako cha kujibia.

SEHEMU A (Alama 15)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

1. Chagua herufi ya jibu sahihi katika vipengele (i) hadi (x), kisha andika herufi ya jibu hilo katika kijitabu chako cha kujibia.

(i) Neno lipi kati ya maneno haya linaweza kudokeza mtenda au mtendwa?

  1. Kiunganishi   
  2. Kivumishi
  3. Kihisishi 
  4. Kiwakilishi 
  5. Kielezi
Choose Answer :


(ii) Ni sentensi ipi haina kitenzi kisaidizi?

  1.  Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alikuwa mtiifu.
  2. Watoto wanatakiwa kulala mapema ili wawahi shuleni.
  3. Paka alikuwa anataka kula chakula cha mbwa.
  4. Juma alikuwa anasoma kitabu cha hadithi za mapenzi.
  5. Robert Kelly anataka kuja kutumbuiza mwezi Desemba.
Choose Answer :


(iii)  Ni sentensi ipi inawakilisha kikamilifu wahusika wa fasihi simulizi?

  1. Vitu, mahali, wanyama, binadamu, fanani na maleba.
  2. Hadhira, wanyama, maleba, binadamu na fanani.
  3. Hadhira, binadamu, wanyama, vitu, mahali na fanani. 
  4. Fanani, vitu, mahali, binadamu, maleba na wanyama.
  5. Wanyama, manju, binadamu, vitu, mahali na maleba.
Choose Answer :


(iv)  Bainisha seti ya maneno inayofaa kuingizwa kwenye kamusi kwa kuzingatia mpangilio wa alfabeti.

  1. Jabali, jadhibika, jabiri, jadi, jalada
  2. Jabali, jabiri, jadhibika, jadi, jalada
  3. Jabali, jadi, jadhibika, jalada, jabiri 
  4. Jabiri, jabali, jalada, jadi, jadhibika
  5. Jabali, jalada, jabiri, jadhibika, jadi
Choose Answer :


(v) Ni sifa ipi haitofautishi fasihi simulizi na fasihi andishi?

  1. Ukubwa 
  2. Uhifadhi
  3. Uwasilishaji
  4. Ukuaji
  5. Ueneaji
Choose Answer :


(vi) Jozi ipi ina vipengele sahihi vinavyounda umbo la ndani la kazi ya fasihi simulizi?

  1. Falsafa, muundo, ujumbe, wahusika
  2. Mandhari, msimamo, ujumbe, dhamira
  3. Ujumbe, mtazamo, migogoro, dhamira 
  4. Ujumbe, msimamo, dhamira, wahusika
  5. Lugha, mgogoro, falsafa, mtindo
Choose Answer :


(vii) "Ngombe zangu wanatoa maziwa mengi." Kosa lililojitokeza katika tungo hii ni lipi kati ya haya?

  1. Unyumbuaji wa maneno
  2. Udondoshaji wa herufi 
  3. Unyumbuaji wa maneno 
  4. Upatanisho wa kisarufi
  5. Uongezaji wa kiambishi
Choose Answer :


(viii)  "Serikali imeweka mikakati kabambe ili kupunguza umasikini."Neno "ili" katika sentensi hii ni aina gani ya neno?

  1. Kielezi        
  2. Kiunganishi
  3. Kiwakilishi 
  4. Kihisishi
  5. Kivumishi
Choose Answer :


(ix) Mpangilio sahihi wa vipashio vinavyounda lugha ya Kiswahili ni upi?

  1. Mofimu, kishazi, kirai, neno na sentensi.
  2. Mofimu, neno, kirai, sentensi na kishazi.
  3. Neno, kirai, Kishazi, sentensi na mofimu.
  4. Neno, mofimu, kirai, kishazi na sentensi. 
  5. Mofimu, neno, kirai, kishazi na sentensi.
Choose Answer :


(x) Ni jambo gani linalodhihirisha upekee wa kazi fulani ya kifasihi?

  1. Muundo wa kazi husika.
  2. Wahusika wa kazi husika. 
  3. Jina la kazi husika.
  4. Jina la mtunzi wa kazi husika.
  5. Mtindo wa kazi husika.
Choose Answer :


2. Oanisha maana za dhana za uandishi zilizo katika Orodha A kwa kuchagua herufi ya dhana husika katika Orodha B, kisha andika herufi husika katika kijitabu chako cha kujibia.

ORODHA A ORODHA B
  1. Kujieleza kwa lugha fasaha, mpangilio mzuri wa mawazo na kutumia misamiati.
  2. Kujenga fikra fulani katika kifungu cha maneno.
  3. Mpangilio mzuri wa mawazo unaoeleweka kwa mwandishi na msomaji.
  4. Kifungu cha maneno chenye kuelezea wazo maalumu, au sehemu ya wazo lililo katika mtiririko.
  5. Alama ya uandishi inayotenga maneno yaliyo katika orodha fulani.
  1. Mantiki 
  2. Mkato 
  3. Uandishi 
  4. Insha 
  5. Wazo
  6. Aya
  7. Kistari


View Ans


SEHEMU B (Alama 40)

Jibu maswali yote katika sehemu hii.

3. Taja njia zilizotumika kuunda maneno yafuatayo:

  1.  Amirijeshi
  2. View Ans


  3. Kiswahili
  4. View Ans


  5. Kifaru
  6. View Ans


  7. Chajio
View Ans


4.Andika nahau yenye maana sawa na tungo zifuatazo:

  1. Jumanne ni kijana mchoyo.
  2. View Ans


  3. Yule ni mropokaji sana.
  4. View Ans


  5. Malingumu ni mwizi.
  6. View Ans


  7. Mwalimu wetu ameoa.
View Ans


5. (a) Kwa kutumia njia ya mnyumbuliko, unda nomino mbili kwa kila kitenzi kifuatacho:

(i) Piga

View Ans


(ii) Lima

View Ans


(iii) Pika

View Ans


(iv) Cheza

View Ans


(b) Tunga tungo moja kwa kila kipengele (i) — (iv) ukizingatia viambajengo vyakila moja: 

(i) Kishazi tegemezi + Kishazi huru

View Ans


 (ii) Kishazi huru

View Ans


  (iii) Kishazi tegemezi

View Ans


  (iv) Kishazi huru + Kishazi huru

View Ans


6.  (a) Soma kwa makini sentensi (i) hadi (iv), kisha fafanua kwa pamoja vipengele vinne vinavyodhihirisha uhusiano baina ya Kiswahili na lugha za Kibantu. 

(i) Mtoto amelala (Kiswahili) 

View Ans


(ii) Mwana agonili (Kingoni) 

View Ans


(iii) Mwana yogonile (Kigogo)

View Ans


(iv) Omwana yanagila (Kihaya)

View Ans


(b) Kwa kutumia mifano na kutoa hoja mbili kwa kila moja, eleza kwa ufupi mafanikio ya lugha ya Kiswahili enzi za Waarabu katika:

(i)    Dini

View Ans


(ii)  Biashara

View Ans


7.  Kwa kutumia mifano kutoka katika riwaya ya Takadini na Watoto wa Mama Ntilie, eleza kwa kifupi mambo manne ya kufanana kati ya wahusika Sekai na Mama Ntilie kuhusu wasifu wao wa ndani.

View Ans


8.  Soma kifungu cha habari kifuatacho, kishajibu maswali yanayofuata:

Soni aliamka usingizini na kuendelea na safari yake. Awali alishtushwa na mitikisiko iliyotokea karibu na mbuyu. Hakujua yuko wapi lakini hakuchelewa kukumbuka nia ya safari yake. Aliukamata mkuki wake vizuri na ngao yake pia. Alipiga goti moja na kusimama hali akiuangalia mbuyu. Punde, aliwaona nyani wawili wakikimbilia nyasini. Wakasimama na kumtazama Soni. Naye alipoona hakuna hatari ya wanyama wakali, aliendelea na safari yake. Muda huo wa mchana ulikuwa salama kwani wanyama wakubwa walikuwa mapangoni mwao. Zaidi zilisikika sauti za panzi, nyenje na ndege tu waliojibizana kwa zamu.

Soni alipumzika kidogo kwa mara nyingine ili kumnyonyesha mtoto. Hata hivyo, vivuli virefu vilimkumbusha kuwa usiku ulikaribia. Lakini hakusikia wala kuona dalili yoyote ile iliyoonesha kuwa binadamu waliishi katika eneo hili. Bado hakuelewa ni wapi alipokuwa. Ni kosa gani alilofanya? Je, mwanawe hakuwa binadamu? Ni-kwewtofauti yake .ni_rangi-tu2 Hakuwa na vidole vya mikono na miguu vilivyomzidi baba yake. Macho yake na masikio pia yalikuwa sawa, aliyahesabu yote. Pale kila kitu kilipowekwa pamoja, mtoto alikuwa karibu sawa na wengine kuliko tofauti yake ya rangi tu. Sasa nvbona wanataka kumuua?

Soni alianza kukimbia kwa kasi kwani kama hangefika kijiji jirani, basi kutoroka kwake kungekuwa kazi bure. Punde si punde alishtushwa na mlio wa vipande vya miti vilivyovunjika. Soni alisimama akabana pumzi zake akisubiri sauti ile isikike tena. Huyo hakuwa mnyama mkali bali mtu aliyekusanya kuni. Upesi Soni aliharakisha upande ilikotoka sauti. Ghafla akamwona mzee mmoja akikusanya kuni. Alisogea kiasi ambacho kungetokea hatari angekimbia. Alimsalimia mzee yule. "Tafadhali kuwa mwema ili umsaidie mwanao aliyepotea," alisubiri atakavyojibiwa. Kwa sauti ile yule mzee alizunguka na kuinua shoka lake kama ishara ya kutisha. Punde alipogundua kuwa aliyeongea alikuwa ni mwanamke, alipata ahueni na kulishusha shoka lake chini. Wakati ule Soni alisita na kuamua kusimama. Tumaini alizinduka usingizini. Huenda alihisi shaka iliyomkumba mama yake, akaanza kulia.

Punde si punde, yule mzee alijiandaa kwa mashambulizi. Aliwaza kuna mtu nyuma ya yule mama. Iweje mwanamke mwenye mtoto mchanga aranderande msituni bila ya kuwa na mlinzi? Huenda anatumiwa na kijana imara aliyetaka kumuua. Wakati huo angefanyaje? Alikusanya kuni chache alizozipasua, akageuka ili aondoke. "Tafadhali usinitupe niliwe na wanyama wa usiku. Nisaidie! La, huwezi kunisaidia binti yako, basi msaidie mwanangu. Hajaonja maisha bado, na si vyema kufa sasa. Kilio mfululizo cha yule mtoto na maneno ya Soni vilimgusa yule mzee. Ingawa alisita, lakini hatimaye aligeuka nyuma. Kutokana na kauli yake, alihisi Soni alikuwa mgeni katika eneo hilo. Akaamua hata kama iweje, angemsaidia. Kwa hadhari kubwa aliwasogelea mama na mtoto wake. "Njoo mwanangu, tutakwenda kibandani kwangu."

Maswali

  1.  Pendekeza kichwa cha habari hii kisichozidi maneno matatu.
  2. View Ans


  3. Unafikiri kwa nini Soni alitoroka nyumbani kwake na kukimbilia msituni?
  4. View Ans


  5. Mwandishi wa habari hii anaichukuliaje jamii ya akina Soni?
  6. View Ans


  7. Kutokana na habari uliyosoma, eleza nafasi ya mwanamke katika jamii kwa kutoa hoja mbili.
View Ans


SEHEMU C (Alama 45)

Jibu maswali matatu (3) kutoka katika sehemu hii.

9.Wewe ni mshiriki wa shindano la uandishi wa insha lililoandaliwa na Baraza la Kiswahili la Taifa. Kaulimbiu ya shindano ni "Watoto zingatieni daima maonyo ya wazazi wenu". Kwa kutumia kauli mbiu hii, andika insha ya kisanaa isiyopungua maneno mia mbili (200) na isiyozidi maneno mia mbili hamsini (250), yenye kuishia na methali "Asiyesikia la mkuu huvunjika guu".

View Ans


ORODHA YA VITABU KWA SWALI LA 10-12

USHAIRI

Wasakatonge   -  M.S. Khatibu (DUP)

Malenga Wapya  - TAKILUKI (DUP) 

Mashairi ya Chekacheka  -  T.A. Mvungi (EP & D. LTD)

RIWAYA

 Takadini     -   Ben J. Hanson (MBS)

Watoto wa Mama Ntilie  -  E. Mbogo (H.P) 

Joka la Mdimu   -   A.J .Safari (H.P.)

TAMTHILIYA

Orodha   -    Steve Reynolds (MA)

Ngoswe Penzi Kitovu cha Uzembe - E. Semzaba (ESC)

Kilio Chetu  -  Medical Aid Foundation (TPH)

10. Kwa kutumia diwani mbili ulizosoma eleza jinsi taswira tatu kutoka katika kila diwani zilivyotumiwa na msanii kuwasilisha ujumbe kwa jamii.

View Ans


1l . "Waandishi wa kazi za fasihi huibua migogoro mbalimbali na kupendekeza masuluhisho ili kuelimisha jamii husika". Thibitisha kauli hiyo kwa kutoa hoja tatu kwa kila kitabu kutoka katika riwaya mbili ulizosoma.

View Ans


12. Kwa kutumia tamthiliya mbili ulizosoma, fafanua madhara yanayotokana na kukosekana kwa elimu ya jinsia kwa vijana kwa kutoa hoja tatu kutoka katika kila kitabu.

View Ans


Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256