STD VII SAYANSI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2015

2015 -SAYANSI

Chaguajibu sahihi kisha andika herufi yake kwenye karatariya kujibia.

1. Lipi kati ya makundi yafuatayo linawakilisha sifa za viumbe hai?

  1. Kufa, kula na kuona
  2. Kufa, kuzaa na kubadilika rangi 
  3. Kupumua, kuishi na kusikia 
  4. Kupumua, kuzaa na kutembea.
  5. Kujongea, kupumua na kuzaa.
Chagua Jibu


2. Mbegu chotara kwa wanyama na mimea ni bora kwa sababu gani?

  1. Hurefuka sana na hazihitaji mbolea.
  2. Hutoa mazao mengi na hustahimili magonjwa.
  3. Hukomaa haraka na hutoa mazao yenye uzito mkubwa. 
  4. Hazihitaji virutubisho na hustahimili magonjwa. 
  5. Hukomaa haraka na hazihitaji dawa.
Chagua Jibu


3. Lipi kati ya makundi yafuatayo ni sifa zinazotumika kutambua wanyama wa kundi la reptilia?

  1. Kutaga mayai, kuwa na damu baridi na kuishi majini. 
  2. Kutaga mayai, kuishi majini na kuishi nchi kavu.
  3. Kutaga mayai, kuwa na damu ya joto na kuishi nchi kavu.
  4. Kutaga mayai, kuwa na damu baridi na kupumua kwa kutumia mapezi.
  5. Kutaga mayai, kupumua kwa kutumia ngozi na kuishi majini.
Chagua Jibu


4. Damu huchukua oksijeni na kutoa kabondayoksaidi kupitia:

  1. Viribaehewa 
  2. Kuta za mapafu
  3. Koromeo
  4. Kapilari
  5. Pua
Chagua Jibu


5. Kukosekana kwa chanikiwiti katika mmea huweza kusababisha:

  1. mmea kukosa madini joto
  2. mmea kushindwa kusanisi chakula
  3. majani ya mmea kukauka 
  4. majani ya mmea kuwa njano
  5. maj ani ya mmea kupukutika.
Chagua Jibu


6. Fototropizimu ni kitendo cha mmea kuota kuelekea kwenye:

  1. mwanga 
  2. kani ya mvutano 
  3. maji 
  4. giza
  5. kemikali.
Chagua Jibu


7. Sehemu ya chembe hai inayohusika na kutawala shughuli zote za chembe hai huitwa:

  1. saitoplazimu 
  2. vakuoli
  3. kloroplasti 
  4. kiwambo cha seli
  5. nyukliasi
Chagua Jibu


8. Kielelezo kifuatacho kinaonyesha viumbe hai wenye sumu isipokuwa

  1.    
  2.    
  3.    
  4.    
  5.    
Chagua Jibu


9. Tendo Ia mimea kusafirisha maji kutoka kwenye mizizi hadi kwenye majani huitwa:

  1. osmosis 
  2. difyusheni 
  3. msukumo
  4. mgandamizo 
  5. mjongeo
Chagua Jibu


10. Ni tezi ipi kati ya zifuatazo huratibu utendaji wa tezi zingine zote katika mwili wa binadamu?

  1. Kongosho. 
  2. Pituitari
  3. Thairoidi
  4. Adrenali 
  5. Parathairoidi
Chagua Jibu


11. Sehemu ya kike ya ua inayohusika na uzazi ni:

  1. stameni 
  2. staili 
  3. ovari
  4. Petali
  5. Sepali
Chagua Jibu


12. Tofauti kati ya tunda na mbegu ni: 

  1. Mbegu ina tunda.
  2. Tunda huota.
  3. Tunda lina kotiledoni mbili. 
  4. Mbegu huota. 
  5. Mbegu haziliwi.
Chagua Jibu


13. Mambo muhimu kwa ajili ya afya na uhai ni:

  1. kucheza mpira wa miguu, kuoga, kufua nguo na kula sana.
  2. kula, kuwa msafi, kupumzika na kucheza.
  3. kufanya mazoezi, kula chakula bora, kupumzika na kuwa msafi.
  4. kula mayai, kuburudika, kulala na kusafisha mazingira.
  5. kuoga, kula na kulala.
Chagua Jibu


14. Vyakula vyenye kabohaidreti huwezesha mwili:

  1. kuhimili magonjwa
  2. kuwa na joto
  3. kukua kwa haraka 
  4. kuwa na nguvu 
  5. kuwa mwororo
Chagua Jibu


15. Kati ya yafuatayo ni yapi magonjwa yasiyoambukiza?

  1. Malaria, mafua na kisukari.
  2. Pumu, kisukari na kipindupindu.
  3. Kichocho, safura na matende
  4. Kuhara, homa ya matumbo na pumu
  5. Pumu, kifafa na tetekuwanga.
Chagua Jibu


16. Mapumziko baada ya kazi ni muhimu kwa sababu gani?

  1. Mwili hupoa. 
  2. Mwili hutulia.
  3. Mwili hurejesha nishati. 
  4. Mwili hufanya shughuli nyingine.
  5. Mtu hupata fursa ya kulala.
Chagua Jibu


17. Magonjwa yanayozuilika kwa kutumia chanjo ni :

  1. Pumu, kifaduro, malaria na kipindupindu 
  2. Kifua kikuu, malaria, pumu na surua
  3. Surua, dondakoo, kifua kikuu na kifaduro
  4. Malaria, surua, kifua kikuu na kipindupindu
  5. Dondakoo, kifua kikuu, UKIMWI na surua
Chagua Jibu


18. Wakazi wa Mlalo hula maharage, nyama na wali kwa afya zaidi wanahitaji kuongeza:

  1. samaki 
  2. mboga za majani
  3. kuku
  4. mkate
  5. kunde
Chagua Jibu


19. Kipi kati ya vifuatavyo kinaweza kupungua mwilini kwa kushiriki katika michezo na mazoezi?

  1. Sukari 
  2. Protini 
  3. Sumu
  4. Uchafu 
  5. Fati
Chagua Jibu


20. Kipi kati ya vifuatavyo siyo njia sahihi ya kujikinga na ugonjwa wa malaria?

  1. Kufyeka nyasi 
  2. Kufukia madimbwi
  3. Kutumia chandarua 
  4. Kupuliza dawa
  5. Kuchoma moto taka
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256