STD VII MAARIFA_JAMII ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2010

MAARIFA YA JAMII 2010

URAIA, JOGRAFIA NA HISTORIA 

SEHEMU A

Chagu jibe hullo sahihi kisha andika herufi inayohusika mbele ya kilo swali katika karatasi ya kujibia uhyopewa.

1. Ukoo ni muungano wa:

  1. familia zinazokaa karibu 
  2. familia nyingi zenye asili moja
  3. familia nyingi zilizo rafiki 
  4. baba, mama na watoto.
  5. familia zilizoungana kufanya kazi pamoja.
Chagua Jibu


2. Utamaduni maana yake ni

  1.  imani, desturi, mila na miiko ya jamii ya watu
  2.  kuimba na kucheza kwa pamoja
  3.  namna ya kufanya matambiko katika jamii
  4.  desturi na mila za jamii Fulani
  5.  utaratibu wa kuishi
Chagua Jibu


3. Kiongozi wa serikali ngazi ya kata ni

  1. Diwani 
  2. Afisa mtendaji wa kata
  3. Mwenyekiti wa kata
  4. Katibu kata
  5. Afisa mifugo wa kata
Chagua Jibu


4. Ili Afrika ijitegemee kiuchumi inahitaji

  1. misaada toka nje 
  2. Ongezeko kubwa la watu
  3. sayansi na teknolojia 
  4. mikopo ya masharti nafuu
  5. wawekezaji wa kiafrika.
Chagua Jibu


5. Lengo kuu la kuanzishwa kwa Jumuiya ya Madola lilikuwa

  1.  kupata makoloni zaidi barani Afrika
  2.  kuimarisha uhusiano baina ya Uingereza na nchi ilizozitawala
  3.  kuoongeza kiasi cha malighafi zilizokuwa zinahitajiwa na wazungu.
  4.  kuwaachia watumwa ambao bado walikuwa hawajawa huru
  5.  kumfanya malkia wa Uingereza aogopwe na ulimwengu mzima.
Chagua Jibu


6. Mahakama inayotoa hukumu ya kesi za mauaji ni

  1. Mahakama ya mwanzo 
  2. Mahakama ya wilaya
  3. Mahakama kuu 
  4. Mahakama ya hakimu mkazi
  5. Mahakama ya Rufaa
Chagua Jibu


7. Nchi zinazopakana na Tanzania upande wa kusini ni

  1.  Msumbiji na Malawi
  2.  Msumbiji na Zimbabwe
  3.  Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo na Malawi
  4.  Burundi na Malawi
  5.  Rwanda na Malawi
Chagua Jibu


8. Nini tofauti kati ya nyota na sayari?

  1.  Nyota humweka wakati sayari hazimweki
  2.  Nyota zinatoa mwanga mweupe, wakati sayari hutoa mwanga wa rangi ya njano.
  3.  Sayari huonekana mchana lakini nyota huonekana usiku tu.
  4.  Nyota hazina mwanga wakati sayari zina mwanga
  5.  Sayari zote zina viumbe hai wakati nyota hazina viumbe hai
Chagua Jibu


9. Bonde la ufa limegawanyika sehemu ya Mashariki na Magharibi katika nchi gani?

  1. Kenya 
  2. Uganda 
  3. Tanzania 
  4. Burundi 
  5. Ethiopia
Chagua Jibu


10. Vifuatavyo vilikuwa ni vyama vya ukombozi kusini mwa Afrika isipokuwa

  1. ANC 
  2. PAC 
  3. SWAPO 
  4. KANU 
  5. UNITA
Chagua Jibu


11. Mkusanyiko wa shughuli zinazohusisha wafanyabiashara na walaji au watumiaji huitwa 

  1. Soko 
  2. duka
  3. Bidhaa 
  4. mteja 
  5. fedha
Chagua Jibu


12. Bara la pili kwa ukubwa ulimwenguni ni

  1. Asia 
  2. Afrika 
  3. Australia
  4. Amerika ya Kaskazini 
  5. Amerika ya kusini
Chagua Jibu


13. Rais wa kwanza wa Bunge la Umoja wa Afrika lililoanzishwa Machi 2004 ni

  1. Dr. Salim Salim 
  2. Dr. Emek Anyauko
  3.  Mh. Getrude Mongela 
  4. William Erek 
  5. Peter Omu
Chagua Jibu


14. Mtanzania anaruhusiwa kupiga kura katika uchaguzi mkuu anapofikia umri wa miaka 

  1. 15 
  2. 25 
  3. 40 
  4. 21 
  5. 18
Chagua Jibu


15. Hapo awali mabara yote yalikuwa yameshikana na kuwa bara moja lililojulikana kama 

  1. Andes 
  2. Pangaea
  3. Australia 
  4. Eurasia 
  5. Antaktika
Chagua Jibu


16. Tabaka la ozone huweza kuharibiwa na

  1.  kuongezeka kwa gesi ya oksijeni
  2.  Kuongezeka kwa gesi ya haidrojeni kwenye anga
  3.  moshi wenye kemikali unaotoka viwandani na kwenye magari
  4.  kupungua kwa gesi ya kaboni daioksaidi kwenye anga
  5.  vumbi linalosambaa angani kutokana na shughuli za uchimbaji wa madini
Chagua Jibu


17. Rhoda anachemsha maji ya kunywa kila siku kwa sababu maji yaliyochemshwa

  1. ni safi na salama 
  2. yana ladha nzuri
  3. hukata kiu haraka 
  4. huua wadudu walioko katika matumbo yetu
  5. huwa na virutubisho vingi
Chagua Jibu


18. Lengo mojawapo la michezo shuleni ni

  1. kutumia viwanja vya shule vizuri
  2. kuleta umoja na ushirikiano
  3. kuwapa zawadi washiriki
  4. kutambua shule zisizo na viwanja vya michezo
  5. kupata wachezaji wa kulipwa
Chagua Jibu


19. Serikali za mitaa zina aina ......za Halmashauri

  1. moja 
  2. nne 
  3. tano 
  4. tatu 
  5. sita
Chagua Jibu


20. Idadi kubwa ya wakimbizi katika bara la Afrika inasababishwa na

  1. umaskini katika nchi nyingi za Afrika
  2. migogoro ya kifamilia 
  3. miundo mbinu duni
  4. upungufu wa ajira 
  5. machafuko ya kisiasa
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256