STD VII KISWAHILI ONLINE SELF NECTA TEST FOR YEAR 2016

Katika swali la 1 — 20, weka kivuli katika herufiyajibu lililo sahihi.

1.  "Wachache wamehamia Boro". Katika sentensi hiyo "Wachache" limetumika kama aina gani ya neno?

  1. Kivumishi
  2. Kielezi     
  3. Kiwakilishi
  4. Kitenzi 
  5.  Kiunganishi
Chagua Jibu


2.         Alimwita nyumbani kwake kwa dhamira ya kumpa karo ya shule. Neno "dhamira" lina maana ipi?

  1. Dhamana 
  2. Madhumuni
  3. Thumuni  
  4.  Dhumuni 
  5. Dhamini
Chagua Jibu


3.         Kauli ipi inaonesha hali ya kutendewa?

  1. Tumechimba visima vyetu. 
  2.  Tunachimbisha kisima chetu. 
  3. Tulichimbiwa kisima chetu. 
  4. Tumechimba kisima chetu.
  5. Tutachimba kisima chetu.
Chagua Jibu


4.         Katika vifungu vya maneno vifuatavyo, kifungu kipi kipo katika kauli taarifa?

  1. Unataka kuondoka lini? 
  2. Alitaka kukuuliza unaondoka lini. 
  3. Ni lini wewe utaondoka? 
  4.  Aliuliza, utaondoka lini?
  5. Aliuliza kuwa ataondoka lini?
Chagua Jibu


5.         Mwenyekiti hakufika mkutanoni leo. Kitenzi "hakufika" kipo katika hali gani?

  1. Mazoea  
  2. Kuendelea  
  3. Timilifu
  4. Matarajio 
  5.  Kanushi
Chagua Jibu


6.         "Wapiganaji wetu walipowasili visiwa vya Comoro walishangiliwa kwa   Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?

  1. hofu   
  2.  mzaha  
  3. shangwe
  4. mayowe
  5. dhihaka
Chagua Jibu


7.         Mawaziri wote wa Baraza la Mapinduzi waliapishwa. Neno "wote" limetumika kama aina gani ya neno?

  1. Nomino  
  2.  Kiwakilishi 
  3. Kitenzi
  4. Kivumishi   
  5. Kiunganishi
Chagua Jibu


8.         Babu amemhamishia yule mbuguma kwenye zizi kubwa. Neno "mbuguma" lina maana

  1. Mbuzi dume anayelima  
  2. Ngombe dume anayelima
  3. Kondoo jike aliyezaa 
  4. BWombe jike anayelima
  5. Ngombe jike anayeendelea kuzaa
Chagua Jibu


9.         "Chama kimeteka nyara sera ya serikali." Wingi wa sentensi hiyo ni upi?

  1. Vyama vimeteka nyara masera ya serikali. 
  2.  Vyama vimeteka nyara sera ya serikali. 
  3. Vyama vimeteka nyara serikali.
  4.  Vyama vimeteka sera za serikali.
  5. Vyama vimeteka nyara visera vya serikali.
Chagua Jibu


10.     Nyumba ya ndege huitwaje?

  1. Mzinga 
  2. Kiota 
  3. Korongo
  4.  Banda 
  5.  Shimo
Chagua Jibu


11.     "Wanafunzi hodari watapewa zawadi". Sentensi hiyo ipo katika wakati gani?

  1. Ujao 
  2.  Timilifu 
  3. Uliopita   
  4.  Mazoea 
  5. Uliopo
Chagua Jibu


12.     Maji yamejaa "pomoni" Neno "pomoni" ni aina ipi ya neno?

  1. Nomino  
  2.  Kiwakilishi   
  3. Kielezi
  4. Kihisishi  
  5. Kivumishi
Chagua Jibu


13.     Kati ya maneno "Sherehi, Sherehe, Shamrashamra, Hafla, Tafrija" neno lipi halihusiani na mengine?

  1. Sherehi  
  2. Sherehe 
  3.  Shamrashamra 
  4. Hafia 
  5. Tafrija
Chagua Jibu


14.     Neno lipi kati ya maneno yafuatayo lina maana sawa na "thubutu"?

  1. Ufidhuli  
  2. Ujasiri 
  3. Umahiri 
  4. Ukakamavu 
  5. Utashi
Chagua Jibu


15."Kuzua kizaazaa" ni msemo wenye maana gani?

  1. Ushabiki   
  2. Upendeleo
  3. Malumbano
  4. Masikitiko  
  5. Majungu 
Chagua Jibu


16. Mtu anayetafuta kujua jambo fulani kwa kuuliza maswali huitwaje?

  1. Mawazo
  2. Mbeya
  3. Mfitini
  4. Mdadisi
  5. Mjuaji 
Chagua Jibu


17. Neno Mchakato lina maana ya mfululizo wa................

  1. Mawazo
  2. maoni
  3. shughuli
  4. safari
  5. fikra
Chagua Jibu


18. Neno lipi kati ya yafuatayo lina maana sawa na neno shehena

  1. roda
  2. furushi
  3. mizigo
  4. bidhaa
  5. robota
Chagua Jibu


19. Mtu aliyezaliwa na wazazi wa rangi mbalimbali huitwaje?

  1. Albino
  2. Mkimbizi
  3. mhamiaji
  4. chotara
  5. mzawa
Chagua Jibu


20.      Baada ya miaka minne Kalunde ... ...... mafunzo yake ya udaktari. Ni neno lipi linakamilisha sentensi hiyo?

  1. aliitimu 
  2.  alihimidi
  3.  aliitimisha
  4. alihitimu 
  5.  halihitimu
Chagua Jibu


  BOFYA HAPA KUPAKUA APP YA LEANING HUB
ILI KUFUNGUA MTIHANI MZIMA  




Try Another Test | 
Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256