?> EXAM SERIES EXAM
STANDARD SEVEN ANNUAL SERIES

OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOGIA

MTIHANI WA MWISHO WA MWAKA DARASA LA SABA

SAYANSI NA TECHNOLOJIA

MUDA:1:30                                                             

JINA_____________________________________SHULE_________________________

Chagua herufi ya jibu sahihi 

  1.               Ipi kati ya zifuatazo sio kazi ya mfumo wa upumuaji?
  1.             Usafirishaji wa oksijeni kwenye tishu
  2.             Kutoa joto na maji mwilini
  3.             Mbadilishano wa hewa mwilini
  4.             Kuzungumza, kupiga yowe na kuimba
  1.               Mbadilishano wa gesi hutokea kwenye……….
  1.             Koromeo
  2.             Pua
  3.             Trakea
  4.             Aliveoli
  1.               Vinyweleo na unyevunyevu unaoopatikana katika pua, husaidia……………
  1.             Mbadilishano wa hewa
  2.             Kunasa vijidudu na uchafu
  3.             Kusafirisha hewa kwenda kwenye mapafu
  4.             Kupooza hewa inayoingia mwilini kupitia puani
  1.               Unapotoa hewa nje ya mapafu misuli katika mbavu…………….
  1.             Hulegea
  2.             Hutanuka
  3.             Hukaza
  4.             Hukatika
  1.               Upumuaji umegawanyika katika hatua mbili ambazo ni mbadilishano wa gesi katika mapafu Pamoja na……….
  1.             Kuingiza na kutoa hewa kwenye damu
  2.             Kupitisha hewa kwenye koromeo
  3.             Kuingiza na kutoa hewa kwenye mapafu
  4.             Mapafu na kifua kusinyaa


6. Damu huchukua oksijeni na kutoa kabondayoksaidi kupitia:

  1.             Viribaehewa 
  2.             Kuta za mapafu
  3.             Koromeo
  4.             Kapilari
  5.              Pua
  1.                Zifuatazo ni kasoro za milango ya fahamu isipokuwa…………
  1.              Uziwi
  2.               Kutokuona mbali
  3.               Anemia
  4.              Kutokuona karibu
  1.                Mlango wa fahamu unaofanya kazi ya kuhisi baridi au joto ni………..
  1.              Jicho
  2.               Sikio
  3.               Ulimi
  4.              Ngozi
  1.                Kazi ya sikio la nje la binadamu ni………….
  1.              Kukusanya mawimbi ya sauti
  2.               Kutafsiri mawimbi ya sauti
  3.               Kutawanya mawimbi ya sauti
  4.              Kusisimua sikio la ndani
  1.            Mpangilio wa vifupa vitatu katika sikio la kati ni kama ufuatao………….
  1.              Fuawe, nyundo, kikuku
  2.               Kikuku, nyundo, fuawe
  3.               Nyundo, kikuku, fuawe
  4.              Nyundo, fuawe, kikuku
  1.            Ubongo umegawanyika katika sehemu tatu ambazo ni…………
  1.              Serebramu, medula oblongata na ugwemgongo
  2.               Serebelamu, ugwemgongo na medula oblongata
  3.               Serebramu, serebelamu na medulla oblongata
  4.              Medulla oblongata, serebramu na ugwemgongo
  1.            Neva inayopeleka taarifa kutoka kwenye pua kwenda kwenye ubongo inaitwa………..
  1.              Neva ya olifaktori
  2.               Neva ya optiki
  3.               Neva ya akaustika
  4.              Neva ya oditori
  1.            Neva inayotoa taarifa kutoka kwenye retina kwenda kwenye ubongo inaitwa……………
  1.              Neva ya oditori
  2.               Neva ya optiki
  3.               Neva ya akaustika
  4.              Neva ya olifaktori
  1.            Yafuatayo ni  aina ya mazoezi ya mwili, isipokuwa……….
  1.              Kutembea
  2.               Kucheza mpira
  3.               Kuruka Kamba
  4.              Kusikiliza muziki
  1.            Mpira wa miguu ni mchezo unaofaa Zaidi kwa kundi la………..
  1.              Wajawazito
  2.               Watoto wachanga
  3.               Wazee wa miaka 70
  4.              Vijana
  1.            Mlo kamili ni chakula chenye………….
  1.              Virutubisho vya mafuta, kabohaidreti na protini, wanga na hamirojo
  2.               Virutubisho vya protini, kabohaidreti, mafuta, vitamini na madini
  3.               Virutubisho vya vitamini, madini na protini, wanga na hamirojo
  4.              Virutubisho vya vitamini, kalisi, potasiamu, chuma na zinki
  1.            Madini yafuatayo ni muhimu kwa ajili ya kuimarisha mifupa na meno………
  1.              Madini ya chuma
  2.               Madini ya magnesiamu
  3.               Kalisi
  4.              Potasiamu
  1.          Bapa ni sehemu ya…………
  1.             Cherehani
  2.             Baiskeli
  3.             Blenda
  4.             Gurudumu la gari
  1.          Mota katika blenda hubadilisha nishati ya umeme kuwa nishati ya………..
  1.             Joto
  2.             Makaniki
  3.             Mwanga
  4.             Joto na mwanga
  1.          Nishati katika mashine ya kusaga nafaka husafirishwa kutoka kwenye mota hadi kwenye kinu kwa kutumia…………
  1.             Mkanda
  2.             Gurudumu na ekseli
  3.             Nyenzo
  4.             Mteremko
  1.          Sehemu ya kutumbukiza ufunguo katika kitasa ina mashine sahili aina ya………….
  1.             Nyenzo
  2.             Springi
  3.             Skrubu
  4.             Gurudumu na ekseli

22. Tazama alama kwenye kielelezo kifuatacho kwa makini, kisha zipe majina kwa kuzingatia zilivyopangwa kutoka upande wa kushoto.

  1.             Kapasita, dynamo, seli kavu, swichi, betri
  2.             Swichi, glopu, kikinza, kapasita, seli kavu 
  3.             Glopu, kapasita, seli kavu, kikinza, betri 
  4.             Kikinza, glopu, swichi, seli kavu, kapasita
  5.              Swichi, kikinza, glopu, seli kavu, kapasita.


23. Kipi kati ya vifuatavyo hakipitishi mkondo wa umeme?

  1.             Mpira 
  2.             Bati
  3.             Shaba
  4.             Chuma 
  5.              Zebaki


24. Alama zifuatazo zinatumika katika sakiti ya umeme. Je, ni alama ipi inawakilisha kikinza?

  1.             
  2.             
  3.             
  4.             
  5.              

25. Mzunguko kamili wa . . . . . .  huitwa sakiti

  1.             waya
  2.             betri
  3.             soketi
  4.             umeme
  1.          Makundi ya alama za usalama ni………..
  1.             Alama za kuzuia, alama za onyo, alama za lazima na alama za dharura
  2.             Alama za dharura, alama za binafsi na alama hatarishi
  3.             Alama za amri, alama za kuzuia na alama za kukubali
  4.             Alama za hospitali, alama za onyo, alama za barabarani na alama za angani
  1.          Alama za lazima au amri huoneshwa kwa rangi gani?
  1.             Njano
  2.             Nyekundu
  3.             Bluu
  4.             Kijani
  1.          Alama hii inawakilisha nini?

 

  1.             Sumu
  2.             Inashika moto
  3.             Inamomonyoa na kuunguza
  4.             Inadhuru
  1.          Mojawapo kati ya maneno yafuatayo, hayawekwi kwenye viuatilifu vya kuua wadudu.
  1.             Inashika moto
  2.             Sumu au hatari
  3.             Maji yasiyo salama
  4.             Inakereketa
  1.          Unapotumia vitu vinavyohatarisha macho, unapaswa kuchukua tahadhari gani?
  1.             Kuvaa barakoa
  2.             Kufunga kitambaa usoni
  3.             Kuvaa kofia
  4.             Kuvaa miwani
  1.            Nini kinachosababisha kitu kuelea au kuzama kwenye maji?
  1.              Urefu wa kitu
  2.               Upana wa kitu
  3.               Densiti ya kitu
  4.              Kimo cha kitu
  1.            Kama densiti ya kitu ni ndogo kuliko ya maji, nini kitatokea ukidondosha kitu hicho kwenye maji?
  1.              Kitazama
  2.               Kitaelea
  3.               Kitazama na kuelea
  4.              Kitazama au kuelea
  1.            Densiti ya kitu ni tungamo ya kizio kimoja cha…………..
  1.              Uzito
  2.               Urefu
  3.               Kina
  4.              Ujazo
  1.            Nyambizi inazama baharini ikiwa densiti yake ni…….
  1.              Ndogo kuliko densiti ya maji
  2.               Kubwa kuliko densiti ya maji
  3.               Sawasawa na densiti ya maji
  4.              Kubwa au ndogo kuliko densiti ya maji
  1.            Moto wa daraja gani hutokana na kuungua kwa vitu yabisi kama nguo na karatasi?
  1.              Daraja D
  2.               Daraja C
  3.               Daraja A
  4.              Daraja F
  1.            Tindikali ni dutu lenye kemikali ambayo hutumika kubadili karatasi ya litimasi………
  1.              Nyekundu kuwa njano
  2.               Bluu kuwa nyekunu
  3.               Kijani kuwa bluu
  4.              Nyekundu kuwa bluu
  1.            Ni kwa namna gani unaweza kuzuia vitu vya chuma visioate kutu?
  1.              Kuviweka kwenye maji
  2.               Kuvipaka majivu
  3.               Kuviongeza oksijeni
  4.              Kuvipaka rangi
  1.            Nyongo ina tabia mbili muhimu, ambazo ni…………
  1.              Kubadili karatasi ya litimasi ya bluu kuwa  nyekundu na kuua vijidudu
  2.               Kubadili karatasi ya litimasi bluu kuwa nyekundu na kuvunja mafuta mwilini
  3.               Kubadili karatasi ya litimasi nyekundu kuwa bluu na kuvunja mafuta ya wanyama mwilini
  4.              Kubadili karatasi ya litimasi ya bluu kuwa nyekundu na kukinga magonjwa
  1.            Ni gesi gani hutumika wakati wa kuzima moto?
  1.              Kabonidayoksaidi
  2.               Oksijeni
  3.               Haidrojeni
  4.              Naitrojeni

40. Chembe ndogo kabisa za maada zinazounda elementi na zinazohusika katika kutengenezz bondi za kikemikali huitwa:

  1.               molekyuli      
  2.                elektroni      
  3.                protoni
  4.               atomi                                     
  5.                nyutroni

41. Mwanga hupinda unapopita kutoka

  1.               Ncha ya Kaskazini kwenda Kusini      
  2.                media moja kwenda nyingine
  3.                Ncha ya Kaskazini kwenda Mashariki 
  4.               Magharibi kwenda Mashariki 
  5.                Kaskazini kwenda Magharibi

SHEMU YA B. CHUNGUZA PICHA IFUATAYO KISHA JIBU MASWALI

 

Andika majina ya sehemu zifuatazo:

  1. A
  2. B
  3. C
  4. D
  5. E
  6. F
  7. G
  8. H

LEARNINGHUBTZ.CO.TZSTANDARD SEVEN SAYANSI EXAM SERIES 40

Download Learning
Hub App

For Call,Sms&WhatsApp: 255769929722 / 255754805256